Balozi wa Iran nchini Tanzania,Mh.Mehdi Aghajafari akimpokea Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb) alipowasili katika hafla ya kusherehekea siku ya Taifa la Iran iliyofanyika kwenye makazi ya Balozi huyo Jijini Dar es Salaam jana usiku.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb) akizungumza mbele ya wageni mbalimbali walioalikwa katika hafla ya siku ya Taifa la Iran iliyofanyika kwenye makazi ya balozi wa Iran Jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Syria nchini, Mhe.Abdulmonem Annan (kushoto) Jaji mkuu wa Tanzania,  Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati) na Balozi wa Yemen nchini, Mhe.Abdulla Hassan Alamri wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi kwenye hafla ya Siku ya Iran, Naibu waziri Dkt. Mahadhi.
 Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahaya (kulia) akiwa na Maafisa kutoka Wizara hiyo Bw. Mkumbwa Ally (kushoto) na Bw. Leonce Bilauri (katikati) wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri (hayupo pichani) katika hafla hiyo.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akisalimiana na Balozi wa Syria nchini Mhe. Abdulmonem Annan kwenye sherehe hizo.
 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe.Mohamed Chande Othman akizungumza jambo na  Mhe.Dkt.Mahadhi kwenye hafla ya siku ya Iran.
Picha na Reuben Mchome
================================================
STATEMENT BY HON. DR. MAHADHI JUMA MAALIM, (MP) DEPUTY MINISTER OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA ON THE OCCASION OF THE NATIONAL DAY OF THE ISLAMIC REPUBLIC OF IRAN DAR ES SALAAM, 11TH FEBRUARY, 2015
Your Excellency Ambassador Mahdi, Aghajafari Ambassador of the Islamic Republic of Iran;
Your Excellency Juma Alfani Mpango, Ambassador of the Republic of Congo and Dean of the Diplomatic Corps;
Your Excellency Nasri Abujaish, Ambassador of the State of Palestine, and Dean of the Arab Group
Your Excellencies Ambassadors and High Commissioners;
Your Excellencies Heads of Diplomatic Missions;
Your Excellencies Heads of International Organizations;
Distinguished Guests;
Ladies and Gentlemen,
I feel very honoured to stand before you on this special evening when we mark the auspicious event of the 36th National Day of the Islamic Republic of Iran. Indeed it is a particular privilege to join you all this evening as I represent the Government and the people of the United Republic of Tanzania to celebrate this historic day in the history of your beautiful country Your Excellency.
Your Excellency,
Distinguished Guests,
Ladies and Gentlemen,
At this juncture, allow me therefore, on behalf of the Government and the People of the United Republic of Tanzania, to take this opportunity to extend to Your Excellency, and through you to the Government and the People of the Islamic Republic of Iran, our profound and heartfelt congratulations on the occasion of celebrating the 36th Anniversary of the Islamic Revolution of your country.
Your Excellency,
As we join you in this auspicious occasion, I wish to express my satisfaction on the bilateral relations that so happily exist between our two countries and our peoples despite being geographically separated by a long distance.
Such a good relationship can be traced back 1,000 years ago, when Iranians, then under the Shiraz Empire sailed to East Africa.
Tanzania and Iran also have a connection of culture, where there is some similarities of words in both Swahili as well as Persian languages. The Swahili words, "chai" = tea, "achari" = pickle, "serikali" = government, "diwani" = councillor, "sheha" = village councillor, are some of the words also used in Persian bearing testimony to the older connections with Persian merchants. 
Your Excellency,
Distinguished Guests,
Ladies and Gentlemen,
Our two countries already have a good framework for bilateral cooperation.
This is the Joint Permanent Commission (JPC), to coordinate cooperation in the trade, economic, technical and cultural spheres. We are all aware of the inherent obstacles that have militated against the role initially envisaged for the Joint Commission. It is our duty, to learn from our experiences and work together to find ways to make (JPC) arrangement more effective to strengthen our cooperation.
The two countries maintain good cooperation in different sectors; these include health, agriculture, culture, and from vocational to higher education. The two countries are geared to expand and strengthen cooperation in many areas of mutual interests of both countries.
At the Government level there have been exchange of visits at the national levels, to mention a few and recent ones include the then First Vice President of the Islamic Republic of Iran who visited Tanzania in 2012 and the then Minister of Information, Youth, Culture and Sport Dr. Emmanuel Nchimbi visited Iran in 2012. Last week Hon. Dr. Mohammad Javad Zarif, Foreign Minister of Iran, was in our country for a two day official visit.
At global spheres, both countries have been cooperating in all matters of common concerns in Non Alignment Movements (NAM) and United Nations (UN). Allow me at this occasion to reaffirm our commitment to strengthen the close cooperation that exists between our two friendly countries and people.
Your Excellency,
In contemporary world, we all recognize the power and position of private sector.
Thus, the existing friendly relations between our two countries are set to be the corner stone for further expansion and deepening in trade and investment between our private sectors. The just recent visit by Hon. Dr. Zarif to Tanzania with heavy weight CEOs and other prospective investors from Iran to Tanzania set a stepping stone for forging a close economic cooperation between the two countries by increasing trade and investments. Investors from Iran had fruitful discussions with their counterparts organized by Tanzania Chambers of Commerce, Industries and Agriculture (TCCIA).
Through this spirit of enhancing strong cooperation, Tanzania invites more investors from Iran to come to Tanzania to explore opportunities for investment for mutual benefit of both countries. We can expand economic relations to include areas like agribusiness, agro-processing, iron ore and ore extraction and processing, banking and tourism. To walk the talk, I am very happy to note that during the visit by Hon. Zarif, Tanzania and Iran have signed Bilateral Agreement on the Promotion and Protection of the Investments between the two Countries. On the same vein, the third round of negotiations on Avoidance of Double Taxation and Prevention from Fiscal Evasion (DTA) are underway.
Your Excellency,
Distinguished Guests,
Ladies and Gentlemen,
Your Excellency, once again, it is an honour for me to share with you this celebrations of your great country National Day, and I wish to reiterate our sincere congratulations to Your Excellency and  through you, to the Government and brotherly people of the Islamic Republic of Iran, for marking 36th anniversary of your great Islamic Revolution.
We wish you more success in the coming years and decades.
Thank you all for listening.

photo ,




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua rasmi majengo ya ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa yaliyoko jijini Paris Jumatano jioni Januari 28, 2015. Pamoja naye ni Mama Salma Kikwete, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe, Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe Hamad Msauni na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe Mhe Begum Taj.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na wafanyakazi wa ubalozi baada ya kufungua rasmi majengo ya ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa yaliyoko jijini Paris Jumatano jioni Januari 28, 2015. Pamoja naye ni Mama Salma Kikwete, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe, Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe Hamad Msauni na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe Mhe Begum Taj.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na balozi wa New Zealand nchini Ufaransa baada ya kufungua rasmi majengo ya ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa yaliyoko jijini Paris Jumatano jioni Januari 28, 2015. Katikati ni Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe Begum Taj. New Zealand ndiyo iliyoiuzia Tanzania majengo hayo ambayo ni ya ghorofa tano ya ofisi pamoja na jengo lingine la makazi ya balozi na maafisa wa ubalozi.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mwakilishi wa ubalozi wa Uganda nchini Uraransa baada ya kufungua rasmi majengo ya ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa yaliyoko jijini Paris Jumatano jioni Januari 28, 2015. Katikati Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe Begum Taj. Ubalozi wa Tanzania ulikuwa katika majengo ya ubaloizi wa Uganda kabla ya New Zealand kuiuizia anzania majengo hayo ambayo ya ghorofa tano ya ofisi pamoja na jengo lingine la makazi ya balozi na maafisa wa ubalozi.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kitabu cha wageni baada ya kufungua rasmi majengo ya ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa yaliyoko jijini Paris Jumatano jioni Januari 28, 2015. 


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua na kuweka saini kitabu cha wageni baada ya kufungua rasmi majengo ya ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa yaliyoko jijini Paris Jumatano jioni Januari 28, 2015. Katikati Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe Begum Taj. New Zealand ndiyo iliyoiuzia Tanzania majengo hayo ambayo ya ghorofa tano ya ofisi pamoja na jengo lingine la makazi ya balozi na maafisa wa ubalozi.



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akijichanganya na wageni waalikwa ambao ni mabalozi wa nchi mba,limbali za Afrika pamoja na wana Jumuiya ya Watanzania baada ya kufungua rasmi majengo ya ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa yaliyoko jijini Paris Jumatano jioni Januari 28, 2015. Katikati Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe Begum Taj. New Zealand ndiyo iliyoiuzia Tanzania majengo hayo ambayo ya ghorofa tano ya ofisi pamoja na jengo lingine la makazi ya balozi na maafisa wa ubalozi. PICHA NA IKULU

photo , ,

 Makamu wa Rais wa Isaca Tanzania Chapter ambaye pia ni Ofisa Mtendaji Mkuu Wakala wa Serikali Mtandao, Dk. Jabir Bakari akitoa hotuba yake wakati akifungu semina kuhusu usalama wa mifumo ya kompyuta pamoja na ukaguzi wa mifumo hiyo kwa kuwakutanisha wataalumu na kujadiliana kuhusu ukuaji wa teknolojia na usalama.
Aidha Dk. Jabir alisema kuwa semina hiyo inawakutanisha wataalamu wa mifumo ya kompyuta kutoka ndani na nje ya nchi watakaojifunza na kuongeza utaalamu wa kulinda mifumo ya mitandao. 
Naye Mratibu wa Semina hiyo ambaye pia ni Rais wa Isaca Tanzania, alisema kuwa semina hiyo kwa ajili ya kuelezea wadau wa mitandao kuhusu mwelekeo wa teknolojia duniani na ukubwa wa tatizo katika wizi wa mitandao  'miaka ya nyuma kulikuwa na wizi wa kuvunja katika mabenki lakini siku hizi mbinu za wizi zimebadilika na wezi wanaiba kupitia mifumo ua mitandano hasa kompyuta pamoja na simu, kutoa elimu ya ajili ya mifumo ya kompyuta namna ya kuilinda na kuiendeleza.
Katibu wa Tanzania Chapter, Nemayani Kaduma (kulia)akiwa katika semina hiyo.
Baadhi ya washiriki wa semina ya ya kimataifa kuhusu usalama wa mitandao wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Taasisi ya Isaca Tanzania Chapter, Dk. Jabiri Bakari (hayupo pichani) iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Washiri wa semina wakifuatikilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa.
Washiriki wa semina hiyo.
Washiriki.

George Wahome kutoka Isaca-Kenya akitoa mada kuhusu usalama wa mitandao.
Washiriki wa semina.
Rais wa Isaca Tanzania Chapter, Boniface Kanemba akifuatilia mada katika semina hiyo.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Dun & Bradstreet Credit Bureau Tanzania, Adebowale Atobatele akitoa mada katika semina hiyo.
Rais wa Isaca Tanzania Chapter, Boniface Kanemba akizungumza na waandishi wa habari.
Washiri wa semina hiyo wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa.
Rais wa Isaca Tanzania Chapter, Boniface Kanemba (kulia) akimpongeza Isack Maheri  aliyefaulu mitihani ya ukaguzi wa Mitandao ijulikanayo kama CISA.
Rais wa Isaca Tanzania Chapter, Boniface Kanemba (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais wa Isaca Tanzania, Dk. Jabir Bakari (wa tatu kushoto), Katibu wa Tanzania Chapter, Nemayani Kaduma (kushoto) na Mkurugenzi wa Elimu Mtandao, Dk. Carina Wangwe (kulia) na Peter Baziwe (wa tatu kulia)

photo ,

MKATABA wa kujenga tena umoja na kukiunganisha upya Chama Tawala cha Sudan Kusini cha Sudan People’s Liberation Movement (SPLM) ulitiwa saini usiku wa jana, Jumatano, Januari 21, 2015, katika sherehe ya kufana iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Ngurdoto, Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha.
Mkataba huo unaojulikana kama Agreement on the Re-unification of Sudan People’s Liberation Movement umepongezwa kuwa ni hatua muhimu katika kulitoa taifa changa la Sudan Kusini katika hali ya machafuko, vita vya wenyewe kwa wenyewe, kutoelewana na kutoaminiana, mambo ambayo yameligubika taifa hilo tokea mwishoni mwa 2013 wakati kutokuelewana kulipozuka ndani ya SPLM na hatimaye katika Serikali ya nchi hiyo.
Viongozi waliotia saini ni Mheshimiwa Salva Kiir Mayardit, Rais wa Sudan Kusini ambaye pia ni Mwenyekiti wa SPLM na anayeongoza kundi linalojulikana kama SPLM in Government (SPLM-IG), Mheshimiwa Dkt. Riek Machar ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa SPLM na pia aliyekuwa Makamu wa Rais wa Sudan Kusini anayeongoza kundi la SPLM in Opposition (SPLM-IO) na Dkt. Deng Alor Kuol ambaye anaongoza kundi la SPLM Leaders- Former Detainees (SPLM Leaders – FD).
Sherehe hiyo ilishuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho ndicho kimesimamia mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo. Rais Kikwete pia ndiye mdhamini mkuu wa Mkataba huo.
Wengine walioshuhudia tukio hilo muhimu ni Rais wa Uganda, Mheshimiwa Jenerali Yoweri Kaguta Museveni; Rais Uhuru Muigai Kenyatta wa Kenya; Naibu wa Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa, Makamu Mwenyekiti wa zamani wa CCM Mheshimiwa John Samwel Malecela ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo na Katibu Mkuu wa CCM Mheshimiwa Abdulrahman Kinana ambaye alikuwa mwezeshaji wa mazungumzo.
Mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo yalianza mwishoni mwa mwaka jana baada ya Rais Kikwete na Chama cha CCM kuombwa na Rais Kiir Mayardit kukubali chama hicho tawala cha Tanzania kutumia uzoefu na ujuzi wake wa miaka mingi wa uongozi na siasa kujaribu kuleta suluhu ndani ya SPLM.
Mazungumzo hayo ya kutafuta suluhu ambayo yamefanyika kwa awamu mbili, ya kwanza yakiwa yamefanyika Oktoba mwaka jana na pili yakiwa yameanza mwanzoni mwa mwezi huu, Januari 2015,  yameongeza thamani kwenye mazungumzo mengine yanayofanyika Addis Ababa, Ethiopia chini ya usimamizi wa taasisi ya IGAD na yanayojadili jinsi ya kurejesha amani nchini humo.
Viongozi wa SPLM wanaamini kuwa kwa sababu mgogoro wa kisiasa nchini mwao ulianzia ndani ya chama hicho na kwa sababu SPLM ndicho chombo pekee ambacho kinawaunganisha wananchi wote wa Sudan Kusini, basi busara inaelekeza kuwa suluhu ianze kutafutwa ndani ya chama hicho.
Mkataba wa jana, kimsingi, unalenga kuweka mazingira ya kujenga utulivu, maelewano, amani na umoja wa kudumu ndani ya chama hicho na nchini humo kwa kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mambo ya msingi yaliyokubaliwa kuhusu shughuli za siasa, uongozi na oganisheni ya chama hicho yanafanyika bila kukawia.
Mkataba huo pia unalenga kuhakikisha kuwa chama cha SPLM kinabuni na kutekeleza sera za kuondokana na ukabila, makundi yenye mitazamo finyu na mwenendo wa kijeshi katika siasa za Sudan Kusini.
Aidha, Mkataba huo unalenga kuhakikisha kuwa chama cha SPLM kinafanya mageuzi ya kuanza kujenga utamaduni wa kuvumiliana na ujenzi wa misingi ya demokrasia.
Mkataba huo pia unataka watu wote ambao walishiriki katika mauaji na umwagaji damu katika vita vya wenyewe kwa wenyewe wasiruhusiwe kugombea wala kushika nafasi ya uongozi wa umma ndani ya chama hicho.
Pia viongozi wote wa Sudan Kusini wanatakiwa, chini ya Mkataba huo, kuwaomba radhi wananchi wa nchi hiyo ya Sudan Kusini kwa kuruhusu nchi hiyo kuingia katika machafuko ya umwagaji damu mkubwa.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
22 Januari,2015

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe akikaribisha viongozi na wajumbe katika mkutano huo
 Waziri Mkuu Mstaafu na Makamu Mwenyekiti wa zamani wa CCM Mheshimiwa John Samwel Malecela ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo akisoma muhtasari wa mazungumzo hayo

 Sehemu ya ukumbi wa mkutano huo

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza utiaji wa saini wa  Mhe. Salva Kiir Mayardit  Rais wa Sudan Kusini ambaye pia ni Mwenyekiti wa SPLM na anayeongoza kundi linalojulikana kama SPLM in Government (SPLM-IG), Mheshimiwa Dkt. Riek Machar ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa SPLM na pia aliyekuwa Makamu wa Rais wa Sudan Kusini anayeongoza kundi la SPLM in Opposition (SPLM-IO) na Dkt. Deng Alor Kuol ambaye anaongoza kundi la SPLM Leaders- Former Detainees (SPLM Leaders – FD). 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) na Bw. Deng Alor Kuol wakionesha hati baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa pongezi kwa Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) na Bw. Deng Alor Kuol

baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia wakati  Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono na

kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia wakati  Rais Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (kushoto) na Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana mikono na

kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa  makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015 usiku.

photo ,


 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua pazia kuzindua nyumba za kisasa za makazi ya wanajeshi akisaidiana na Balozi wa China nchini Mhe Lu Youqing, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa Dkt Hussein Mwinyi na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia kwa pamoja na baadhi ya viongozi baada ya kuzindua nyumba za kisasa za makazi ya wanajeshi akisaidiana na Balozi wa China nchini Mhe Lu Youqing, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa Dkt Hussein Mwinyi na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili tayari kuzindua nyumba za kisasa za makazi ya wanajeshi Gongo la Mboto jijini Dar es salaam. 
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa mradi huo wa nyumba za kisasa za makazi ya wanajeshi Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.
  Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa mradi huo wa nyumba za kisasa za makazi ya wanajeshi Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.
  Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa mradi huo wa nyumba za kisasa za makazi ya wanajeshi Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.

Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya wanajeshi baada ya kuzindua  nyumba za kisasa za makazi ya wanajeshi Gongo la Mboto jijini Dar es salaam. PICHA NA IKULU

photo , ,