Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa kwanza kulia) kwa pamoja na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museven (wa pili kulia), Rais wa Afrika Kusini, Mhe Jacob Zuma (wa tatu kutoka kulia), Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Mhe. Alain Nyamitwe (wa tatu kushoto) na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Richard Sezibera (wa pili kushoto), wakiimba wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kabla ya kuanza rasmi kwa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kujadili hali ya siasa na usalama nchini Burundi. Mkutano huo ulifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 31 Mei, 2015. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (wa pili kutoka kulia) akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Joyce Mapunjo na  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje (kulia)  nao wakiimba wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Dkt. Richard Sezibera akisoma maazimio yaliyofikiwa mara baada ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kumalizika.
Kundi la Watu Maalum la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalofuatilia hali ya siasa na usalama nchini Burundi chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Jaji Joseph Sinde Warioba  wakifuatilia mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini.
Juu na Chini ni Wajumbe mbalimbali wakifuatilia mkutano wa wakuu wa nchi wa EAC
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya (katikati) akiwa pamoja na Mkurugenzi Msaidizi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Burundi, Bibi Victoria Mwakasege nao wakifuatilia mkutano
Maafisa Mambo ya Nje nao wakifuatilia kwa makini mkutano 
Sehemu ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini nao wakifuatilia mkutano 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari,  Bw. Assah Mwambene (katikati) kwa pamoja na Afisa Habari wa Sekretarieti ya Maziwa Makuu Bw. Macdonald Mwakasendile (kushoto) wakirekodi matukio 
Rais Kikwete akifuraia jambo na Rais wa Afrika Kusini Mhe. Zuma pamoja na Rais wa Uganda Mhe. Museveni mara baada ya kumaliza mkutano.
Rais Kikwete akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Bi.Nkoosazana Dlamini-Zuma kabla ya kuanza mkutano. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe akiongozana na Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta tayari kwenda kuanza mkutano wa kujadili hali ya usalama nchini Burundi .
Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje, Balozi Liberata Mulamula akizungumza jambo na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya,, Bw. Vervaeke.

....Kuwasili kwa viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Mulamula akisalimiana na Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyetta akipita kwenye Gwaride la Heshima mara baada ya kuwasili nchini
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Harrison Mwakyembe akimtambulisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula kwa Rais wa Uganda mara baada ya kumpokea Rais huyo alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Rais Museven akipita katikati ya  Gwaride la heshima. 
Balozi wa Tanzania nchini Afrika ya Kusini Balozi Radhia Msuya akisalimiana na Rais wa Afrika ya Kusini alipowasili nchini
Picha ya Pamoja baada ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.Picha na Reginald Philip

photo , ,


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikaribishwa na Spika wa Bunge la nchi ya Finland Mhe Maria Lohela siku alipotembelea bunge la nchi hiyo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Spika wa Bunge la nchi ya Finland Mhe Maria Lohela siku alipotembelea bunge la nchi hiyo.
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake akikutana na kufanya mazungumzomna Spika wa Bunge la nchi ya Finland Mhe Maria Lohela siku alipotembelea bunge la nchi hiyo.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mahojiano na wanahabari jijini Helsinki, Finland.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mtafiti na mwanasayansi  Mtanzania wa mambo ya mawasiliano na mitandao katika Chuo Kikuu cha Aalto cha Helsinki Dkt Edward Mutafungwa alipotembelea chuoni hapo kujionea shughuli za chuo hicho maarufu nchini Finland
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akigonganisha glasi na Mari Kiviniemi, Waziri wa Masuala ya Nje wa Finland wakati wa dhifa iliyoandaliwa kwa heshima yake jijini Helsinki
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mabalozi wa sasa na wa zamani waliopata kuiwakilisha Finland nchini Tanzania
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watanzania waishio Finland. Wa pili kushoto ni mwalimu wa Rais Kikwete alipokuwa Chuo Kikuu cha Dar  es salaam Profesa MarjaLiisa Swantz, ambaye ni Mfini
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wafanyabiashara wa Finland pamoja na washirika wao wa Tanzania baada ya mkutano wao jijini Helsinki, Finland
Rais Jakaya Kikwete na ujumbe wake wakipata maelezo ya uzaishaji nishati toka kwa viongozi wa kampuni ya Watsila nje kidogo ya jiji la Helsinki
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo alipotembelea kiwanda cha METSO cha  kutengenezea vipuli vya mitambo ya gesi na mafuta katika jiji la Helsinki, Finland.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Watanzania waishio Sweden alipokutana nao Alhamisi jijini Stockholm
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Watanzania waishio Sweden alipokutana nao Alhamisi jijini Stockholm
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Watanzania waishio Sweden alipokutana nao Alhamisi jijini Stockholm
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya mchoro kutoka kwa Msanii wa Kimataifa wa Kitanzania aishiye Sweden Bw. Charles Njau alipomutana na  Watanzania waishio Sweden alipokutana nao Alhamisi jijini Stockholm
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza mtaalamu wa kimataifa wa mambo ya mapishi aishiye Sweden Chef Issa Kipande ambaye mwaka jana alikuwa katika timu ya taifa ya Sweden kwenye mashindano ya kombe la dunia la mapishi walikoibuka na medali ya dhahabu. Chef Issa, ambaye pia anaedeesha hoteli Mtwara, hivi karibuni amefungua mgahawa mkubwa mkubwa kuliko yote wa Ki Afrika katika Ulaya yote mjini Trolhattan, nje kidogo ya jiji la Stockholm, wenye uwezo wa kuchukua watu 400 kwa wakati mmoja
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na viongozi wa jumuiya ya watanzania waishio nchii Sweden jijini Helsinki
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake akilakiwa na Mfalme Carl Gustav wa 16 wa Sweden katika kasri la Mfalme jijini Stockholm, Sweden
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi mkuu wa SIDA Bw. Torbjorn Petterson makao makuu ya shirika hilo la maendeleo la Sweden jijini Stockholm
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wafanyakazi wa SIDA  katika makao makuu ya shirika hilo la maendeleo la Sweden jijini Stockholm
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Spika wa Bunge la Sweden Mhe Urban Ahlin alipotembelea Bunge la nchi hiyo jijini Stockholm
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Spika wa Bunge la Sweden Mhe Urban Ahlin alipotembelea Bunge la nchi hiyo jijini Stockholm
Rais Kikwete akilakiwa na Mfalme Carl Gustav wa XVI  wa Sweden katika kasri la Mfalme jijini Stockholm
Rais Kikwete akilakiwa na Mfalme Carl Gustav wa XVI wa Sweden. PICHA NA IKULU

photo , ,


Katibu Mkuu wa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abduwakil akizungumza na kuwapongeza wajumbe wa Kikao Kazi cha Uandaaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara yake wa mwaka wa fedha 2015/2016 katika kazi hicho kinachoendelea mjini Morogoro.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mwamini Malemi akitoa mwongozo wa majadiliano kwa Wakuu wa Idara, Maafisa Ununuzi, Maafisa Bajeti na Wakurugenzi Wasaidizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi baada ya kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Ununuzi kwa mwaka wa fedha 2014/2015 kutoka kwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi cha wizara hiyo Mapesi Manyama katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara wa mwaka wa fedha 2015/2016 kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro. Kushoto ni Kamishna wa Fedha wa Jeshi la Magereza Gaston Sanga aliyesimama ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mapesi Manyama.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Manyama Mapesi akitoa ufafanuzi wa taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Ununuzi kwa mwaka wa fedha 2014/2015 wa wizara hiyo, aliyoiwasilisha katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara wa mwaka wa fedha 2015/2016 kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro. Wa kwanza kutoka kulia walioketi ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mwamini Malemi katikati ni Kamishna wa Fedha wa Jeshi la Magereza Gaston Sanga akifuatiwa na Kamishna wa Lojistiki na Fedha wa Jeshi la Polisi Clodwig Mtweve.
Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi cha Jeshi la Polisi Asenga akitoa maelezo na kuwapitisha katika Sheria Mpya ya Ununuzi ya mwaka 2011 katika Taasisi za Umma wajumbe wa Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa mwaka wa fedha 2015/2016 wa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Mapitio hayo yamefanyika katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara wa mwaka wa fedha 2015/2016 kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro.
Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Usajili wa Vyama Marlin Komba katika wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya Kisheria kuhusu masuala ya Ununuzi katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wa mwaka 2015/2016 kinachowahusisha Maafisa Bajeti, Maafisa Ununuzi, Wakurugezi, Wakurugenzi Wasaidizi na Wakuu wa Taasisi zote za wizara hiyo kinachoendelea katika hoteli ya Oasisi mjini Morogoro , Wanaomsikiliza ni baadhi ya wajumbe wa kikao hicho kutoka Jeshi la Polisi na Uhamiaji.
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Haji Janabi akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya Kifedha yanayohusu Ununuzi katika Taasisi za Umma katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa mwaka wa fedha 2015/2016 wa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kikao kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro.
Mrakibu Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Fane Kapinga akiwasilisha Mada kuhusu Uandaaji wa Mpango wa Ununuzi wa Mwaka wa Fedha wa 2015/2016 kwa kutumia Majedwali yaliyoainishwa na Wakala wa Ununuzi Serikalini (PPRA) katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wa mwaka 2015/2016 kinachowahusisha Maafisa Bajeti, Maafisa Ununuzi, Wakurugezi, Wakurugenzi Wasaidizi na Wakuu wa Taasisi zote za wizara hiyo kinachoendelea katika hoteli ya Oasisi mjini Morogoro.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lilian Mapfa akifuatilia kwa makini ufafanuzi wa Sheria Mpya ya Ununuzi ya mwaka 2011 katika Taasisi za Umma wakati Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi cha Jeshi la Polisi Mathew Asenga akitoa maelezo na kuwapitisha katika Sheria Mpya ya Ununuzi ya mwaka 2011 katika Taasisi za Umma wajumbe wa Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa mwaka wa fedha 2015/2016 wa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro.
Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Makame wa kwanza kutoka kulia akifuatiwa na Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji TRITA mjini Moshi John Choma na watatu kutoka kulia ni Kamishna wa Utawala na Fedha wa Idara ya Uhamiaji Piniel Mgonja wakimsikiliza kwa Makini Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Manyama Mapesi wakati akitoa ufafanuzi wa taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Ununuzi kwa mwaka wa fedha 2014/2015 wa wizara hiyo, aliyoiwasilisha katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara wa mwaka wa fedha 2015/2016 kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro.

photo , ,