Huu ni mtaro ambao umeziba na maji hayaendi,na watu kutupa uchafu ndani yake kama unavyoonekana.
Juu ya huo mtaro kuna mgahawa wa chakula,ambao watu wanautumia kwa mahitaji ya chakula.
Kama picha inavyoonesha maji machafu yakiwa yametuama,na uchafu ukiwa umetupwa ndani yake.
Ikifika mchan watu hukaaa hapo juu na kupata chakula hii ni hatari kwa afya ya binadamu.

Ukifika maeneo ya makumbusho nyuma ya Jengo la Tigo maarufu mtaa wa kwa bwela kwa wauza viatu maarufu kwa wakina dada,hali ya usafi katika mitaro ya eneo hili ni ya kutisha ingawa imezungukwa na maofisi makubwa kama kampuni za simu na mabenki mengi.Dj sek blog ilifanya utafiti makini na kujione hali ya mitaro hiyo ikiwa katika hali mbaya kiusafi,Kwanza mitaro hiyo imeziba hivyo kusababisha maji kutuama na kupelekea maji hayo kuvunda na kuwa rangi ya njano.

Kingine cha kushangaza zaidi ndani ya mitaro hiyo watu hutumia kama sehemu ya kutupia uchafu kama mifuko ya rambo,makopo n,k.Jambo lingine ambalo ni la hatari zaidi ni eneo la juu ya mitaro hiyo kuna mgahawa ambao unauza chakula kwa ajili ya matumizi ya binadamu.Jambo la kujiuliza je watoa huduma katika mgahawa huo hawaoni hali hiyo ya uchafu ambao upo kwenye eneo lao?na je hawaoni kwamba ni hatari kwa afya za binadamu wanaokula eneo hilo?Tulipojaribu kuwauliza walikuwa hawana majibu ya kutoa.Tunaomba serikali ya mtaa wa makumbusho walione hili na kulishughulikia na sio kukaa ofisini mpaka magonjwa yatokee ndipo tuanze kuhangaika.
PICHA NA HABARI KWA HISANI YA DJ SEK BLOG

photo ,

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika PICHA|MAKTABA 
Dar es Salaam.Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo inaanza kikao chake cha siku mbili ikitarajiwa kujadili masuala mazito, hasa misukosuko iliyokikumba katika siku za karibuni.
Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika ilisema kikao hicho kitakachofanyika Dar es Salaam kitapokea, kujadili na kufanya uamuzi wa masuala mbalimbali ikiwamo hali ya siasa na ripoti ya fedha.
“Suala mojawapo litakuwa kujadili mihutasari ya mikutano iliyopita na yatokanayo na mikutano hiyo, taarifa ya hali ya siasa na ripoti ya fedha,” ilisema taarifa hiyo ya Mnyika, ambaye yuko ziara ya kikazi huko Uturuki.
Pia utajadili mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba, taarifa ya utekelezaji wa Programu ya Chadema ni Msingi na shughuli za kanda na taarifa ya utekelezaji wa Mpango Mkakati kuhusu maboresho.
Chadema katika mawimbi makali
Miongoni mwa mambo ambayo yanatarajiwa kujadiliwa katika kikao hicho ni mustakabali wake katika kipindi hiki ambacho kinapita katika mawimbi makali kutokana na kuibuka kwa malumbano ya waziwazi baina ya viongozi wake waandamizi na pia kusimamishwa kwa baadhi ya viongozi wa mikoani.
Matukio ya karibuni yanajumuisha malumbano kati ya Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kuhusiana na masuala ya posho, kusimamishwa kwa Mwenyekiti wa Chadema wa Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba, kuvunjwa kwa uongozi wa Mkoa wa Mara na pia kuondolewa kikaoni kwa Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda.
Wafuatiliaji wa mambo ya siasa watakuwa wanakitazama kikao hiki kama fursa ya kuweka sawa mambo ili kiendelee kutoa ushindani kwa chama tawala.
Alipoulizwa kama matukio ya hivi karibuni yatajadiliwa katika kikao hicho, Mnyika alikataa kuingia kwa undani na badala yake alisema taarifa zitatolewa baada ya kikao.
“Niko nje ya nchi, mengine utapewa majibu kesho (leo) kwa yale ambayo yatakuwepo katika taarifa zitakazowasilishwa. Yale ambayo hayatakuwepo utajulishwa pia iwapo hayatajadiliwa,” alisema Mnyika.
Zitto na Lema
Zitto na Lema waliingia katika vita ya maneno mwanzoni mwa Novemba kuhusiana na masuala ya posho ya vikao.
Vita hiyo ilianzishwa na Lema katika kikao cha wabunge wiki iliyopita aliposema kuwa Zitto anafanya unafiki kukataa posho.
Lema alimtuhumu Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kwamba anakataa posho za vikao bungeni, lakini anapokea posho nyingi kutoka mashirika mbalimbali ya kijamii nchini.
Lema aliweka tuhuma hizo kwenye Mtandao wa Jamii Forum huku akisema suala hilo halihitaji vikao vya chama kulijadili isipokuwa vyombo vya habari na hususan, mitandao ya kijamii kwani hata Zitto hutumia mitandao hiyo.
Akijibu hoja hizo, Zitto alisema tangu siku nyingi alikwisha piga marufuku kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kupokea posho kutoka taasisi au mashirika yanayosimamiwa na kamati hiyo.
Alisema tangu alipokuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma(POAC), alipiga marufuku posho na pia aliwahi kuwashtaki Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) wabunge wanaochukua posho kutoka taasisi za Serikali.
Ripoti kuhusu Zitto mtandaoni
Zitto pia alipata msukosuko mwingine baada ya kusambazwa ripoti inayoitwa ‘Taarifa ya Siri ya Chadema’ iliyomtuhumu kuwa alikuwa anashirikiana na CCM na viongozi wa Idara ya Usalama wa Taifa kuhujumu chama hicho.
Ripoti hiyo inayodaiwa kuwa iliandaliwa na Idara ya Upelelezi ya Chadema, ilieleza kuwa Zitto alikuwa akipokea fedha kutoka kwa maofisa wa usalama na kuzisambaza kwa makada wengine wa chama hicho ili wafanye kazi ya kukihujumu.
Hata hivyo, Chadema kupitia kwa Mnyika ilitoa taarifa kupinga vikali suala hilo.
CAG kukagua ruzuku
Pia, Zitto aliingia katika malumbano na chama chake baada ya kutuhumu vyama vya siasa kuwa hesabu zake hazikaguliwi na CAG.
Chadema ilipinga vikali madai hayo na kueleza kuwa imekuwa inatumia taasisi binafsi kufanya kazi hiyo.
Mwigamba, Shibuda na uongozi Mara
Suala jingine linalotazamiwa kujadiliwa katika kikao hicho ni kusimamishwa kwa Mwigamba na Baraza la Uongozi Kanda ya Kaskazini ambako kulizuka vurugu kiasi cha kunyang’anywa kompyuta mpakato (laptop) baada ya kudaiwa alikuwa anasambaza taarifa za kuhujumu chama hicho.
Suala lake linasubiri uamuzi wa kikao cha Kamati Kuu kama lile la kuvunjwa kwa uongozi wa Chadema wa Mara.
Pia kitendo cha Baraza la Kanda ya Ziwa Mashariki kumtimua Shibuda kwa madai kwamba halina imani naye nacho kina uwezekano mkubwa wa kujadiliwa. Chanzo: MWANANCHI

photo ,



Katika hali ya kuonyesha kwamba wafanyabiashara wa eneo la kariakoo hawataki wala kusikia kuhusu mashine za T.R.A,Wafanyabiashara hao wameamua kufunga mabango katikati ya mitaa yakiwa na ujumbe wa kupinga matumizi ya mashine hizo.
Leo ni siku ya pili kwa wafanyabiashara hao kugoma kufanya biashara,Swali la msingi je Serikali inaonaje hali hii ya wanainchi kukosa huduma?na pia huu ni mkoa wa nne sasa baada ya Mbeya,Morogoro na Mtwara.PICHA NA DJ SEK

photo ,

Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operatin humbly accepting his appointment as a new Chairperson for the Commonwealth Ministerial Action Group (CMAG), a meeting that was held today at the Bandaranaike Memorial International Conference Hall (BMICH) in Colombo, Sri Lanka. 
The Commonwealth Ministerial Action Group in session during their meeting today held at the Bandaranaike Memorial International Conference Hall (BMICH) in Colombo, Sri Lanka. 
Minister Membe (2nd left) and Hon. Prof. G.L. Peiris, Sri Lankan External Affairs Minister reviewing Presidential election report on Maldives from the Commonwealth team of observers.


Hon. Minister Membe (right), congratulates his counterpart Sri Lankan External Affairs Minister Hon. Prof. G.L. Peiris (left),for his country as a host of the Commonwealth Heads of Government Meeting (CHOGM) and for the heartfelt hospitality throughout the weeklong meetings. 
The Sri Lankan External Affairs Minister  Hon. Prof. G.L. Peiris congratulates Hon. Minister Bernard Membe for been elected as a new CMAG Chairperson. 
Mr. Kamalesh Sharma (left), Commonwealth Secretary-General congratulates Hon. Minister Membe. 
Hon. Samura M. W. Kamara, Sierra Leone Minister for Foreign Affairs and International Cooperation congratulates Hon. Minister Membe. 
Minister Membe (right), in a discussion with Ms. Mmasekgoa Masire-Mwamba (center), the Commonwealth Deputy Secretary-General and Ambassador Peter Kallaghe (left), High Commissioner of the United Republic of Tanzania in London, with accreditation to the United Kingdom, to the Republic of Ireland and to the Commonwealth.
Hon. Minister Membe gets congratulations from representative of the Cyprus Foreign Affairs Minister (left) and from the representative of the New Zealand Foreign Affairs Minister.
Hon. Minister Membe, who is a new CMAG Chairperson, in a photo with Ms. Mmasekgoa Masire-Mwamba (left), the Commonwealth Deputy Secretary-General and a representative of the Guyana Foreign Affairs Minister (right). 
Hon. Minister Membe (2nd right), in a group photo with Ambassador Kallaghe (2nd left), together with Foreign Service Officers Mr. Amos Msanjila (left) and Ms. Eva Ng'itu (right), from the Tanzania Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation. 
Hon. Minister Membe (center), in a photo with Ambassador Kallaghe (left) and Ambassador Celestine Mushy, Director of the Department of Multilateral Co-operation.
Foreign Service Officer Ms. Eva Ng'itu congratulates Hon. Minister Membe. 
Foreign Service Officer Mr. Amos Msanjila congratulates Hon. Minister Membe. 
Communication Officer Ms. Tagie Daisy Mwakawago congratulates hon. Minister Membe for his appointment as a new CMAG Chairperson.
Hon. Minister Membe (left), held discussion with Ambassador Kallaghe (2nd left), Prof. Severine Rugumamu (2nd right) and Ambassador John William Herbert Kijazi (right) High Commissioner of the United Republic of Tanzania in India with accreditation to the Democratic Socialist Republic of Sri Lanka.  Minister Bernard K. Membe (MP) was unanimously elected Chairperson of the Commonwealth Ministerial Action Group on the Harare Principles (CMAG) in Colombo, Sri Lanka today.
Congratulations to Ms. Eva Ng'itu and Mr. Amos Msanjila for a job well done!
Foreign Minister Bernard Membe elected Chair of CMAG

By TAGIE DAISY MWAKAWAGO
Colombo, Sri Lanka

Tanzania Foreign Minister Bernard K. Membe (MP) was unanimously elected Chairperson of the Commonwealth Ministerial Action Group on the Harare Principles (CMAG) in Colombo, Sri Lanka today.

“We appoint you as our new Chairperson because of your strong institutional of knowledge and active mind,” said Hon. Samura M. W. Kamara, Sierra Leone Minister for Foreign Affairs and International Cooperation.  He said that the decision to elect Tanzania was easy, hoping that Tanzania will continue to spearhead CMAG’s values during her tenure. 

The eight group members of CMAG comprised of Commonwealth countries of Cyprus, India, Sri Lanka, Solomon Islands, Pakistan, Guyana, New Zealand and Sierra Leone expressed their confidence with Tanzania Foreign Minister Membe for his experience and wisdom.  Tanzania sums up the total nine group members of CMAG.

The Commonwealth Ministerial Action Group also elected Hon. Murray McCully, Foreign Minister of New Zealand as a Vice-Chair.

Speaking as a new CMAG Chair, Hon. Membe said that he appreciated tremendously the unanimous support received from fellow members.  “I am truly humbled by your decision to elect me as your new Chair.  I assure you of my unwavering commitment in protecting the core groundwork that CMAG stands for,” said Minister Membe.

The Ministers also jointly agreed the removal of Maldives from CMAG’s formal agenda, after receiving an update from the Commonwealth observers that the Presidential elections held this week in that country were declared credible and peaceful. Earlier this week CMAG had agreed to table Maldives on the Group’s formal agenda pending free and fair presidential elections in the country.

In a joint statement issued after their meeting, the Ministers congratulated the people of Maldives for showing their firm commitment to democracy, and for exercising their franchise in record numbers.  “We welcomed the successful conclusion of the presidential election and noted the interim statement of the Commonwealth Observer Group, which stated that the election had been ‘credible and peaceful’, noted the CMAG statement. 

Commenting on Sri Lanka as host of the Commonwealth Heads of Government Meeting, Minister Membe congratulated the country for their hospitality and commitment in restoring normalcy.  “You have demonstrated good leadership and endurance despite the turbulences you had faced in the past,” said Minister Membe.

On his part, Sri Lankan External Affairs Minister Prof. G.L. Peiris said that hosting CHOGM had enabled foreign representatives to witness his country emerging from the shadow of war conflicts.  “This is a true characteristic of our Sri Lankans for their resilience and ability to bounce back,” said Prof. Peiris.

Minister Membe has been in Sri Lanka for the past three days participating in the Foreign Ministers side-meetings as a preparatory meeting of the Commonwealth Heads of Government Meetings (CHOGM).  President Kikwete led the Tanzania delegation and participated in the Heads of State meetings from 15-17 November here in Sri Lanka. 

photo ,

Ujenzi wa Barabara za Kisasa ijini Dar Es Salaam, Kazi inaendelea,sehemu hizi zitatumika kama vituo vya kupandia na kushushia abiria mara ujenzi wa barabara za kisasa utakapokamilika,

photo



Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride maalum kabla ya kulihutubia Bunge mjini Dodoma .
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kwenye kitabu cha Wageni kwenye Ofisi ya Spika wa Bunge,Mh. Anne Makinda (kushoto) huku Waziri Mkuu,Mh. Mizengo Pinda akishuhudia.
Spika wa Bunge Anna Makinda akimaribisha Rais Kikwete kulihutubia Bunge.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma.
Rais Wa Zanzibar Dr.Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal wakufuatilia hotuba ya Rais Kikwete kwa makini.
Baadhi ya Wabunge na Mawaziri wakifatilia Hotuba ya Mh. Rais.


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Anna Makinda akimsindikiza Rais Kikwete nje ya Bunge baada ya kulihutubia mjini Dodoma.
Rais wa Muungano wa Jamhuri ya Tanzania ,Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein,Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakiwa katika picha ya Pamoja na Wabunge Baada ya Rais Kulihutubia Bunge mjini Dodoma.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiteta na kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Mhe.Freeman Mbowe baada ya Rais kulihutubia bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma.
Spika Mstaafu Pius Msekwa, Jaji Mkuu Othman Chande na Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal wakimpongeza Rais Kikwete baada ya kulihutubia Bunge mjini Dodoma.Picha na Freddy Maro.IKULU.

photo ,



Ndugu Wanahabari,

NILIPOKUWA katika ziara ya bara la Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba 2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

 “Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu) kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema.

Ripoti hiyo ilinihusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola 250,000 za Marekani kupitia kwenye akaunti yake binafsi.

Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imenifadhaisha, kunisikitisha na kunikasirisha.

Taarifa hii iliibuliwa katika kipindi ambacho nilikuwa safarini kutetea haki za Watanzania na Waafrika ambao utajiri wao wa rasilimali unafaidiwa na watu wachache waliohifadhi mali katika nje za nje na pia kupigania makampuni ya mataifa tajiri yalipe kodi stahiki katika nchi zetu.

Pengine lengo la ripoti hiyo lilikuwa ni kutaka kunipoteza kutoka katika nia na dhamira yangu ya dhati ya kutaka Watanzania wafaidike na utajiri wao. Muda ambao watunzi wa ripoti hiyo waliamua kutoa taarifa yao unazua maswali mengi kuliko majibu.

Nafahamu kwamba mimi ni mwanasiasa ambaye nimekuwa mlengwa (target) wa mashambulizi kutoka kwa makundi mbalimbali ya wanasiasa na vikundi vyao. Kama mwanasiasa, niko tayari kupokea changamoto zozote zinazokuja na uanasiasa wangu.

Hata hivyo, ambacho sitakubali ni kwa watu kutumia jina langu na uanasiasa wangu kunichafua mimi binafsi na watu wengine wasiohusika kwa sababu ya kutaka kutimiza malengo yao ya kidhalimu.

Raia huyo wa Kijerumani tayari amekana kuhifadhi fedha zangu. Kwa maelezo yake kwa baadhi ya viongozi wa Chadema amekana kuwa na akaunti inayotajwa na amekana pia kuwepo nchini Ujerumani katika siku na wakati uliotajwa kwenye ripoti hiyo.

Ripoti hiyo imemtaja pia mtu kama Dk. Charles Kimei, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB ikidai kwamba nilikutana naye na alishiriki kwenye igizo hilo la kunipa fedha.

Niseme mapema kwamba tangu kuzaliwa kwangu sijawahi hata mara moja kukutana na Dk. Kimei popote pale ndani au nje ya nchi. Kumuingiza mtu ambaye amejenga jina lake kwenye taaluma ya kibenki kwa sababu tu ya lengo ovu la kumchafua Zitto Zuberi Kabwe si uungwana bali ni unyama.

Kutokana na uchafuzi huu wa wazi dhidi ya taswira yangu binafsi na watu wengine walioingizwa kwenye mkumbo huu, nimeandika rasmi kwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Wilbrod Slaa kumwomba athibitishe kwamba kinachoitwa Taarifa ya Siri ya Chadema ni kweli ni taarifa ya chama au kiikanushe ili niweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa hekaya hiyo.

Cha ajabu, nimepokea ujumbe wa kutishiwa maisha kutoka kwa mtu anayejiita Theo Mutahaba na kuahidiwa KUPOTEZWA endapo nitaendelea na jitihada zangu za kupambana na ufisadi na kutafuta haki kwa Watanzania wote pasipo kujali tofauti zao za kiitikadi, kikanda, kikabila na kidini.

Natarajia kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wote ambao wamehusika na utungaji na uenezi wa taarifa hii. Nitahakikisha kwamba wahusika wanatafutwa na kufunguliwa mashitaka stahiki ya upotoshaji na kuchafuana.

Ni matarajio yangu kwamba wale wenye mapenzi mema na Tanzania, mimi binafsi na utawala wa sheria, wataelewa nia yangu ya kutafuta haki katika suala hili.
Nimeamua kujitolea maisha yangu kwa ajili ya Watanzania na kama alivyopata kusema Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela; “Struggle Is My Life.”

Forward Ever, Backward Never- Kwame Nkrumah

Zitto Kabwe (Mb)
10/11/2013

photo ,


  Baadhi ya Wanajumuiya ya Watazania waishio Mjini Seattle – Washington Nchini Marekani ambao walikuwa katika tafrija ya pamoja na Ujumbe wa Kiserikali wa Zanzibar uliokuwa mjini humo kushiriki Mkutano wa 15 wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wenye asili ya Afrika wa Mji Huo ukiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
  Baadhi ya Wanajumuiya ya Watazania waishio Mjini Seattle – Washington Nchini Marekani ambao walikuwa katika tafrija ya pamoja na Ujumbe wa Kiserikali wa Zanzibar uliokuwa mjini humo kushiriki Mkutano wa 15 wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wenye asili ya Afrika wa Mji Huo ukiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
  Baadhi ya Wanajumuiya ya Watazania waishio Mjini Seattle – Washington Nchini Marekani ambao walikuwa katika tafrija ya pamoja na Ujumbe wa Kiserikali wa Zanzibar uliokuwa mjini humo kushiriki Mkutano wa 15 wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wenye asili ya Afrika wa Mji Huo ukiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
  Baadhi ya Wanajumuiya ya Watazania waishio Mjini Seattle – Washington Nchini Marekani ambao walikuwa katika tafrija ya pamoja na Ujumbe wa Kiserikali wa Zanzibar uliokuwa mjini humo kushiriki Mkutano wa 15 wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wenye asili ya Afrika wa Mji Huo ukiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
 Najisikia raha kupiga picha ya pamoja na wajukuu zangu. Alijikuta akitamka maneno hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif mara baada ya kuwahutubia Wanajumuiya ya Watanzania waishio Mji wa Seattle Nchini Marekani kwenye tafrija aliyoandaliwa yeye na ujumbe wake.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwaasa Wanajumiya ya Watanzania wanaoishi Seattle kukumbuka hatma ya maisha yao ya baadaye kwa kuwekeza nyumbani.
  Mtoto Hanan Masoud Kayanda wa familia za Wanajumiya ya Watanzania wanaoishi Seattle akimuuliza swali Balozi Seif kuhusu masuala ya Elimu Zanzibar ambalo lilijibiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Nd. Abdulla Mzee Abdulla aliyekuwemo pia kwenye ujumbe wa Zanzibar uliozuru Mji huo wa Kifahari.
  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akipokea zawadi maalum kutoka kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Seattle Nd. Yona Isimika kwenye tafrija aliyoandaliwa na Ujumbe wake Mjini Seattle. Kati  kati yao ni Meneja Mkuu wa Benki ya Watu wa Zanzibar Limited { PBZ } Juma Amour Mohammed.
 Balozi Seif akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wana kamati ya maandalizi ya Tafrika aliyoandaliwa  yeye na ujumbe wake ya Jumuiya ya Watanzania waishio Seattle
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed hakuwa mbali katika kupiga picha ya pamoja na baadhi ya wanajumuiya ya Watanzania wanaoishi Seattle Nchini Marekani. Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
------------------------------------------------
Watanzania waishio na kuendesha maisha yao Nchini Marekani wameawa kuwa makini katika kuutumia  vyema muda wao wa maisha Nchini humo kwa kufikiria  mbinu za kujiwekea mitaji itakaowajengea hatma njema hapo baadaye endapo watafikia maamuzi ya kurejea kuishi nyumbani siku zijazo.
Nasaha hizo zimetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akizungumza na Wanachama wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi katika Mji wa Seattle ndani ya Jimbo la Washington kwenye tafrija maalum iliyoandaliwa na wana jumuiya hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Ramada Tukwila Mjini Seattle.
Balozi Seif alisema wapo baadhi ya Watanzania  waliobahatika kupata fursa na nafasi nzuri za kuendesha maisha katika Mataifa mbali mbali ya nje hasa  ya ulaya lakini wengi kati yao wameishia kuwa na maisha mabovu kwa kukosa kujiwekea misingi mizuri.
Alisema tabia ya kuendelea na kuendekeza starehe sambamba na matumizi ya kifahari kwa msingi wa kutaka sifa hutoa sura mbaya kwao lakini kinachoumiza zaidi ni kile kizazi chao kinachowategemea.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaomba wana Jumuiya hiyo ya Watanzania wanaoshi Mjini Seattle kuzingatia na kuheshimu sheria na taratibu za nchi wanayoishi  ili kulinda desturi na ukarimu walionao.
Amewapongeza wana jumuiya hiyo ya Watanzania wanaoishi Mjini Seattle kwa umoja na ushirikiano waliokuwa nao bila ya mgongano na ubaguzi wa uzawa ambao ndio utanaowasaidia katika kuimarisha mila na silka zao.
“ Ukweli sifa tulizokuwa nazo sisi Watanzania hatufanani na wenzetu wa mataifa mengine . Hivyo Utanzania wetu ni vyema tukauendeleza kwa kusaidiana na ofisi za balozi zetu zilizo  karibu “. Alisisitiza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
Akijibu baadhi ya maswali alioulizwa na Wanajumuiya hiyo ya Watanzania waishio Mjini Seattle Balozi Seif aliwatoa hofu wanajumiya hao kwa kuwaeleza kwamba Zanzibar na Tanzania kwa ujumla hivi sasa inaendelea kuwa shwari licha ya vituko vinavyotokea katika baadhi ya wakati hasa vile vilivyokuwa vikiwatia hofu wananchi vya kumwagiwa watu tindikali.
Alieleza kwamba Serikali iko makini katika kuhakikisha vitendo vya uvunjaji wa amani havipewi nafasi na tayari vyombo vya ulinzi vinaendelea na operesheni za kuwasaka watu wenye tabia kama hizo zinayotishia maisha ya Jamii.
Akijibu swala la operesheni kimbunga iliyowakumba watu waliokuwa wakiishi kinyume na taratibu za uhamiaji Nchini Tanzania Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema Serikali iliamua kufanya operesheni hiyo baada ya kugundua  wahamiaji haramu ndio wanaohusika na masuala ya ujambazi Nchini.
Alifahamisha kwamba watu wote walioondoshwa Nchini Tanzania kupitia operesheni Kimbunga hiyo wamebainika kutokuwa na kibali jambo ambalo ni kosa kwa  mujibu wa mfumo na taratibu za uhamiaji Kimataifa.
Hata hivyo Balozi Seif alifafanua kwamba Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuheshimu haki za Binaadamu haijamkataza mtu wa nchi yoyote Duniani kuishi Tanzania endapo atazingatia sheria za Nchi zilizopo.
“ Serikali imelazimika kuwa makini katika kulinda usalama wa wananchi baada ya kugundua kwamba wengi wa wahamiaji haramu ndio waliokuwa wakihusika katika masuala ya ujambazi na matukio ya hatari hapa Nchini “. Alisema Balozi Seif.
Wakitoa salamu zao kwa wanajumiya hao Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Mh. Nassor Ahmed Mazrui  wamewashauri wanajumuiya hao kuzitumia fursa za mitaji zilizopo nchini humo kwa kuanzisha miradi Nchini Tanzania.
Mawaziri hao walisema mitaji hiyo ambayo fedha zake hazina masharti makubwa zinaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa ajira hasa kwa vijana pamoja na kuongeza vipato vyao vitakavyopunguza umaskini.
Walieleza kwamba wanajumiya hayo  ni vyema wakaitumia Diasfora wakielewa kwamba Tanzania ni yao na kwame bila ya wao hakutakuwa na mgeni atakayeweza kuweka misingi ya kuimarisha uchumi wa taifa.
Mapema Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Mjini Seattle  Jimboni Washington Nchini Marekani Nd. Yona Isimika alisema jumuiya yao iliyoanzishwa mwaka 2008 hivi sasa ina karibu wanachama Mia Nne.
Nd. Yona alisema Jumuiya yao iliyolenga kuuendeleza Utamaduni, Mila na Silka zao za Kitanzania iko katika mchakato wa kubadilisha katiba ili ikidhi matihaji yao hasa wakati wanapopatwa na matatizo.
Mwenyekiti huyo wa Jumuiya ya Watanzania waoishi Seattle Washington alipongeza Ujumbe huo wa Zanzibar ulioongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa hatua yake ya kukutana nao ikiwa ni ugeni wa mwanzo tokea kuanzishwa kwa jumuiya hiyo mwaka 2008.
  
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
11/11/2013.
 

photo ,