Showing posts with label Majanga. Show all posts
Showing posts with label Majanga. Show all posts

Rais Kikwete akimjulia hali mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, Said Mohamed Saad.
 
HABARI KAMILI
Said ambaye ndiye mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, yenye maduka mengi makubwa ya vitu vya nyumbani ndani ya Dar es Salaam na mikoa kadhaa ya Tanzania, anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini lakini mmoja wa watu waliomshuhudia, amefafanua jinsi hali ilivyo mbaya.
“Ameungua sana, tunatarajia kati ya kesho au keshokutwa (wikiendi iliyopita) atafanyiwa oparesheni ya jicho. Jamani tindikali ni mbaya sana, usimmwagie mwenzako. Ndugu yetu ameharibika sana,” kilisema chanzo chetu kwa ombi la kutotajwa jina gazetini, kikaongeza:
“Kila anayemjua vizuri, anapomwona anamwaga machozi. Picha za jinsi alivyoathirika baada ya kumwagiwa tindikali zimevuja mpaka kwa familia, ni kilio kwa ndugu. Wanawake wanalia zaidi.”

JK ATINGA HOSPITALI
Wiki iliyopita, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, alikuwa kwenye ziara ya kikazi nchini Afrika Kusini alipokwenda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini ya Afrika (SADC).
Mkutano huo ni wa Pande Tatu za SADC (Troika of SADC) na akiwa huko, alipata fursa ya kwenda kumjulia hali katika hospitali aliyolazwa ambayo haijajulikana jina.
Chazo chetu kilisema: “Rais Kikwete alisikitika sana. Wakati anatoka wodini alisonya. Alionesha jinsi alivyosikitishwa na unyama aliotendewa Said.”


photo

Taarifa ambazo zimepatikana kwenye mitandao ya Ki-jamii zinaelezwa kuwa, jana usiku katika kata ya Minepa jimbo la Ulanga Magharibi, vijana waliosadikiwa kuwa wa “green guard” waliwavamia viongozi wa CHADEMA na kuwajeruhi...

Waliojeruhiwa ni Mwenyekiti wa Jimbo bw. Kibam Ally Mohammed (aliyevaa shati ya michirizi), Katibu wa Jimbo bw. Lucas Lihambalimo (aliyevaa shati jekundu) na Bw. Severin Matanila, Katibu Mwenezi tawi la Minepa (aliyekaa, mwenye bandeji), ndiye mlinzi wa mgombea.

photo

KIPANDE CHA VIDEO KIKIOYESHA NAMNA MLIPUKO ULIVYOTOKEA
Kutoka kushoto mwenye Fulana Nyekundu ameumia vibaya sana, mtu wa pili kwake ni mwanadada Judy ambaye alipoteza maisha palepale. aliyeshika laptop ni mwana jamii forum
.

Baadhi ya Watoto waliokaa hapo juu ndiyo waliokufa na baadhi kuumia vibaya kwa bomu, hapo ndipo bomu lilipo angukia..

photo