1Waziri Mkuu mstaafu Mh. Fredrick Sumaye akisalimiana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama Baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Sokoine tayari kwa tamasha la Krismas lililofanyika kwenye uwanja wa huo jijini Mbeya , Mh. Fredrick Sumaye amewaasa watanzania kumcha mungu na kuchagua viongozi waadilifu wenye uzalendo wa nchi, wenye kupenda na kuhurumia wananchi masikini na wenye hofu ya mungu ili kulinda amani ya nchi yetu jambo litakalofanya hata maombi yanayofanyika kuombea taifa la Tanzania yapokelewa na Mungu , Tamasha hilo kesho linaendelea mkoani Iringa ambapo wakazi wa mjini Iringa wanapata nafasi nyingine ya kumcha mungu kwa njia ya uimbaji 2Waziri Mkuu mstaafu Mh. Fredrick Sumaye akisalimiana Katibu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT), David Mwasota kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw Alex Msama 3Waziri Mkuu mstaafu Mh. Fredrick Sumaye akizindua albam ya Kwaya ya Umoja wa Kwaya ya makanisa mbalimbali jijini Mbeya yenye inayoitwa Mubhopege Pa Finganilo yenye nyimbo nane kulia ni Katibu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT), David Mwasota na kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw Alex Msama. 4Katibu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT), Askofu David Mwasota akiiombea albam ya Mubhopege Pa Finganilo ya Kwaya ya Umoja wa Kwaya ya makanisa mbalimbali jijini Mbeya huku Waziri Mkuu mstaafu Mh. Fredrick Sumaye,Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw Alex Msama na mmoja wa waratibu wa tamasha la Krismas Bw. John Melele wakishiriki katika maombi hayo. 5Mwimbaji wa muziki wa injili Upendo Nkone akifanya vitu vyake kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya wakati wa tamasha la Krismas leo. 6Mwimbaji Ambwene Mwasongwe naye amesifu na kuabudu pamoja na mashabiki wake kama anavyoonekana akiwa jukwaani. 7Mwimbaji Ambwene Mwasongwe naye amesifu na kuabudu pamoja na mashabiki wake kama anavyoonekana akiwa akitunzwa na mashabiki wake wakati akiimba jukwaani. 10Tumaini Njole na wacheza shoo wake wakiwa angani wakati wakifanya vitu vyao jukwaani. 11Mashabiki walishindwa kukaa chini wakati wote wa tamasha. 14Mwimbaji Joshua Mlelwa akikonga nyoyo za mashabiki wake kwa uchezaji wake jukwaani. 15Mwimbaji Joshua Mlelwa akikonga nyoyo za mashabiki wake kwa uchezaji wake jukwaani. 17Mashabiki wakipata taswira kwa simu zao huku burudani ikiendelea. 18Mwimbaji Emmanuel Mgogo naye amefanya mambo makubwa sana katika tamasha hilo. 20Waziri Mkuu mstaafu Mh. Fredrick Sumaye akizungumza na mashabiki wa muziki wa injili. 21Mwimbaji Joshua Mlelwa akikonga nyoyo za mashabiki wake kwa uchezaji wake na wacheza shoo wake huyu amekuwa pia akifanya maonesho kama haya Ulaya na Marekani .. 22
Edson Mwasabwite kulia ni Faraja Ntaboba kutoka DRC Congo wakionyesha vitu vikubwa kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya. 23Mwimbaji kutoka Kenya Ritha Kisava ambaye ameshiriki Tamasha la Krismas kwa mara ya kwanza akiimba hii ilikuwa kama utabulisho wake kwa mashabiki wa muziki wa Injili nchini Tanzania. 25Waziri Mkuu mstaafu Mh. Fredrick Sumaye akiteta jambo na mmoja wa waratibu wa tamasha la Krismas Bw. John Melele wakati wa tamasha hilo.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MBEYA)

photo , ,


Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Loyce Ruhembe akiwakaribisha Wanahabari ambao wakitembelea gerezani hapo Desemba 19, 2014. Wanahabari hao wapo katika ziara ya kikazi katika miradi mbalimbali ya Uzalishaji mali inayotekelezwa kwa mafanikio makubwa na Jeshi la Magereza(kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Mororogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kato Rugainunula.
Wafungwa wa kike wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro wakifuma mashuka katika Kiwanda cha Ushonaji cha Gereza hilo. Wafungwa hao wanapitiwa ujuzi wa aina mbalimbali ikiwemo Ushonaji wa nguo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Programu za Urekebishaji ndani ya Magereza hapa nchini.
Muonekano wa mashuka na mito yake yanayofumwa na Wafungwa Wanawake katika Kiwanda cha Ushonaji cha Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro.
Wanahabari wakionja chakula cha Wafungwa katika Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro walipotembelea Gereza hilo Desemba 19, 2014(kulia) ni Mwandishi kutoka Gazeti la Habari Leo, Bi. Regina Kumba(kushoto) ni Mwandishi kutoka Gazeti la Daily News, Bw. Finning Simbeye(katikati) ni Mwanahabari kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Bi. Rose Mdami.
Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Loyce Ruhembe akipokea rasmi msaada wa vitu mbalimbali vilivyotolewa na Wanahabari hao kwa ajili ya Wafungwa wa kike gerezani hapo walipotembelea Gereza hilo Desemba 19, 2014.
Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Loyce Ruhembe akikabidhi msaada huo kwa Mfungwa wa Kike ambaye ndiye Nyampara Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro. Wafungwa wa Gereza hilo wamewashukru Wanahabari hao kuwatembelea pamoja na msaada huo walioutoa na wameahidi kuwa raia wema mara wamalizapo vifungo vyao.
Msaada wa vitu mbalimbali vya Kibinadamu na vinavyoruhusiwa Magerezani vilivyokabidhiwa na Wanahabari walipotembelea Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro Desemba 19, 2014.
Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Loyce Ruhembe(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wanahabari walipotembelea Gereza hilo Desemba 19, 2014. Wa tatu kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kato Rugainunula.(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

photo ,

Wafungwa wa Gereza Idete wakilima shamba kwa kutumia trekta kama inavyoonekana katika picha. Wafungwa hao wamepatiwa ujuzi wa kulima na trekta wakiwa gerezani ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Programu mbalimbali za Urekebishaji zinazofanywa na Jeshi la Magereza hapa nchini. Kwa wastani Wafungwa hao hulima hekari 10 kwa siku.
Mkuu wa Gereza Idete, Mkoani Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Beno Hunja akifanya mahojiano Maalum na Waandishi wa Habari(hawapo pichani) walipotembelea Ofsini kwake Desemba 17, 2014 kujionea ujenzi unaoendelea wa mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji. Mradi huo unajengwa kwa kutumia fedha za ndani na utagharimu kiasi cha Bilioni 2.8 hadi kukamilika kwake hivyo kukamilika kwa mradi huo kutalifanya Jeshi la Magereza kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi kuliko hivi sasa.
Mkuu wa Gereza Idete, Beno Hunja akiwaongoza Waandishi wa Habari kutembelea eneo kunakojengwa mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji.
Sehemu ya Mbanio na chanzo Kikuu cha kupokelea maji yatakayotumika katika mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji wa Gereza Idete.
Waandishi wa Habari kutoka Vyombo mbalimbali wakifanya mahojiano na Mkuu wa Gereza Idete(hayupo pichani) walipofanya ziara yao ya kikazi Desemba 17, 2014 kujionea ujenzi wa mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji.
Mfereji ambao tayari umekamilika kujengwa katika mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji wa Gereza Idete, Mkoani Morogoro.(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza)

photo , ,


Kaimu Meneja wa LAPF Kanda ya Mashariki, Isaya Mwakifulefule (kushoto), akimkabidhi, Ofisa Elimu wa Vifaa na Takwimu wa Wilaya ya Kibaha, Doris Semkiwa (kulia), bati na rangi zenye thamani ya sh.milioni 3.5 zilizotolewa na mfuko huo jana, kusaidia ujenzi wa maabara katika Shule ya Sekondari ya Mihande ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Rais Jakaya Kikwete za kuhakikisha kila shule ya sekondari nchini inakuwa na maabara. Anayeshuhudia makabidhiano hayo katikati ni Mkuu wa shule hiyo, Flora Masha.
Kaimu Meneja wa LAPF Kanda ya Mashariki, Isaya Mwakifulefule (kushoto), akipeana mkono na Mkuu wa shule hiyo, Flora Masha wakati akikabidhi msaada huo. Kulia ni   Ofisa Elimu wa Vifaa na Takwimu wa Wilaya ya Kibaha, Doris Semkiwa. 
Kaimu Meneja wa LAPF Kanda ya Mashariki, Isaya Mwakifulefule (kushoto), akipeana mkono na Ofisa Elimu wa Vifaa na Takwimu wa Wilaya ya Kibaha, Doris Semkiwa. Kulia ni Mkuu wa shule hiyo, Flora Masha.   
Hapa ni kubadilishana mawazo baada ya makabidhiano hayo.
Kaimu Meneja wa LAPF Kanda ya Mashariki, Isaya Mwakifulefule (kushoto), akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo.
Jengo la maabara la shule hiyo lililokamilika ujenzi wake.
Jengo la maabara ambalo ujenzi wake unaendelea.
Baadhi ya majengo ya shule hiyo yanvyoonekana.
Jengo la utawala la shule hiyo.
Dotto Mwaibale
MFUKO wa Pensheni wa LAPF umeunga jitihada za Rais Jakaya Kikwete za kuhakikisha kila shule ya sekondari nchini inakuwa na maabara kwa kutoa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya sh.milioni 3.5 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa maabara katika Shule ya Sekondari ya Mihande iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha.
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo Mlandizi wilayani humo jana, Kaimu Meneja wa Kanda ya Mashariki wa mfuko huo, Isaya Mwakifulefule alisema mfuko huo umejiwekea utaratibu wa kusaidia kutoa misaada mbalimbali katika  shughuli za maendeleo ya kijamii.
"Mfuko wetu kila kanda nchini wamekuwa wakishiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo na katika hilo mnaweza kuwa mashuhuda kwani siku za hivi karibuni mmeweza kuona tulivyotoa msaada kwa ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi (albino)" alisema Mwakifulefule.
Alisema ujenzi maabara katika shule hapa nchini ni muhimu sana katika wakati huu wa ulimwengu wa sayansi na teknolojia ambapo wanahitaji wanayansi wengi kwa utaalamu wa aina mbalimbali hasa katika masuala ya utafiti.
Alitaja vifaa vilivyotolewa na mfuko huo kuwa ni mabati na rangi kwa ajili ya kukamilishia ujenzi wa maabara hizo na alitoa mwito kwa wadau wa maendeleo na mifuko mingine kujitokeza kusaidia eneo hilo kwani kuna mahitaji makubwa ya maabara nchini.
Akipokea msaada huo kwa niana ya Mkurugenzi wa Halmshauri hiyo, Ofisa Elimu Vifaa na Takwimu wa wilaya hiyo, Doris Semkiwa alisema msaada huo utapunguza changamoto ya ujenzi wa maabara kwenye shule hiyo.
Alisema ujenzi wa maabara katika wilaya hiyo umekamilika kwa asilimia 67 na kuwa ujenzi huo unaendelea kwa kasi ambapo wanatarajia kukamilisha kazi hiyo mapema iwezekanavyo.
Alisema kwa wilaya nzima yenye shule za sekondari 8 mahitaji ni kuwa na maabara 24 na tayari wamejenga 14 na kuwa fedha zinazotumika kwa ujenzi huo zinatoka katika mapato ya ndani ya Halmshauri, wadau mbalimbali na nguvu za wananchi.
Aliongeza kuwa ujenzi huo utagharimu zaidi ya sh, milioni 400 na kuwa changamoto kubwa ni mapato ya ndani kuwa kiduchu na kuwa kama wangekuwa na fedha za kutosha wangeweza kumaliza kwa wakati ujenzi huo.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Flora Masha aliwashuku LAPF kwa msaada huo pamoja na Halmsahauri kwa fedha za luzuku inazozitoa kila mwezi kusaidia mambo mbalimbali katika shule hiyo na zingine sanjari na ujenzi wa maabara hizo.
"Naishukuru Halmshauri kwa fedha hizo ambazo imekuwa ikitupa kila mwezi kusaidia katika maeneo mbalimbali" alisema Masha.

photo ,


Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu has commended a remarkable initiative by Tanzania National Parks in introducing new tourism products at Lake Manyara National Park. Nyalandu said this during the official launching of the hot springs boardwalk way and hippo pool viewpoint projects at the park yesterday. 
Hon. Nyalandu said that the two projects will add value to the tourism sector by increasing the number of tourist arrivals in the country and urged other stakeholders to be innovative in introducing products that will attract more tourists. 
 The Manyara boardwalk way and hippo pool viewpoint projects worth about 200 millions were initiated to counter the decreased trend of tourist numbers in the park following the flashfloods hit the park in March 2013 which damaged most of tourist infrastructures. 
The first ever tourism product in the national parks, the boardwalk way is featured with 1.5 meters wide impressive wooden structure, creating a 300 meters long trail standing 1.5 meters above ground winding up in an observation platform that is 15 meters long and 2.5 meters wide. 
The trail meanders through the hot springs and lakeshore around a marsh and finally into the lake. 
The boardwalk will give visitors a unique view and wonderful photo opportunities at every turn of the boardwalk trail. 
The Hot springs boardwalk way is designed to simply give people a nice place to walk along the numerous hot springs and be close to the attractions and enjoy the wide view of the lake. 
 Visitors will use the facilities boardwalk way for free and have opportunity of walking around 600 meters on a return trip to the lakeshore and over the hot springs. Educational signage with entertaining themes will be erected in key locations to allow visitors’ easy reading and understanding of the nature and the resources found in the area. 
 These signs will educate visitors about the ecology and adaptation of plants and animals to the area. Moreover, it will explain the fragility of the ecosystem and why it is so important to use the boardwalks to avoid, as much as possible, disturbing the environment. 
Moreover, the viewpoint is a freestanding wooden platform rising by 8 feet above the ground measuring 56 feet in length and 5 feet in width. It is about 8 km away from main gate. 
Standing at the top of the viewing platform enables the viewer a spectacular view of the marshland and its inhabitants – waterfowl, hippo, buffalo and wildebeest – from a point of vantage while affording the visitor a high sense of security. 
 Issued by Corporate Communications Department 
TANZANIA NATIONAL PARKS P.O.BOX 3134 ARUSHA
The newly launched Hippo view point in Lake Manyara National Park
The newly launched Hot springs boardwalk way in Lake Manyara National Park
Some of the TANAPA staff in a group picture with the Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu (seated third left).
Chairman of the Tanzania Association of Tour Operators Mr. Wilbard Chambulo was also there to emphasis the importance of National Parks.
Chief Park Warden for Lake Manyara National Park Mr. Domician Njau explaining about the newly launched projects during the official launching of the hot springs boardwalk way and hippo view point at Lake Manyara National Park yesterday.
Chief Park Warden for Lake Manyara National Park Mr. Domician Njau (right) explain a point to Hon. Lazaro Nyalandu, Minister for Natural Resources and Tourism as they walk through the Lake Manyara Hot springs boardwalk way yesterday.
Director General of TANAPA Allan Kijazi giving out welcoming remarks during the official launching of the hot springs boardwalk way and hippo view point at Lake Manyara National Park yesterday.
Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu (2nd right) cuts a ribbon to officially launch the Lake Manyara hot springs boardwalk way and hippo pool view point in Lake Manyara. Others in the picture from left are Manyara Regional Commissioner Hon. Elaston Mbwilo; Director General of TANAPA Allan Kijazi and the Chairman of the Parliamentary Committee on Lands, Natural Resources and Environment Hon. James Lembeli.
Minister for Natural Resources and Tourism Hon. Lazaro Nyalandu unveils the foundation stone of the Lake Manyara hot springs boardwalk way yesterday.

photo ,