Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiwa na Rais mpya wa Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika wakiwa katika picha ya pamoja baada ya rais mpya wa Malawi kukabidhiwa madaraka leo jijini Brantyre kwenye hoteli Sunbird. Baada ya kukutana viongozi hao walipata fursa ya kuzungumzia masuala la kidiplomasia baina ya nchi hizi mbili na kukubaliana kuendelea kuwa na mahusiano mema kama nchi zinazoishi ndugu na jirani. Picha kwa Hisani ya Ikulu ya Malawi
***************************************
MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI SHEREHE ZA MAKABIDHIANO YA URAIS NCHINI MALAWI
Makamu  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DkT. Mohammed Gharib Bilal, Jumatatu Juni 02, 2014 ameshiriki katika sherehe za kukabidhi madaraka kwa Rais mpya wa Malawi Profesa Arthur Peter Mutharika katika sherehe zilizofanyika kwenye uwanja wa Kamuzu Banda jijini Blantyre. Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Rais wa Botswana sambamba na wawakilishi wa nchi za Zimbabwe, Msumbiji, Afrika Kusini na nyinginezo.
Akihutubia baada ya kukabidhiwa sime ambayo ni ishara ya kuwa kiongozi wa watu wa Malawi, Rais Mteule Mutharika alisisitiza kuwa, katika kipindi cha utawala wake atahakikisha kuwa anaifanyia makubwa Malawi sambamba na uhakikisha kuwa anaifanya Malawi itimize majukumu yake ya kimataifa kufuatia kutambua kuwa kujitenga kunaweza kuifanya Malawi kutonufaika na fursa zilizopo duniani.
“Nchi hii ipo katika dunia na siyo rahisi tena kuwa na fikra kwamba Malawi inaweza kubaki peke yake kama kisiwa. Tunahitaji kuwa na wenzetu wa kusaidia maendeleo ya Malawi. Tunawahitaji wahisani toka Kusini ama Mashariki, tunayahitaji mataifa tajiri na mataifa yanayoendelea. Tutafanikiwa sana kama tutaendeleza urafiki kwa wote. Tufanye hivi bila kujali kuwa sisi ni taifa kwani hali ya sasa inahitaji kila mmoja wetu kushirikiana na mwenzake,” alisema.
Katika hotuba hiyo pia amesisitiza kuwa kipindi chake cha utawala atajitahidi kukabiliana na rushwa na kwamba hatakuwa na mchezo kwa wala rushwa katika kipindi akiwa madarakani. Pia alisisitiza kuhusu umuhimu wa kuiunganisha Malawi kwa miundombinu bora ili kuboresha maisha ya wananchi sambamba na kusogeza huduma za wananchi karibu.
Rais Mutharika aliapishwa juzi baada ya kuwashinda washindani wake akiwemo Rais aliyemaliza kipindi chake Joyce Banda ambaye hata hivyo hakuweza kutokea katika sherehe hizi za kukabidhi madaraka. Akizungumzia suala la kutohudhuria kwa Rais Banda, Rais Mteule Mutharika alisema alitegemea Rais Banda kuwepo lakini hakufika nay eye anatambua kuwa wakati wa uchaguzi kulikuwa na tofauti baina yao lakini kwa sasa uchaguzi umeisha na amesahau yaliyopita ili kuanza ukurasa mpya wa kuijenga Malawi. Katika shughuli hiyo pia Rais wa zamani wa Malawi Kamuzu Banda alihudhuria.
Makamu wa Rais Dkt. Bilal na msafara wake walitarajiwa kurejea nyumbani, hii Jumatatu mara tu baada ya kukamilika kwa kazi hii ya makabidhiano.
 Imetolewa na: Ofisi ya Makamu wa Rais
Juni 02, 2014 Blantyre, Malawi

photo ,

DSC_0024
IN Action; Ms.Usia Nkhoma Ledama from UNIC take part in inviting various guests.
By Damas Makangale, MOblog Tanzania
The Tanzanian government has reassured the United Nations (UN) that it will not hesitate to contribute more peacekeepers to UN Peacekeeping operations.
Tanzania already contributes 2,259 peacekeepers in Darfur, Lebanon, Abyei, South Sudan and Democratic Republic Congo (DRC) for peacekeeping missions but has promised a larger commitment.
Speaking today during the commemoration of the International Day of UN Peacekeepers at Mnazi Mmoja Grounds, Dar es Salaam; Minister for Defense and National Service, Dr Hussein Mwinyi stated that the government is ready and willing to continue serving in their noble duty.
“The success of the peacekeepers can be seen in various places such as the DRC, where the Intervention Brigade (FIB) (a joint effort by the UN and African counterparts) helped the government to defeat the M23 rebels. This is a major positive step in bringing back stabilization and security in the Eastern DRC,”
DSC_0034
Tanzania People's Defense Forces Brass Band enters the Mnazi Mmoja Heroes Grounds.
“As you are all aware, the theme for this year is “UN Peacekeeping: a force for peace, a force for change, a force for the future,” he said.
Dr Mwinyi added that the UN peacekeeping is tackling new challenges to protect citizens as well as ensure peace for tomorrow’s future.
He clarified that new technologies such as unarmed, unmanned aerial vehicles are being deployed to face such challenges.
Dr Mwinyi emphasised that stronger cooperation between the UN and other regional organizations will contribute to the success of the peacekeeping missions and he praised its special role on the peace and security agenda.
DSC_0048
Tanzania People's Defense Forces in action during the commemoration of International Day of UN Peacekeepers.
Acting UN Resident Coordinator and UNICEF Representative, Dr Jama Gulaid said that today, more than 116,000 UN personnel from more than 120 countries serve in 16 peacekeeping operations.
“At great personal risk, these military, police and civilian personnel help stabilize communities, protect civilians, promote the rule of law and advance human rights…last year 106 peacekeepers perished carrying out their duty under the UN flag bringing the total number of lives lost in the history of peacekeeping to more than 3,200,” he said.
He went on to say that the UN peacekeeping is modernizing to ensure that it can tackle tomorrow’s peace and security challenges in order to foster peace and tranquility around the world.
DSC_0092
Guest of Honour Minister of Defense and National Service, Hon. Dr. Hussein Mwinyi listen attentively to the National Anthem from members of Tanzania People's Defense Forces during the ceremony.
DSC_0097
Tanzania People's Defense Forces in action.
DSC_0105
A soldier from TPDF raising UN Flag to mark the International Day of UN Peacekeepers.
DSC_0115
High table stands in a one minute silence to remember UN Peacekeepers who lost their life on Peacekeeping operations.
DSC_0124
TPDF Soldiers in action.
DSC_0153
Guest of Honour Minister of Defense and National Service, Hon. Dr. Hussein Mwinyi, walk to lay a wreath on Mnazi Mmoja Heroes Grounds tower.
DSC_0155
Hon. Dr. Hussein Mwinyi lays a wreath.
DSC_0158
Major General Officer Commanding, Hassan Vuai Chema, lays a wreath at Mnazi Mmoja Heroes Grounds tower.
DSC_0159
Major General Officer Commanding, Hassan Vuai Chema pays respect.
DSC_0161
Acting Resident Coordinator and Country Representantive of the United Nations Children's Fund in Tanzania (UNICEF) Hon. Dr. Jama Gulaid walks to lay the Wreath during the International Day of UN Peacekeepers at Mnazi Mmoja Heroes Grounds today.
DSC_0167
Hon. Dr. Jama Gulaid lays a wreath.
DSC_0168
Hon. Dr. Jama Gulaid paying his respect.
DSC_0174
The Tanzania People's Defense Forces Representantive (TPDF), The Dean of all Defense Attache's in Tanzania, Brigadier General Edumund Obi lays a wreath at Mnazi Mmoja Heroes Grounds to commemorate the soldiers who lost their life during Peacekeeping operations.
DSC_0207
High Table: from Left is Chief of Special Operations and Deputy Commissioner of Police, DCP Simon Sirro, Acting Resident Coordinator and Country Representantive of the United Nations Children's Fund in Tanzania (UNICEF) Hon. Dr. Jama Gulaid, Guest of Honour Minister of Defense and National Service, Hon. Dr. Hussein Mwinyi, Major General Officer Commanding, Hassan Vuai Chema and The Tanzania People's Defense Forces Representantive (TPDF), The Dean of all Defense Attache's in Tanzania, Brigadier General Edumund Obi.
DSC_0183
Some of the Tanzanian Peacekeepers who attended the ceremony today at Mnazi Mmoja Heroes Grounds.
DSC_0190
Some of the students from Azania Secondary School were among of the invitees.
DSC_0208
A group of High Commissioners and Ambassadors and other invitees who attended the commemoration.
DSC_0213
Officials from the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation and UN.
DSC_0232
Singers from UN Peacekeeping mission Entertaining invited guests.
DSC_0297
Guest of Honour Minister of Defense and National Service, Hon. Dr. Hussein Mwinyi gives an opening remarks and the commitment made by the government of Tanzania through UN Peacekeeping missions.
DSC_0264
Acting Resident Coordinator and Country Representantive of the United Nations Children’s Fund in Tanzania (UNICEF) Hon. Dr. Jama Gulaid, speaks during the commemoration of the International Day of UN Peacekeepers.
(All Photo by Zainul Mzige of modewjiblog)

photo ,


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwasilisha Bungeni  Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka wa fedha 2014/2015 mjini Dodoma tarehe 27 Mei 2014
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (wa tatu kutoka kushoto) akiwa na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha (wa kwanza kulia) pamoja na Mke wa Waziri, Mama Dorcas Membe na Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia, Balozi Mohammed Maundi wakifuatilia kwa makini Hotuba ilikuwa ikitolewa na Mhe. Membe (hayupo pichani) Bungeni.
Katibu Mtendajii wa Jumuiya ya Maedneleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika, Dkt. Stergomena Tax (katikati) akiwa na wageni wengine wakifutilia Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka 2014/2015
Baadhi ya Wawakilishi kutoka Balozi za nchi mbalimbali zilizopo hapa nchini wakifuatilia Hotuba ya Mhe. Membe (hayupo pichani)
Baadhi ya Wanafunzi kutoka Vyuo Vikuu vya Mzumbe, SAUT, UDSM, UDOM na CFR wanaochukua Kozi za Uhusiano wa Kimataifa wakifuatilia hotuba ya Mhe. Membe.
Baadhi ya Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia hotuba ya Mhe. Membe

Watendaji  kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia hotuba.
Watendaji wengine kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia Hotuba ya Mhe. Membe.
Wajumbe wakimsikiliza Mhe. Membe
Mwakilishi kutoka Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Betty Machangu (Mb.) akiwasilisha Hotuba kwa niaba ya Kamati hiyo
Mhe. Membe (kushoto) akiwa na Naibu wake Mhe. Dkt. Mahadhii Juma Maalim (Mb.) wakifuatilia hotuba wakati Mhe. Machangu (hayupo pichani) akiwasilisha
Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje kutoka Kambi ya Upinzani, Mhe. Ezekiel Wenje nae akiwasilisha hotuba ya kambi yake.
Mhe. Membe akiongozana na Mhe. Wenje kutoka Bungeni mara baada ya kipindi cha mchana kumalizika.
Mhe. Membe, Mama Dorcas Membe (wa nne kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na Dkt. Tax  wakiwa nje ya Viwanja vya Bunge mara baada ya kipindi cha mchana kumalizika

photo ,

DSC_0073
MO akisalimiana na wazee wa kijiji cha Uhamaka kabla ya kuanza kuzungumza na wananchi.
DSC_0094
MO akisalimiana na mmoja wa watoto waliofika kwenye mkutano wake Uhamaka.
DSC_0086
Mbunge MO akilakiwa na mmoja wa bibi kizee aliyefika kwenye mkutano wake , Karibu mjukuu wangu hapa Uhamaka.
DSC_0107
Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji (MO), akiweka saini kwenye kitabu cha ofisi ya kijiji cha Uhamaka Manispaa ya Singida wakati akiwa kwenye ziara ya kiazi ya siku moja kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo katika jimbo hilo, kulia ni diwani wa kata hiyo na Shaban Kiranga. Kushoto ni mjumbe wa NEC Manispaa ya Singida, Hassan Mazala.
DSC_0184
Diwani wa Kata ya Uhamaka CCM, Kiranga akimkaribisha Mbunge MO, Katani kwake kujionea ujenzi wa vyumba vya madarasa mawili sekondari ya Kata hiyo.
DSC_0198
Afisa Mtendaji wa Kata ya Uhamaka akisoma taarifa ya ujenzi huo.
DSC_0220
Mbunge Dewji akizungumza na wananchi wa kijiji cha Uhamaka wakati wa mkutano wake wa kutembelea jimbo hilo.
DSC_0111
Sehemu ya umati wa Kinamama na watoto wa kijiji cha Uhamaka Manispaa ya Singida wakimsikiliza Mbunge wao.
DSC_0119
Kikundi cha Ngoma na Kwaya ya kijiji cha Uhamaka wakiimba wimbo wa kumkaribisha Mbunge wao Mohammmed Dewji (MO).
DSC_0243
Mjumbe wa NEC Manispaa ya Singida, Hasan Mazala akizungumza kwenye mkutano huo.
DSC_0177
Vijana nao walihudhuria mkutano wa Mbunge wao MO katika kijiji cha Uhamaka.
DSC_0278
: MO akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa ya sekondari ya Uhamaka.
DSC_0274
DSC_0287
Sheikh wa msikiti wa kijiji cha Ititi akimkaribisha MO.
DSC_0294
Sehemu ya Msikiti wa kijiji cha Ititi ambapo MO aliguswa na kuwachangia mifuko 30 ya Saruji na Mabati 30 kwa ajili ya kuedeleza ujenzi wao.
DSC_0344
MO akishiriki kucheza ngoma ya Kinyaturu.
DSC_0380
Viongozi wa kijiji cha Uhamaka wakiwa ofisini kwao na Mbunge MO .
DSC_0387
Afisa Mtendaji wa kijiji cha Ititi, Jumanne Ivanga akisoma taarifa ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Ititi kwa Mbunge MO.
DSC_0404
MO akihutubia wananchi wa kijiji cha Ititi, pia aliahidi kutoa mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa zahanati hiyo.
DSC_0425
“ Kwa hiyo mimi kama Mbunge wenu nitatoa mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huu sawa jamani.” Alisisitiza MO huku akishangiliwa na wananchi hao.
DSC_0449
DSC_0433
Kinamama wa kijiji cha Uhamaka wakimshangilia Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji (MO) wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa Zahanati ya Kijiji hicho jana.
DSC_0454
Sehemu ya viongozi wa dini na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Ititi wakimsikiliza mbunge wao.
DSC_0468
Jamani mmeona utekelezaji wa ilani ya CCM..??? Ni maneno ya MNEC Manispaa ya Singida, Hassan Mazala akizungumza na wakazi wa kijiji cha Ititi.
DSC_0473
Mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM Manispaa ya Singida, Hassan Mazala akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo.
DSC_0488
Mh. Mohammed Dewji akimsikiliza MNEC Hassan Mazala.
DSC_0522
Afisa Mtendaji wa kijiji cha Ititi Jumanne Ivanga akimwonyesha Mbunge Mh. Mohammed Dewji sehemu ambapo Zahanati hiyo itajengwa.
DSC_0526
Muonekano wa sehemu ya Zahanati ya Kijiji cha Ititi itakapojengwa.
DSC_0537
Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji (MO), akisalimiana na viongozi wa kijiji cha Unyianga mara baada ya kuwasili kwenye hafla fupi ya kukagua mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kijiji wakati wa ziara jimbo kwake.
DSC_0557
MO akicheza na baadhi ya wanakikundi wa uhamasishaji kwenye hafla hiyo.
DSC_0565
MO akisikiliza mashairi kutoka kwa kijana Masoud Mkari mara baada ya kuwasili kwenye hafla fupi ya kukagua mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kijiji wakati wa ziara jimbo kwake.
DSC_0581
Afisa Mtendaji wa kijiji cha Unyianga, Ramadhani Mpondo akisoma taarifa fupi ya mradi wa ujenzi wa Sekondari ya kijiji hicho mbele ya Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini.
DSC_0607
Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji (MO), akizungumza na wapiga kura wake kuhusu mchango wake katika ujenzi wa shule hiyo inayojengwa kwa nguvu za wanakijiji pamoja na mfuko wa jimbo la Singida Mjini ambapo ameahidi mifuko 100 ya Saruji pamoja na Mabati 100.
Ujenzi wa mradi wa Sekondari ya Kijiji cha Unyianga ulibuniwa na Halmashauri ya kijiji na kuafikiwa na wananchi kwenye mkutano mkuu wa kijiji baada ya kubaini changamoto nyingi zinazohusu wanafunzi wanaoendelea na masomo sekondari ya kata ya Mwankoko ikiwa ni umbali uliopo kati ya Unyianga na Mwankoko takribani Kilometa 18 kwenda na kurudi, hali inayowalazimu wanafunzi kutembea umbali mrefu na hivyo kuchoka na kushindwa kufanya vizuri kwenye masomo.
DSC_0586
Baadhi ya wanakijiji wa Unyianga wakimsikiliza Mbunge wao Mh. Mohammed Dewji.
DSC_0589
DSC_0622
MNEC wa Manispaa ya Singida, Hassan Mazala akiwahamisha wananchi kushiriki kuchangia shughuli za maendeleo.
DSC_0653
Mh. Mohammed Dewji akipata picha ya pamoja na wapiga kura wake.
DSC_0656
Mh. Mohammed Dewji akikagua mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kijiji wakati wa ziara ya jimboni kwake.
20140523_181746
Mh. Mohammed Dewji, akifurahi na watoto walipomwambia wanampenda sana wangetamani kuwa kama yeye.

photo ,