Gidabuday,W.F.Mratibu wa mashindano Hayo.
 
Tanzania inatimiza miaka 30 tangu kumpoteza kiongozi wake shupavu aliyefariki kwaajalimbaya ya gari Aprili 12 1984 mkoani Morogoro.

Si mwingine bali ni aliyekuwa Waziri Mkuu katika seriakali ya awamu ya kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine aliyezaliwa 1938 wilayani Monduli mkoani Arusha.

Tanzania itaadhimisha miaka 30 ya kifo cha Sokoine, ni kwa kukumbuka mema yote aliyoyafanya kiasi kwamba hadi leo anakumbukwa.

Tanzania pia mwaka huu inasherehekea maadhimisho ‘Jubilee’ ya miaka 50 tangu nchi zetu mbili za Tanganyika na Zanzibar ziungane.


Tanzania pia leo hii inaandaa historia nyingine tena ‘Katiba Mpya’ huu ni mwaka wa historia ambayo haipatikani kwingine Afrika kama si duniani.

Mimi kama mratibu wa mbio hizo ‘Race Director’ ninapenda kuwaomba wabunge wa bunge maalum la katiba watenge siku hiyo muhimu ya Sokoine Day kuja Monduli kusherehekea na watanzania wenzao ili wapate ile ‘Original Spirit’ waliyokuwa nao viongozi wetu.

Bilashaka watarudi Dodoma na Baraka za mzalendo halisi, Baraka ambazo zitawapa nguvu wabunge ili wawe na maridhiano katika maamuzi na hatima ya katiba mpya.

Kutakuwa nambioza Half Marathon yenye maana kamili ya “Mini Marathon” na pia kutakuwa na mbio za Kilomita 2 kwa wanafunzi pamoja na wakubwa maana philosophy ya michezo ni kwamba hakuna umri maalu! ‘Sports for All
 

Mwisho ninawatakia heri na safari njema kuelekea Monduli; “KUWA MZALENDOSAMBAZA UPENDO”.

Kwa Maelezo zaidi bofya hapa : Wazalendo 25 Blog

photo ,

Mwanasheria Amani Mwaipaja (Mwenye Shuka la Kimasai) akiwa na baadhi ya Washiriki wa mafunzo ya Wasaidizi wa sheria ndani ya wilaya Mpya ya Gairo. Wasaidizi hao wamepewa mafunzo ya siku tano.

photo

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi (Mb), (Mwenye kaunda suti nyeusi) akisalimiana na Makamanda wa JWTZ mara baada ya kupokelewa na Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Luteni Jenerali Samuel Ndomba (Aliyesimama kulia kwa Mhe. Waziri) muda mfupi kabla ya Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania,
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili kwenye Kikosi cha Komando kuanza ziara yake ya kujionea hali na utimamu wa vikosi vya JWTZ Mkoani Morogoro.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea taarifa ya Utawala na Utendaji kivita kutoka kwa Mkuu wa Kikosi cha Komando wakati wa ziara yake.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipewa maelezo kwa kutumia mchoro kuonesha mzunguko mzima wa maeneo atakayotembelea katika kikosi cha Komando.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia kupitia kilengeo maalum kinachotumiwa kwenye silaha na makomando kulengea shabaha.
Makomando wakimuonesha Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (hayuko pichani) mapigano bila shilaha wakati wa ziara yake.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia mapambano ya kareti, taikondo na judo yaliyokuwa yakioneshwa na makomando wa JWTZ (Hawamo pichani).
Komando wa JWTZ akionesha uwezo wa kukwepa mapigo ya risasi za adui kwa kupita juu ya mapigo hayo kwa kutumia kamba na kisha kuendelea na jukumu alilopewa.
Kamanda wa Kikosi cha Uhandisi wa Medani akitoa taarifa ya Utawala na Utendaji Kivita kwa Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (Hayupo pichani) mara baada ya Kikosi hicho kutembelewa.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifafanua maeneo kadha ambayo Wahandisi Medani wa JWTZ wamefanya kazi nzuri kurejesha miundombinu ya reli, barabara na madaraja hata pale ambako Mamlaka za Kiraia zimekuwa na maoni kuwa kazi hizo zingehitaji muda mwingi zaidi.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo kuhusu baadhi ya mitambo mipya ya kutengeneza barabara katika Kikosi cha Uhandisi Medani.


Picha/habari na Luteni Kanali Juma Nkangaa Sipe, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Ulinzi na JKT

photo ,