Pichani ni Jengo litakalojengwa jijini Dar es salaam na litagharimu Dola za kimarekani milioni 77,kutakuwa na hoteli ya hadhi ya Nyota Tano, Ofisi za Biashara, kutakuwa na Sehemu ya kuegesha magari, jengo hili litatakuwa kivutio kwa Wawekezaji na Utalii.
(23 Juni 2014)
 Baadhi Malori na Vifaa vingine vya kutendea kazi vikiwa tayari kuahiria ujenzi huu unaanza mara moja baada ya zoezi la uwekaji wa jiwe la msingi kukamilika.

 Mama Maria Nyerere akiwasili kwenye sherehe ya uwekaji jiwe la msingi wa ujenzi wa jengo la Malimu Nyerere Foundation Square
 Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mheshimiwa Benjamini Mkapa akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu Ndugu Cleopa Msuya wakati wa shughuli za uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa jengo refu la ghorofa la Mwalimu Nyerere Foundation.
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (kushoto) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (kulia) kwa pamoja wakifunua kitambaa kuashiria kuwekwa jiwe la msingi katika eneo litakapojengwa jengo la Taasisi ya  Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
  Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (kushoto) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (kulia) wakijippongeza baada ya kuweka jiwe la msingi katika eneo litakapojengwa jengo la Taasisi ya  Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (katikati) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (wa pili kulia) kwa pamoja  wakimwaga mchanga kuashiria kuanza kwa ujenzi jengo la Taasisi ya  Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam,Kulia ni Balozi wa China nchini Tanzania Lu Youqing na Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akibadilishana mawazo na Profesa Shivji pamoja na Wazee wengine wakati wa shughuli za uwekaji wa jiwe la msingi wa Ujenzi wa jengo la Mwalimu Nyerere Foundation Square.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku akihutubia wakati wa Uwekaji wa jiwe la msingi wa jengo la Mwalimu Nyerere Foundation Square.

Picha ya Pamoja baada ya zoezi la uwekaji wa jiwe la Msingi kukamilika.
(Picha na Adam Mzee)

photo , ,

DSC_0217
Baadhi ya washiriki wa mashindano ya resi za Ngalawa wakijiandaa tayari kwa kuanza mashindano hayo katika shamra shamra za tamasha la 17 la ZIFF 2014 linaloendelea visiwani Zanzibar.(Picha na Zainul Mzige wa MOblog).

NGALAWA zote 11 zilizoingia majini kukamilisha mzunguko wa saa mbili wa resi za ngalawa mjini Zanzibar zilimarisha mashamshamu hayo bila najali na timu tatu zilipewa zawadi za ushindi.
Resi za Ngalawa kama zinavyojulikana ni utamaduni halisi wa visiwa vya pemba na Unguja na ni sehemu ya tamasha kubwa la filamu la kimataifa la Zanzibar ambalo linaendelea visiwani hapa.
Kwa wale waliozaliwa maeneo ya bara, resi hizi zilikuwa kivutio kikubwa kwao kutokana na maandalizi yanayofanywa kabla ya kuingia majini na dau kunyanuliwa.
Wakati dau limenyanyuliwa, maji yamekuwa yakichotwa ama ndani ya Ngalawa au nje katika bahari kumwagia tanga katika hali inayoelezwa kuliimarisha katika ukinzani wa upepo.
“mbio za Ngalawa ni kipimo kikubwa cha Uzanzibari wetu na kila mwaka ZIFF huhitimisha utashi wake wa kuwa na tamasha la nchi za jahazi kwa kuwa na mbio za ngalawa” alisema mshehereshaji Muslim Nassoro Abdalla katika shamrashamra zilizofanyika ufukweni kandoani mwa hoteli ya Tembo.
DSC_0235
Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (mwenye t-shirt ya njano) akupiliza Kipenga kuashiria kuanza kwa mashindano hayo yaliyofanyika kwenye fukwe za Hoteli ya Tembo visiwani Zanzibar.

Muslim ambaye alisema kwamba mwaka huu walitaka kuwa na mbio za timu 20 (ngalawa) walishindwa kuhitimisha ndoto hiyo kutokana na masuala nje ya uwezo wa ZIFF.
Ili kukamilisha vyema mbio hizo kunatakiwa kuwa na boti za kutosha za uokozi kama kutatokea ajali.
Mwaka juzi kulitokea ajali ambayo hata boti ilipofanya uokozi nayo ikazidiwa na kulazimisha watu kukwama mpaka jioni walipopata boti nyingine kutoka Bandarini.
Wakati wa mbio za resi ambazo washindi wa kwanza ni timu iliyokuwa ikiongozwa na Hatibu Suleiman waliokuwa ndani ya ngalawa Ipo Siku, ngoma mbalimbali za asili zilipigwa ufukoni kama hamasa huku watu wakisubiri marejeo ya ngalawa hizo.
DSC_0241
Baadhi ya Ngalawa zinazoshiriki 
mashindano hayo zikianza kukata mawimbi.

Mbio hizo ambazo zilianzishwa na mbunge wa Kiembesamaki na Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF, Mahmoud Thabiti Kombo mshindi wake wa pili alikuwa ni timu ya haji Hassan (kama nadhodha) ndani ya ngalawa Kipanga. Aidha Hassan Simai na wenzake waliokuwa katika ngalawa iliyoitwa peace of Love walikuwa washindi wa tatu.
Timu ya ngalawa ambayo inahitaji ujuzi katika utekaji tanga , kulirekebisha na kubalansi ngalawa inahitaji watu wapatao watano na si chini ya watatu.
Tamasha la filamu linaendelea mjini hapa kwa shughuli mbalimbali zikiwemo za mafunzo ya utunzi, utengenezaji wa filamu na uhakiki wake.
DSC_0262
Pichani juu na chini ni Sehemu ya wakazi wa Zanzibar wakishuhudia mashindano hayo.
DSC_0266 Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo ( wa pili kulia) akiwa meza kuu na mmoja wa wadhamini wa mashindano hayo Mohammed DSC_0299 DSC_0268
Burudani ya Ngoma kutoka Nungwi ikitumbuiza wakati wa mashindano hayo.
DSC_0314
Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akionyesha moja ya zawadi t-shirt kwa watoa burudani waliokuwa wakishindana kucheza ngoma za asili.
DSC_0286
Mkazi wa Nungwi na Stone town (mwenye kaptura) wakishindana kutoa burudani ya ngoma za asili za visiwani humo wakati wa mashindano hayo.
DSC_0325
Mshehereshaji wa tamasha la ZIFF 2014, Muslim Nassor akimuonyesha moja ya zawadi (haipo pichani) mkazi wa Stone town aliyekuwa akisherehesha wakati wa mashindano ya Ngalawa kwenye fukwe za hoteli ya Tembo visiwani Zanzibar.
DSC_0581
Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akikabidhi zawadi kwa mshindi wa tatu nahodha wa resi za Ngalawa iliyopewa jina la " Peace of life" M, Bw. Hassan Simai.
DSC_0586
Mshindi wa tatu nahodha wa resi za Ngalawa, "Peace of life" Bw. Hassan Simai katika picha ya pamoja na mdhamini wa Ngalawa yao iliyopewa jina la " Peace of life" Mkurugenzi mtendaji wa Zanlink, Bw. Sanjay Raja.
DSC_0593
Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akikabidhi zawadi kwa mshindi wa pili nahodha wa resi za Ngalawa iliyopewa jina la "Kipanga" Haji Hassan. Katikati ni mdhamini wa Ngalawa ya Kipanga, Bi. Latifa Mohamed Omar kutoka Zan Air.
DSC_0594
Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF, Mh. Mahmoud Thabit Kombo akikabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza wa nahodha mashindano ya resi za Ngalawa, Bw. Khatib Suleiman katika shamra shamra za tamasha la 17 la ZIFF linaloendelea kutimua vumbi visiwani Zanzibar.
DSC_0598
mshindi wa kwanza wa mashindano ya resi za Ngalawa, Bw. Khatib Suleiman (kushoto) akipongezwa na mdhamini wake mwakilishi wa Com-Net Zanzibar Bw. Mohammed (katikati). Kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya ZIFF, Mh. Mahmoud Thabit Kombo.

photo ,

Bw Harusi ,Joshua Nassari na Bi Harusi Anande Nnko wakapanda usafiri mwingine tofauti na ule waliofika nao katika Hotel ya Ngurdoto na safari hii ni kuelekea uwanja wa User-River kwa ajili ya sherehe.
Msafara ukaanza safari yake kutoka Ngurdoto huku njiani madereva wa Boda boda wakiwa wamezunguka gari la Maharusi na wengine wakionesha mbwembwe.

Baada ya mwendo kido Maasai nao wakaomba msafara wa pikipiki ukae pembeni wakidai ni zamu yao sasa kusindikiza Maharusi.
Huko uwanjani MC ,Masanja Mkandamizaji na Salum Mwalimu walikuwa bize kuweka mambo sawa.
Wageni mbalimbali walikuwepo uwanjani hapo wakingojea Maharausi miongoni mwao ni wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Maharusi ,Joshua Nassari na Anande Nnko wakiwa na wapambe wao katika pozi la kuchukua Taswira.
Taswira katika maeneo mbalimbali ya Ngurdoto Mountain Lodge.


Bi Harusi Anande Nnko akiwa amebebwa na Bwana Harusi pamoja na wapambe wake.
Pozi tofauti za Maharusi.
Maharusi wakiwa katika picha ya pamoja na wazizi wa Bi Harusi Anande Nnko pamoja na ndugu zao.
Maharusi wakiwa na Mzee Edwin Mtei pamoja na Mama Mtei.


Bwana Harusi Joshua Nassari akiwa katika pozi la picha na wazazi wake.


Mbunge wa viti maalum Lucy Owenya pia alihakikisha na yeye anakuwa kwenye kumbukumbu za Picha ,Baada ya picha safari ilikuwa ni ya kuelekea Ukumbini yote utayaona hapa hapa.
 

photo , ,


Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mh Said Mecky Sadick akiongea wakati wa msiba wa Marehemu George Otieno (Tyson) leo kwenye viwanja vya leaders ambapo wakazi wa Jiji la Dar Walijitokeza kwaajili ya Kutoa Heshima zao za Mwisho kwa Marehemu kabla ya kusafirishwa kuelekea Kenya Kwa Mazishi
 Mtoto wa Kwanza wa Marehemu George Otieno (George Tyson) wa kwanza kushoto akiwa na majonzi yakuondokewa na baba yake kipenzi huku Mama yake naye akiwa mwenye huzuni tele na simanzi.
Mwakilishi wa Wanahabari kutoka TV1 ambapo Marehemu alikuwa mfanyakazi katika kituo hiko cha Runinga akiongea machache kabla ya kutoa heshima za mwisho
 Mama Mkwe wa Marehemu George Tyson, Natasha akielekea kuketi upande wa meza kuu. Natasha ni mama mzazi wa Aliyekuwa Mke wa Marehemu George Tyson ajulikanae kama Monalisa
 Mboni Masimba akielekea jukwaa kuu kwaajili ya kuketi
 Mwimbaji wa Nyimbo za injili akiimba wimbo kwaajili ya kuwafariji wafiwa wote katika viwanja vya leaders mapema
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi ambapo Marehemu kwa kusaidia na Mboni Masimba walikwenda kutoa Msaada wa madawati katika shule hiyo Mkoani Dodoma na mauti kumfika wakati wakitoka Mkoani Dodoma
 Wafanyakazi wa TV 1
 Baadhi ya Wafanyakazi wa TMT wakiwa na majonzi
 Mke aliyekuwa akiishi na Marehemu
 Umati wa Waombolezaji
Mwakilishi wa Wasanii Kutoka Morogoro
 Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam akitoa heshima za Mwisho
.Na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

photo , ,