Wakili Msomi Valentine Kamugisha (mwenye shati Jeupe) akiwa na Mwasisi wa Blog hii Mheshimiwa Amani Mwaipaja ndani ya Banda la Sheria lililomo ndani ya viwanja vya maonyesho ya wakulima Nanenane Morogoro
 Waikili Msomi Valentine Kamugisha akiwa nje ya Banda la Sheria



BANDA LA SHERIA LAWA KIVUTIO NANENANE
Banda la sheria lililomo ndani ya viwanja vya maonyesho ya wakulima nanenane Morogoro limekuwa kivutio kwa watu mbalimbali wakiwemo wakulima, wanafunzi na wanasheria kutokana na ukweli kuwa Banda hilo limekuwa likitoa msaada wa kisheria kwa watu mbalimbali wenye matatizo ya kisheria.

Mbali na banda la sheria kutoa ushauri kuhusu masuala ya kisheria lakini ndani ya banda hilo kuna vitabu, vijarida na vipeperushi mbalimbali vinavyohusu sheria mbalimbali za nchi yetu
 
 

+-

photo





Wakili Msomi Valentine Kamugisha (Wa Kwanza Kulia mwenye Shati Jeupe) akiwa na baashi ya maafisa wa Banda la Wakala wa Mbegu za Kilimo-ASA



photo


photo











photo


Ndugu Abbas Mbwela, Mjasiliamali anayechipukia akiwa katika viwanja vya Maonyesho nanenane.

photo

MDAU

0 Comments Imetumwa na Unknown at 8/04/2013 03:00:00 PM

Naibu  Katibu wa TASO-Kanda ya Mashariki Morogoro Bwana Dastan Lukosi akiwa amepozi nje ya Banda la Sheria alipokuwa akitembelea shughuli mbalimbali ndani ya Viwanja vya Maonyesho ya Wakulima-Nanenane Morogoro

photo

J 






 Bi. Joyce akitoa maelezo kwa timu ya Mwaipaja Blog juu ya  matumizi ya Mafuta yatokanayo na Nazi isiyokomaa

 Mtafiti akitoa maelezo ndani  ya Banda la Wizara ya Kilimo Chakula Na Ushirika ndani ya Banda la Wizara hiyo


 Mtafiti Joseph Mbogoni akitoa maelezo kwa wanaottembelea banda hilo

Baadhi ya watu wakiangalia bidhaa na kupata taarifa ya namna wizara inavyofanya kazi zako ikiwemo kufanya tafiti za kilimo
Baadhi ya Bidhaa zikiwa katika Banda la Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika ndani ya viwanja vya maaonyesho ya wakulima-Nanenane Morogoro 2013

photo ,








Banda la Msaada wa Sheria lililopo ndani ya viwanja vya maonyesho ya wakulima nanenane yanayofanyika Mkoani Morogoro. Banda hili linaendeshwa kwa ufadhili wa Mwanasheria Mshauri na Mtafiti-Amani Mwaipaja

photo


morgan-tsvangirai 
Mkuu wa waangalizi wa uchaguzi mkuu wa Zimbabwe kanda ya Afrika Kusini, Bernard Membe, ameelezea wasiwasi mkubwa kuwa daftari la wapiga kura lingali kutolewa siku moja kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika nchini humo.
Hii ni licha ya kuwa daftari hilo kuwa kiungo muhimu kwenye uchaguzi utakaofanyika Jumatano.
Taarifa zinazohusiana
Siasa
Chama cha MDC chake hasimu wa rais Mugabe, Morgan Tsvangirai, kimesema kinajiandaa kwenda mahakamani kuweza kupata daftari hilo.
Shughuli ya kupiga kura itamaliza serikali ya Muungano kati ya MDC na chama cha rais Mugabe Zanu-PF .
Rais Mugabe anataka kugombea urais hata baada ya kuitawala nchi hiyo kwa miaka 33. Anamenyana na waziri mkuu Morgan Tsvangirai
Ikiwa imesalia siku moja kabla ya upigaji kura, hakuna chama kilichopokea sajili la wapiga kura.
Mahasimu hao wawili wakuu, wamekuwa wakigawana mamlaka tangu mwaka 2009, baada ya mkataba kuafikiwa kwa usaidizi wa muungano wa nchi za ukanda wa Afrika Kusini SADC, ili kumaliza mgogoro wa kisiasa uliosababisha vurugu za baada ya uchaguzi 2008.
Bwana Membe, ambaye ni waziri wa mambo ya nje wa Tanzania alisema kuwa daftari la wapiga kura sio siri kubwa na kuwa lilipaswa kutolewa zamani sana.
“lazima itolewe kwa wapiga kura ili waweze kuhakiki majina yao, waweze kujua watakapopiga kura,” alisema bwana Membe.
Katibu mkuu wa chama cha MDC Tendai Biti alisema kuwa chama hicho kitachukua hatua za kisheria dhidi ya tume ya uchaguzi ili kuweza kupata sajili hilo.
Chanzo:BBC

photo

Mwanasheria Mshauri (Consultant) na Mwanaharakati wa Haki za Binadamu nchini Tanzania Ndugu Amani Mwaipaja anatarajiwa kuzindua Rasmi Huduma yake ya Ushauri wa Kisheria kwa nji ya Simu ifikapo katikati ya Mwezi Agosti Mwaka Huu.

Akizungumza na timu ya Mwaipaja Blog Mwanasheria huyo amesema kuwa lengo la huduma hiyo ni kuweza kuisaidia zaidi jamii iishiyo pembezoni na ambayo imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo kwa kutembea umbali mrefu ikitafuta msaada wa kisheria.
Kupitia huduma hiyo, watu mbalimbali watakaokabiliwa na matatizo ya kisheria wataweza kupata ushauri wa kisheria na kupewa mwongozo kwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno kwa kuuliza swali au kuomba ufafanuzi.

Akielezea upatikanaji wa huduma hiyo ya ushauri wa kisheria kwa njia ya simu mwaipaja alieleza taratibu za kujiunga kwa kuandika neno mwaipaja (Acha Nafsi) kisha andika ujumbe wako alafu utume kwenda namba 15678.

Mwaipaja alitoa wito kwa wote wenye kuhitaji huduma hiyo kujiunga na huduma hiyo kuanzia sasa kwakuwa tayari huduma hiyo imeshaanza kufanya kazi.

photo

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Pereira Silima(kulia) pamoja na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Thailand, Mhe. Sura Pong Tovichakehaikul(kushoto)wakisa ini Mkataba wa kubadilishana Wafungwa kati ya Tanzania na Thailand(Picha na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza)


photo

Rais Kikwete akimjulia hali mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, Said Mohamed Saad.
 
HABARI KAMILI
Said ambaye ndiye mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, yenye maduka mengi makubwa ya vitu vya nyumbani ndani ya Dar es Salaam na mikoa kadhaa ya Tanzania, anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini lakini mmoja wa watu waliomshuhudia, amefafanua jinsi hali ilivyo mbaya.
“Ameungua sana, tunatarajia kati ya kesho au keshokutwa (wikiendi iliyopita) atafanyiwa oparesheni ya jicho. Jamani tindikali ni mbaya sana, usimmwagie mwenzako. Ndugu yetu ameharibika sana,” kilisema chanzo chetu kwa ombi la kutotajwa jina gazetini, kikaongeza:
“Kila anayemjua vizuri, anapomwona anamwaga machozi. Picha za jinsi alivyoathirika baada ya kumwagiwa tindikali zimevuja mpaka kwa familia, ni kilio kwa ndugu. Wanawake wanalia zaidi.”

JK ATINGA HOSPITALI
Wiki iliyopita, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, alikuwa kwenye ziara ya kikazi nchini Afrika Kusini alipokwenda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini ya Afrika (SADC).
Mkutano huo ni wa Pande Tatu za SADC (Troika of SADC) na akiwa huko, alipata fursa ya kwenda kumjulia hali katika hospitali aliyolazwa ambayo haijajulikana jina.
Chazo chetu kilisema: “Rais Kikwete alisikitika sana. Wakati anatoka wodini alisonya. Alionesha jinsi alivyosikitishwa na unyama aliotendewa Said.”


photo