Baadhi ya Vitu vinavyopatikana kwenye mnada wa Wami Dakawa
 Mbuzi hawa walishauzwa mapema
 Nyama Choma hupatikana kwa wingi
 Mbuzi Choma pia wapo

Baadhi ya Vibanda vinavyotoa huduma ya chakula na vinywaji

photo

Bondia Francis Cheka wa Tanzania (kulia) akimuadhibu mpinzani wake Mmarekani, Phill Williams, wakaati wa pambano lao la raundi 12 la kuwania Ubingwa wa Dunia uzito wa Super Middle (WBF) lililofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu. Katika pambano hilo Bondi Mtanzania Francis Cheka ameweza kumgalagaza kwa Pointi mpinzani wake na kutwaa ubingwa huo.
*******************
Na Mwandishi Wetu
HATA hivyo pambano hilo pamoja na yale ya utangulizi yaliingia dosari baada ya wachezaji kama Alfonce Mchumiatumbo, aliyekuwa akizichapa na Chupac Chipindi katika pambano lao la utangulizi la raundi sita, kugoma kupanda ulingoni kwa kile walichokuwa wakieleza mabondia hao kuwa wanahitaji kumaliziwa pesa zao za mkataba wa kucheza mechi hizo kabla ya kupanda ulingoni. 
Nao mabondia Mada Maugo na Thomas Mashali, pia waligoma kupanda ulingoni wakishinikiza kumaliziwa pesa zao kwanza jambo ambalo lilifanya kuzua taflani ukumbini hapoa huku mapambano yakichelewa kuanza.
Ilipofika muda wa Cheka kupanda ulingoni pia alisikika mtangazaji akimuita muandaaji wa mapambano hayo ili kufika chumba alichokuwa Bondia mtanzania, Francis Cheka ili kumalizana naye mkwanja ili akubali kupanda ulingoni.
Alisikika Cheka akimuwakia muandaaji huyo kuwa, '' Nini Mmarekani hata angekuwa Mchina, nimalizie changu kwanza ili nipande ulingoni, ambalo pia lilichukua muda wa majadiliano hadi kuingiliwa kati na wadhamini na wadau wa ngumi waliotangaza kujikomiti kulipa pesa hizo wanazodai mabondia, ndipo mabondia hapo wakapanda ulingoni.

Aidha katika pambano la raundi 10 la mabondia Mada Maugo na Thomas Mashali la kuwania Ubingwa wa WBF wa Afrika, Thomas Mashali ameweza kumshinda kwa pointi 2 tu mpinzani wake Mada Maugo na kutwaa Mkanda huo wa ubingwa wa WBF wa Afrika.
Na katika pambano la Utito wa Juu la utangulizi la Raundi sita kati ya Bondia Alfonce Mchumiatumbo na Chupac Chipindi, Mchumiatumbo amemchapa kwa KO mpinzani wake katika raundi ya tano, baada Chupac kunyoosha mikono juu kuashiria na wasaidizi wake kutupa taulo ulingoni kuashiria kushindwa kumalizia mchezo huo.  
 Waziri wa Habari, Fenella Mukangara (katikati) akipozi na mabondia Phill na Cheka, ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa pambano hilo la kimataifa.
 Waziri wa Habari, Fenella Mukangara (wa pili kushoto) akimvisha Mknda wa Ubingwa wa Dunia wa WBF Bondia Francis Cheka baada ya kumchapa kwa Pointi mpinzani wake Mmarekani, Phill Williams, katika pambano lao la raundi 12 lililofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu.
 Mashabiki wa Cheka wakifurahi na kumbeba baada ya kutangazwa mshindi.
 Bondia Mmarekani Phill Williams (kulia) akichapana na Francis Cheka wa Tanzania katika pambano lao lililomalizika usiku huu kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee.
 Mabondia hao wakiliana Timing.......
 Cheka (kulia) na Phill wakichapana......
 Cheka (kulia) na Phill,wakiendelea kuchapana 
We subiri inakuja hiyooooo
 Sehemu ya mashabiki wa mchezo huo waliofurika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee kumshuhudia Cheka akimchakza Mmarekani. kwa Picha Zaidi Bofya hapa>>>

photo ,

Wanasheria Amani Mwaipaja (Mwenye Fulana) ambaye pia ni mwasisi wa Blog hii akiwa na Mwanasheria Msomi Berious Nyasebwa walipokutana na kutembelea ofisi  ya Blog hii mkoani Morogoro 

Wanasheria hao wameishauri timu ya Mwaipaja Blog kujikita zaidi katika habari na matukio ya kijamii yanayotokea mkoani Morogoro kwakuwa wadau wengi wanahitaji kufahamu yale yanayotokea katika jamii hususan maeneo ya vijijini

photo

Mwaipaja Blog imepata ofisi mpya iliyoko ndani ya ofisi za Taasisi ya Nakya Group. katika kuboresha huduma ya mwasiliano kwa njia ya blog, Timu ya Mwaipaja Blog imejipanga kufanya mageuzi makubwa katika tasnia ya habari.Wadau wa Blog hii kaeni mkao wa kula
 Meza ya Blogger pamoja na baaadhi ya vitendea kazi kama invyoonekana pichani

photo


photo


photo


Kwa mbaali unaweza kuiona milima ya Uluguru inavyoonekana...Mji kasoro Bahari

photo


photo




photo






 Stand ya Daladala-Mjini
 Round About ya Mjini


photo

 Mwanasheria Berious Nyasebwa akiwa na Msanii Nguli wa Hip Hop Nchini Tanzania Afande Sele ambaye amelazwa kwenye hospitali ya Wazazi ya Uluguru
 Mwanasheria Amani Mwaipaja ambaye ni Mwasisi wa Blog hii akiwa na Afande Sele wodini



photo


Moja ya kitabu kilichoandikwa na Mwanasheria Amani Mwaipaja ambaye ni Mwasisi wa Blog hii kikiwa kimeandikwa kwa lugha ya kiswahili chepesi ili kumwezesha mwananchi wa kawaida kusoma na kuelewa haki mbalimbali alizo nazo.

Kitabu hiki ambacho kimeanza kusambazwa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Morogoro kinahitaji kufikishwa kila sehemu ya Tanzania ili kumsaidia mwananch wa kawaida katika kuifikia haki yake.

Kwa atakayehitaji kuwa wakala wa kitabu hiki ndani ya Tanzania anaombwa kuwasiliana na blog hii kwa mawasiliano yaliyopo hapo juu ili apewe utaratibu

photo