Kwa mbali Turubai likionekana...wanafunzi wakiwa katika majonzi makubwa baada ya kupotelewa na mwanafunzi mwenzao...Rajabu Tenga aliyeuawa na majambazi jana jioni baada ya majambazi hayo kuvamia supamaket iliyoko karibu na chuo kikuu Mzumbe Mbeya campas.
WAOMBOLEZAJI
Belius na Mimi Tukiwa katika hali ya huzuni baada ya kupotelewa na mwimbaji mwenzetu (marehemu Tenga) tuliyekuwa tukiimba nae pamoja katika kundi la A cappella la Mzumbe Brothers.Marehemu Tenga alikuwa akiimba sauti ta nne (bez)
Huzuni ikiwa imetawala katika msiba...hapa wanafunzi wanasikiliza maelezo kutoka kwa mawaziri wa serikali ya wanafunzi (hawapo pichani)
Rajabu Tenga -mwanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe kampas ya Mbeya ambaye amefariki jana jioni baada ya kupigwa risasi na majambazi waliovamia supa maket moja iliyoko jirani na chuo cha Mzumbe.
Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda nyumbani kwao Same zinafanyika.
Marehemu Tenga alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa pili- digrii ya sheria.
MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI................................
may be.....papot to be....msiandae malalamiko...kwa upande wangu nimeingia darasani mara kadhaa kufundisha...sijui kwa wenzangu...infact... all lekchalaz are equal.
Usinckeshe.....wakati mwingine mtu hulazimika kuangua kicheko pale pale point inapokuonekana.....Lintel akifurahi meno 30 na nje yote mbili katika mkutano wa wanafunzi ulioitishwa na co-ordinata na mkurugenzi msaidizi wa huku ughaibuni kwetu...Mbeya kampas
Hapa nimepozi na .......msije mkafikiri ndiye naniii...wangu
Ughaibuni kuzuri jamani...umeona kijani kibichi jinsi kilivyokubali hapo chini?
David Sechome-mwenye tshirt nyeupe akiwa katika mkutano uliofanyika jana ukijumuisha wanafunzi wote wa ughaibuni...
Mwanadada Lintel Komba ( anaetabasam)nae alikuwepo katika mkutano
Waziri mkuu wa uingereza Tony Blair (wa kwanza kushoto-mwenye tai nyekundu) akiwa amepozi na mmoja wa wananchi wake...imetoka eh?
Jamaa akionesha uhodari wake katika kile kinachoitwa...acrobatic................
Kuna kale katabia ka kuiga kila tunachokiona....tuige na hii
Hivi karibuni nikiwa katika safari yangu kuelekea ughaibuni....Mbeya Kampas..niliamua kushuka mji kasoro Bahari ili kusalimia ndugu na jamaa...hapa ni maeneo ya kilakala sekondari...kwa nyuma safu za milima ya uluguru zinaonekana live bila chenga.
Tatizo la kujiunganishia mipira ya maji halipo Dar peke yake...
Bahadhi ya barabara za mji kasoro bahari zinavyoonekana...muda mfupi tu ujao nitakuwa naelekea ughaibuni...tutakutana hukohuko
Mfalme mswati wa zwaziland akiwa katika pozi na mke wake wa kumi na mbili.
Mfalme mswati akiwa katika vazi la kiasili
Mama wa mfalme mswati
Mabiti wakielekea katika milima ya uswazi kwa ajili ya ngoma na sherehe ambapo mfalme hujitwalia mke kutoka miongoni mwa hawa unaowaona...sherehe hizi hufanyika kila mwaka kati ya mwezi agasti na disemba.
Mtoto wa mfalme mswati...ambaye hivi anasoma huko ughaibuni -uingereza..
Kiongozi wa Kundi la wanaume halisi...Juma Kasim Necha akiwa katika pozi baada ya kutoka kupafom katika tamasha la siku sita la Sauti za Busara huko Ngome Kongwe (stone town) Zanzibar
Mwanamuziki Jose kamilion kutoka Uganda nae alishiriki katika tamasha kubwa la muziki linaloshirikisha wanamuziki kutoka sehemu mbalimbali duniani alikuwepo katika usiku wa sauti za busara huko Zanzibar...jamaa yupo mbioni kutoa albamu zake mbili na baada ya hapo anategemea kujiingiza katika fani ya uigizaji wa filamu.
Mwanadada Chiwoniso kutoka nchini Zimbabwe akifanya vitu vyake katika tamasha la SAUTI ZA BUSARA huko ngome Kongwe (stone town)
Mfalme wa Hip Hop kutoka Rock City- Mwanza Falid Kubanda (Fid q) nae alikuwepo.
Maduhu Emanuel (wa kwanza kushoto)ambaye pia ni katibu wa Kampuni ya Acappella Kwanza,Amani mwaipaja-Mwenyekiti wa Kampuni ya Acappella Kwanza (mwenye Batiki),Enos Kazuzu (wa tatu kutoka kushoto-mkuu wa mawasiliano)na Yusuph Mcharia (makam mwenyekiti-mwenye shati jeupe). Picha hii imepigwa mara tu baada ya kutoka kuzungumza na waandishi wa habari juu ya Tukio la tamasha kubwa la kihistoria la muziki wa A cappella litakaloshirikisha vikundi mbalimbali nchini Tanzania.
Hawa ni vijana wa Sonda ya Dlhu kutoka ukonga jijini Dar es salaam..vijana hawa wanaimba muziki wa A cappella ama muziki usiotumia ala za muziki.Ni vijana wadogo kiumri lakini hufanya mambo makubwa wawapo jukwaani.Wanaimba muziki wa Injili.Vijana hawa pia watakuwepo katika Tamasha la muziki wa Acappella litakalofanyika siku ya jumapili katika ukumbi wa Msimbazi centre.Vijana hawa uimbaji pia nyimbo za makabila mbalimbali.Wana albam moja ambayo itazinduliwa hivi karibuni.
Ni jambo la kawaida tunapokuwa Tukuyu kuvaa makoti kama haya...jamaa wamenitumia picha hii wakiwa wamepozi walipotembelea Tukuyu...vipi hapa kwetu Bongo?

NITAPITA ULIPOPITA NA KUACHA ALAMA ZA NYAYO ZAKO
Mzee Mandela katika pozi siku ya hepibathdei yake
Mara moja moja huwa anapiga suti
Akina mama wakifurahia matunda ya Tanzania.katikati..Mh Asha Rose migiro aliyekula bingo baada ya kuchaguliwa kuwa naibu katibu mkuu wa umoja wa mataifa...Aunt emmy umeiona hii?
Kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam lile tamasha la muziki wa A cappella lilokuwa likisubiriwa kwa muda mrefu sasa limewadia....ni tarehe 11/03/2007 katika ukumbi wa Msimbazi centre kwa kiingilio cha shs 3000 kwa watu wazima na shs 1000 kwa watoto...usikose kuja kushuhudia tamasha la waimbaji wenye vipaji...nimedokezwa kuwa mgeni rasmi atakuwa yule mama aliyekuwa mbunge wa jumuiya ya Africa mashariki....mama Hulda Kibacha.
Waandaaji wa Tamasha hilo..A cappella Kwanza wamejipanga vizuri kwa ajili ya tamasha hilo la kihistorianchini.... hili ni tamasha la kwanza la aina hii kufanyika nchini likishirikisha vikundi mbalimbali vinavyoimba muziki waAcappella.
Mratibu watamasha hilo enos misoji kazuzu anadokeza kuwa baadhi ya vikundi vitakavyoshiriki katika tamasha hilokubwa ni pamoja na
1. busy bee kutoka temeke
2. sonda ya dilu kutoka ukonga
3. jerusalem brothers
4. king's ambassadors
5. the final trumpet
6. the voice A cappella kutoka magomeni
7. steps to christ
na vikundi vingine vingi
Tamasha hilo pia litasindikizwa na waimbaji wanaotumia vyombo kama the peace,nuru kitambo,prince amos,nyakorema na wengineo wengi
usikose ...kaka michuzi umeipata hii?matukio mbalimbali kuhusu tamasha hilo yatawajia kupitia blog hii makini...
Aunt Emmy upo hapo?...nawe pia usikose
Kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam lile tamasha la muziki wa A cappella lilokuwa likisubiriwa kwa muda mrefu sasa limewadia....ni tarehe 11/03/2007 katika ukumbi wa Msimbazi centre kwa kiingilio cha shs 3000 kwa watu wazima na shs 1000 kwa watoto...usikose kuja kushuhudia tamasha la waimbaji wenye vipaji...nimedokezwa kuwa mgeni rasmi atakuwa yule mama aliyekuwa mbunge wa jumuiya ya Africa mashariki....mama Hulda Kibacha.
Waandaaji wa Tamasha hilo..A cappella Kwanza wamejipanga vizuri kwa ajili ya tamasha hilo la kihistorianchini.... hili ni tamasha la kwanza la aina hii kufanyika nchini likishirikisha vikundi mbalimbali vinavyoimba muziki waAcappella.
Mratibu watamasha hilo enos misoji kazuzu anadokeza kuwa baadhi ya vikundi vitakavyoshiriki katika tamasha hilokubwa ni pamoja na
1. busy bee kutoka temeke
2. sonda ya dilu kutoka ukonga
3. jerusalem brothers
4. king's ambassadors
5. the final trumpet
6. the voice A cappella kutoka magomeni
7. steps to christ
na vikundi vingine vingi
Tamasha hilo pia litasindikizwa na waimbaji wanaotumia vyombo kama the peace,nuru kitambo,prince amos,nyakorema na wengineo wengi
usikose mtu wangu...kaka michuzi imeipata hii?matukio mbalimbali kuhusu tamasha hilo yatawajia kupitia blog hii makini...usikose
Aunt Emmy upo hapo?...nawe pia usikose
















