Dr Ellen Otaru Okoedion Private Sector Development Programme 2013 Team leader from Tanzania, takes participants through a new website- www.fanyabiasharatanzania.com- launch in Dar es Salaam to help local entrepreneurs formalize and grow their businesses. 
 Dr Ellen Otaru Okoedion Private Sector Development Programme 2013 Team leader from Tanzania, introducing her teammates who also participated in the launch of a new website-www.fanyabiasharatanzania.com- to help local entrepreneurs formalize and grow their businesses. The ceremony was held in Dar es Salaam at the weekend. 
 Malena Rosman, Head of Development Cooperation Division in the embassy of Sweden (holding a flower boutique and wearing a red jacket) in a group photo with Private Sector Development (PSD) Programme 2013 Team shortly after their graduation and launch of a website to  help local entrepreneurs formalize and grow their businesses. Far left is Julia Norinder and far right is Daniel Stendahl PSD Programme Tutors.
 Daniel Stendahl (right) Private Sector Development (PSD) Programme Tutor says a word of thanks after being awarded by the 2013 PSD team who graduated in Dar es Salaam at the weekend and launched a new website- www.fanyabiasharatanzania.com- to help local entrepreneurs formalize and grow their businesses. Left is Julia Norinder also a PSD programme tutor.
 Julia Norinder (second left) and Daniel Stendahl, Private Sector Development (PSD) Programme Tutors being awarded by the 2013 PSD team who graduated in Dar es Salaam at the weekend and launched a new website- www.fanyabiasharatanzania.com- to help local entrepreneurs formalize and grow their businesses. 

Julia Norinder (second left) and Daniel Stendahl, Private Sector Development  (PSD) Programme Tutors being awarded by the 2013 PSD team who graduated in Dar es Salaam at the weekend and launched a new website- www.fanyabiasharatanzania.com- to help local entrepreneurs formalize and grow their businesses. 

 Private Sector Development (PSD) Programme Country focal point, Emmanuel Nnko shows one of his gifts he received from Tanzania 2013 Private Sector Development team.
 Private Sector Development (PSD) Programme Country focal points, Saada Mufuruki (left) and Emmanuel Nnko (second right) being awarded by the 2013 Private Sector Development team. Kwa picha zaidi Bofya hapa >>>>

photo ,

Mwaka 2009, wazo jipya lilizaliwa. Wazo la kuwa na tuzo zitakazopatikana kwa mchakato wa wazi utakaotokana na mapendekezo ya watu wenyewe ya kuchagua mastaa wa michezo, muziki, filamu au vipindi na watangazaji wanaopendwa zaidi. Wazo hilo liliendelea kuboreshwa na mwaka huu (2014), limeiva na liko tayari kutoka kwenye hatua ya wazo la kichwani, na kuwa tukio lenyewe.

"Nilizisajili na kuanzisha mwaka 2009 ila kutokana na mipango na malengo ya kampuni niliamua kuziweka kwanza hadi sasa," anasema Mwenyekiti wa Bongo5 Media Group, Luca Neghesti.

"Sasa hivi tumeshuhudia ukuaji katika tasnia mbalimbali na tumeona ni wakati muafaka wa kuwatunuku wale wanaopendwa na wananchi, kuwapatia tuzo pamoja na zawadi ya fedha taslimu milioni 1" ameongeza.

Tofauti na tuzo zingine, tuzo za watu hazitafuti ubora bali zinalenga wanaopendwa zaidi na tuzo hizi hazitajikita katika tasnia moja peke yake.

Kwa kuanzia, tuzo hizi zitatolewa katika tasnia ya burudani inayojumuisha filamu na muziki. Pia zitaiangazia sekta ya utangazaji kwa kuwatunuku watangazaji na vipindi vinavyopendwa zaidi na watu nchini huku pia mwanamichezo bora (soka, basketball, ndondi na michezo mingine) naye akipewa nafasi.

Tuzo za watu si tuzo za vijana peke yake, zipo kuwakilisha watu wa rika zote.

Tofauti nyingine kubwa ni kuwa tuzo za watu zitalenga kuwatunuku watu kutokana na umaarufu ama kupendwa kwao na si ubora. "Tuzo hizi hazileti ushindani na tuzo zingine kwasababu hazilengi tasnia moja tu," anafafanua Neghesti.

"Tanzania imesifiwa kwa uhuru wa vyombo vya habari na tuzo hizi zinalenga kujumuika na tuzo zingine kuhakikisha watanzania wanaopendwa na kufanya vizuri wanatambuliwa."

Upigaji kura unaanza wiki hii katika vipengele 11 ambapo wananchi wenyewe watachagua majina ya washiriki watakaoshindana kwenye vipengele hivyo. Awamu ya kwanza ya upigaji kura itafungwa baada ya wiki mbili kutoka siku ya kwanza ya upigaji kura na majina ya watu watano waliotajwa zaidi kutoka kwenye kila kipengele watachaguliwa kama watajwa wa mwisho.

Kuanzia hapo, upigaji kura wa wananchi utajikita tu katika orodha ya majina hayo matano kwenye kila kipengele kinachoshindaniwa. Wiki moja baada ya majina ya washiriki kutangazwa, mchujo wa kwanza utafanyika katika kila kipengele na mtu mmoja ataondolewa.

Wiki moja baadaye, mchujo wa pili utafanyika na kuwabakiza washiriki watatu kwenye ila kipengele.

Washiriki wote 33 (watatu katika kila kipengele) waliosalia baada ya kufanyika mchujo wa mwisho, watakuwa wageni wa heshima kwenye utoaji wa tuzo hizo, utakaofanyika wiki moja baada ya mchujo huo wa mwisho.

Katika hafla hiyo, washindi watatangazwa na kila mshindi atapokea zawadi ya fedha taslimu, shilingi 1,000,000 za Kitanzania pamoja na tuzo ya thamani iliyotengenezwa kwa mkono kutoka kwenye mali ghafi asili za Kitanzania.

Tuzo za watu mwaka 2014 zitajumuisha vipengele 11 ambavyo ni pamoja na:

1. MTANGAZAJI WA REDIO ANAYEPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW1 na jina' kwenda 15678)
2. KIPINDI CHA REDIO KINACHOPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW2 na jina' kwenda 15678)
3. MTANGAZAJI WA TV ANAYEPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW3 na jina' kwenda 15678)
4. KIPINDI CHA TV KINACHOPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW4 na jina' kwenda 15678)
5. MWANAMICHEZO ANAYEPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW5 na jina' kwenda 15678)
6. MWANAMUZIKI WA KIUME ANAYEPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW6 na jina' kwenda 15678)
7. MWANAMUZIKI WA KIKE ANAYEPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW7 na jina' kwenda 15678)
8. WIMBO UNAOPENDWA (2013) (tuma SMS yenye 'TZW8 na jina' kwenda 15678)
9. MUIGIZAJI WA FILAMU WA KIUME ANAYEPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW9 na jina' kwenda 15678)
10. MUIGIZAJI WA FILAMU WA KIKE ANAYEPENDWA (tuma SMS yenye 'TZW10 na jina' kwenda 15678)
11. FILAMU INAYOPENDWA (2013) (tuma SMS yenye 'TZW11 na jina' kwenda 15678) JINSI YA YA KUPIGA KURA

Mchakato wa kupendekeza majina ya washiriki katika tuzo hizi utafanyika kwa njia kuu mbili. Ya kwanza ni kwa kutumia tovuti ya tuzo hizi ambayo ni www.tuzozetu.com ambapo utakutana na hatua rahisi ya kupendekeza na kutaja majina katika vipengele vyote 11. Jinsi ya kupiga kura, bofya palipoandikwa Piga Kura na ufuate hatua rahisi kabisa ambayo haikuhitaji kujiandikisha jina wala email yako.

Njia ya pili ni kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu ambapo utaandika neno ‘Tuzo’ kwenda namba 15678. Ukishafanya hivyo utaletewa Menu yenye vipengele vyote 11 vikiwa na code number zake. Kutaja ama kupendekeza jina, tuma code husika na jina kwenye namba hiyo hiyo; kwa mfano Justin Bieber. Gharama ya sms ni ile ile inayotozwa sms ya kawaida.

photo ,

 Mwenyekiti wa Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,Mh. George Kahama (liesimama) akitoa muongozo wa namna vikao vitakavyokuwa vinaendelea kufanyika katika kumbi mbali mbali ndani ya Hoteli ya Malaika,iliwa ni muendelezo wa Kongamano Uwekezaji Kanda ya Ziwa,unaoendelea kufanyika kwenye Hoteli ya Malaika,Jijini Mwanza.Wengine pichani toka kushoto ni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Titus Kamani,Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye ndie Mwenyeji wa Kongamano hilo,Mh. Everist Ndikilo,Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Mh. Charles Kitwanga pamoja na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mh. Christopha Chiza.
Mwenyekiti wa Kikao kinachojadili maswala ya Ufugaji katika Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Titus Kamani (katikati) akizungumza na Wajumbe wa Kikao hicho (hawapo pichani) wakati akitoa muongozo wa kikao hicho kinachoendelea kufanyika hivi sasa katika Ukumbu wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika,jijini Mwanza.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mh. Said Magalula na Kulia ni Meneja wa Kituo cha Uwekezaji Kanda ya Ziwa,Bw. Fanuel Lukwaro
Mtoa Mada iliyohusu Fursa za Uwekezaji katika Ufugaji na Michakato ya kuwa na Machinjio bora,Prof. Lazaro Kurwijila kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine (Idara ya Sayansi ya Wanyama) akisisitija jambo wakati akiwasilisha mada yake hiyo,kwenye Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,linaloendelea kufanyika hivi sasa kwenye Ukumbu wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika,jijini Mwanza.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye ndie Mwenyeji wa Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,Mh. Everist Ndikilo akifatilia kwa makini kikao hicho kinachoendelea kufanyika hivi sasa katika Ukumbu wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika,jijini Mwanza.
Wajumbe wakifatilia kikao hicho.
Mwenyekiti wa Kikao kinachojadili maswala ya Kilimo katika Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mh. Christopha Chiza (kulia) akizungumza na Wajumbe wa Kikao hicho (hawapo pichani) wakati akitoa muongozo wa kikao hicho kinachoendelea kufanyika hivi sasa katika Ukumbu wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika,jijini Mwanza.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Shinganga,Mh. Yohana Balele.
Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),Mh. Aggrey Mwanri (wa pili kulia) akiwa pamoja na Wajumbe wengine kufatilia moja ya vikao vinavyoendelea kwenye Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,linaloendelea kufanyika hivi sasa kwenye Ukumbu wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika,jijini Mwanza.
Wajumbe wakipitia makabrasha mbali mbali ya Kongamano hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii nchini (TTB) Dkt. Aloyce Nzuki (kushoto) akizungumza wakati akiwasilisha mada yake iliyohusu uwepo wa Fursa za Uwekezaji katika Uwindaji na Hoteli wakati wa Kikao kilichokuwa kikijadili maswala ya Miundombinu ya kijamii ikiwa ni pamoja na Elimu na Afya katika Kongamano la Uwekezaji Kanda ya Ziwa,linaloendelea kufanyika hivi sasa kwenye Ukumbu wa Mikutano wa Hoteli ya Malaika,jijini Mwanza.Picha na Othman Michuzi,Mwanza.

photo ,

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza  na viongozi wa  Jumuiya  za Wafanyabiashara wa kati wa Kariakooo na Mikoani kuhusu mgogoro wa matumizi  ya mashine za TRA, Ofisini kwake jijini Dar es salaam Feb 12, 2014- usiku.Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha, Adam Malima. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Baadhi ya viongozi wa Jumuiya za wafanyabiashara wa kati wa Kariakoo na Mkoani  wakimsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipozungumza nao kuhusu mgogoro wa matumizi  ya mashine  za TRA, Ofisini kwake jijini Dar es salaam Februari 12, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akizungumza na viongozi wa  wa Kampuni ya China ya  AVIC Group China  Civil Aviation inayopkusudia kuwekeza katika kampuni ya  Ndgege ya ATCL, Ofisini kwake jijini Dar es salaam, Februari 13, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

photo ,



photo

Mkemia kutoka ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Bi. Lulu Kiwia akitoa ufafanuzi kuhusu Kadi ya Usalama wa Kemikali (Material Safety Data Sheet-MSDS) wakati wa mafunzo
 Washiriki wa mafunzo wakiwa kwenye majadiliano
 Washiriki wa mafunzo wakiwa kwenye majadiliano
Mshiriki wa mafunzo akiwasilisha baada ya majadiliano ya vikundi wakati wa mafunzo
Wataalam wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali wakiwajibika wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari na taasisi zisizo za kiserikali
Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Ubora wa Bidhaa ndugu Daniel Matata akitoa mada wakati wa Mafunzo
Mkemia wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ndugu Fidelis Segumba akitoa ufafanuzi akielezea sheria DNA na Kanuni zake

photo

k
Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali ndugu Sabanitho Mtega amewaasa waandishi wa Habari kutumia Taasisi na Wataalam wa ofisi ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali katika kupata majibu sahihi yanayotokana na Uchunguzi unaofanywa na taasisi hiyo ili kuisadia jamii kupata majibu na taarifa iliyo sahihi kutoka kwenye ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali amesema kuwa ili waandishi wa habari waweze kuandika habari za uhakika ipo haja ya wanahabari hao kushirikiana kwa karibu na ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali na kwa kufanya hivyo watakuwa wameepuka tatizo la kuandika habari za kubahatisha.

Ndugu Mtega ameyasema hayo wakati akitoa ufafanuzi kwenye mafunzo kwa waandishi wa habari na wadau kutoka taasisi zisizo za serikali kwenye ukumbi wa Mikutano wa Wakala wa Maabara wa Mkemia Mkuu wa Serikali

photo

 HABARI KAMILI

Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Msajili wa Kemikali za Viwandani na Majumbani ameandaa mafunzo juu ya Matumizi Salama ya Kemikali kwa ajili ya waandishi wa vyombo vya habari (TV,Radio na Magazeti) na asasi zisizo za kiserikali zinazojihusisha na utoaji wa elimu kwa umma kuhusu matumizi salama ya Kemikali.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa ufunguzi wa mafunzo. Mafunzo hayo yanafanyikia kwenye ukumbi wa Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali uliopo ndani ya jengo la "Mkemia House" barabara ya BarackObama (Zamani Ocean Road)
 Washiriki wa mafunzo wakifuatilia Mafunzo
Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali Ndugu Sabanitho Mtega (Katikati) akifungua mafunzo juu ya Matumizi Salama ya Kemikali. Kushoto kwake ni Bi. Everlight Matinga-Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali. Kulia kwa Kaimu Mkemia Mkuu wa serikali ni Kaimu Meneja wa Kanda ya Mashariki ndugu Daniel.

TUJENGE TAIFA LETU
Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi ya Makosa ya Jinai (Forensic Science) na Vinasaba (kwa kimombo ni Director of Forensic Science and DNA Services) Bi. Gloria Cuthbert Omary ametoa wito kwa waandishi wa Habari kuwa kiungo kati ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Jamii katika kuelimisha na kuleta upatanisho kati ya taasisi hiyo na Jamii ili jamii iweze kujifunza na kuelewa juu ya kazi mbalimbali zinazofanywa na Wakala hiyo.

Bi. Gloria amesema kuwa waandishi wa habari wana wajibu wa pekee katika kujenga taifa kwa kuandika habari zilizo sahihi kutoka mamlaka husika na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo watatoa mwanya kwa wanajamii na wadau mbalimbali kuchangia kwa usahihi hoja na mijadala inayohusiana na kazi au matokeo ya Uchuguzi unaofanywa na Wakala wa Mabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali nchini Tanzania.

 WADAU WA KEMIKALI WAZINGATIE SHERIA NA KANUNI
Wadau wa Kemikali nchini wametakiwa kufuata Sheria na Kanuni wakati wa kuingiza, kusafirisha, kuhifadhi, kuuza, kusambaza na wakati wa kutumia kemikali hizo ili kuepusha madhara yanayoweza kuletwa na matumizi yasiyo salama ya kemikali.

Hayo yamesemwa na Bi. Everlight Matinga ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali (katika ofisi ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali) wakati akitoa ufafanuzi kwenye mafunzo hayo kuhusu sheria ya Kemikali za Viwandani na Majumbani ambayo lengo lake ni kulinda afya za wananchi na mazingira

photo

Mgombea udiwani kwa tiketi ya CHADEMA katika kata ya Sombetini Bw. Ally Bananga :Picha na Maktaba.

 Mgombea udiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bw. Ally Bananga katika kata ya Sombetini jijini Arusha ,atangazwa Mshindi kwa kura 2564 na kumbwaga chini mgombea mwenzake wa Chama cha Mapinduzi Bw. David .L. Mollel aliyepata kura 2098 na Mgombea wa Chama cha CUF nae akaambulia kura 37. Kwa picha zaidi Bofya hapa >>>

photo ,

Mwenyekiti wa kamati ya ardhi,malaisili na mazingira,Mh James Lembeli akizungumza katika kikao cha watumishi wa hifadhi ya taifa ya Arusha na kamati ya ardhi,maliasili na mazingira.
Mwenyekiti wa kamati ya Ardhi,maliasili na mazingira,James Lembeli akiwa ameongozana na naibu waziri wa maliasili na utalii,Mahamud Mgimwa pamoja na kaimu mkurugenzi mkuu TANAPA,Martin Loibooki katika lango kuu la kuingia hifadhi ya taifa ya Arusha(ANAPA).
Baadhi ya watumishi wa hifadhi ya taifa ya Arusha.Naibu waziri wa maliasili na utalii,Mh Mahamud Mgimwa akizungumza katika kikao cha watumishi wa hifadhi ya taifa ya Arusha na kamati ya ardhi,maliasili na mazingira.Kikao cha kamati ya ardhi,malasili na mazingira na watumishi wa hifadhi ya taifa ya Arusha.
Mjumbe wa kamati ya ardhi, maliasili na mazingira ,Mh Humud Abdi Jumaa akizungumza katika kikao cha watumishi wa hifadhi ya taifa ya Arusha na kamati ya ardhi,maliasili na mazingira. Kwa hisani ya Wazalendo 25 Blog

photo , ,