Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akimpongeza Mkurugenzi wa JAMII KWANZA Bw. Amani Mwaipaja baada ya kuanzisha kampeni ya Jamii Kwanza mjini Morogoro.

Mgeni rasmi Mhe. Bernard Membe akikabidhiwa picha yake iliochorwa kwa mkono na msanii Bw. Chipenya wakati wa uzinduzi wa kampeni ya JAMII KWANZA nadni ya Ukumbi wa Glonency -88 mjini Morogoro.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Lazaro Nyalandu akitoa Mchango wake kwa Kampeni ya  JAMII KWANZA.



Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa na nakala ya kitabu changu cha Zijue Sheria na Haki Zangu

photo ,


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Eng. Omari Jumanne Bakari kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO).

Kulingana na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Y. Sefue, uteuzi huo umeanza Desemba 04, mwaka huu, 2013. Eng. Omari Jumanne Bakari ni Mtafiti Mwandamizi katika Tume ya Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam.

Eng. Omari Jumanne Bakari ni Mtanzania mwenye elimu, weledi na uzoefu ambao umemfanya Mheshimiwa Rais aamini kuwa atakapoongoza SIDO, atasaidia kukidhi matarajio ya taifa kwa kueneza ujasiriamali, uwekezaji,uzalishaji na kutoa nafasi za ajira katika ngazi ya viwanda vidogo na vya kati kama msingi imara wa uchumi wa Tanzania, ikiwemo kwa kuingiza sayansi, teknolojia na ubunifu katika viwanda vidogo vidogo.
         “Mwisho”
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
DAR ES SALAAM.

16 Desemba, 2013

photo ,


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe George W. Bush na Mkewe Laura Bush wakiwa jukwaa la viongozi na watu mashuhuri baada ya Kuadhimisha Kumbukumbu ya Kifo cha aliyekuwa kiongozi mashuhuri wa Afrika Kusini na duniani, Mheshimiwa Nelson R Mandela leo Desemba 10, 2013 katika uwanja wa FNB jijini Johannesburg.Picha na IKULU
---
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Desemba 10, 2013, ameungana na viongozi wa mataifa mbali mbali duniani na maelfu ya wananchi wa Afrika Kusini Kuadhimisha Kumbukumbu ya Kifo cha aliyekuwa kiongozi mashuhuri wa Afrika Kusini na duniani, Mheshimiwa Nelson R Mandela.

Maelfu kwa maelfu ya wananchi wamehimili mvua kubwa iliyokuwa inanyesha kwa nguvu kwenye Uwanja wa Michezo wa FNB mjini Johannesburg kumwaga Mzee Mandela ambaye alikuwa ishara kuu ya upinzani wa siasa za ubaguzi wa rangi za makaburu wa Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mandela ambaye alifariki duniani Ijumaa iliyopita, Desemba 5, 2013, alikuwa Kamanda wa Jeshi la Ukombozi la Chama cha African National Congress la Umkhoto we Sizwe akafungwa jela kwa uhaini kwa miaka 27 na utawala wa Makaburu.

Baada ya kutoka jela mwaka Februari 1990, Mzee Mandela alichaguliwa kuwa Rais wa Kwanza wa Afrika Kusini ya mwaka 1994. Lakini Mheshimiwa Mandela alitumikia kipindi kimoja tu cha miaka mitano na kukataa kutumikia kipindi cha pili.

Kiasi cha viongozi 91 kutoka sehemu duniani wamehudhuria Kumbukumbu hiyo iliyokuwa na kila aina ya mchanganyiko wa hisia – wengine wakiwa na majonzi na wengine wakicheza na kuimba kwa muda wote wa shughuli hiyo iliyochukua kiasi cha jumla ya saa tano. 

Mbali na Rais Kikwete ambaye amefuatana na Mama Salma Kikwete, marais wengine mashuhuri duniani waliohudhuria Kumbukumbu hiyo ni Mheshimiwa Barack Obama wa Marekani, Mheshimiwa Francois Hollande wa Ufaransa, Waziri Mkuu wa Uingereza, Mheshimiwa David Cameroun na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Ban Ki Moon.

Kumbukumbu hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi wa zamani wa Marekani wakiwemo marais watatu wa zamani wa Marekani – Mheshimiwa Jimmy Carter, Mheshimiwa Bill Clinton na Mheshimiwa George W Bush na mawaziri wakuu wawili wa zamani wa Uingereza, Mheshimiwa Tony Blair na Mheshimiwa Gordon Brown.

Rais Kikwete kesho, Jumatano, Desemba 11, 2013, ataungana na viongozi wenzake katia katika kutoa heshima za mwisho na kuuaga rasmi mwili wa Marehemu Mandela ambao utawekwa kwenye Majengo ya Urais wa Afrika Kusini ya Union Buildings mjini Pretoria.

photo ,

 Wasanii wa Kikundi cha ngoma wakitumbuiza wakati wa Tamasha la mimi ni Afrika,Afrika ni mimi
 Kikundi cha ngoma kikiendelea kutumbuiza


 Mshehereshaji wa Tamasha la mimi ni Afika,Afrika ni mimi Adam mchomvu akiongea na wakazi wa arusha waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja vya general tyre.

 Adam mchomvu akifurahi na wakazi wa arusha
 Wakazi wa Arusha wakinyoosha mikono juu kama ishara ya kupinga rushwa.
 Msaniii chaba akiwaburudisha wakazi wa Arusha
 Msanii chaba na back voclist wake wakiendelea kutawala steji kwenye viwanja vya general tyre
 Nasty Nastyyyy msaniiii chaba akiimbaaaa jukwaaani
 Msanii Joh makini akiwa kwa steji akiwaburudisha wakazi wa Arusha kwenye Tamasha la kupinga Rushwa mimi ni afrika na afrika ni mimi.
 Kundi la weusiiiiii wakikamata steji vilivyo jana kwenye viwanja vya general tyre


 Sema beiiii ya mkaaa,bei ya mkaaaa kundi la weusi wakiwaimbisha wakazi wa arusha kwenye Tamasha la kupinga Rushwa la mimi ni afrika na afrika ni mimi



 Dogo janja akiwa kwa steji akiwarusha mashabiki
 Kundi la jambo Squadwakirukaaa kingarerooooo na mashabiki wao
 Machaliii machaliiiii wa araaaaa hivyo ndio ilikuwa ikisikika wakati jambo squad wakifanya yao jukwaaani.
 Msanii stamina akiwa kwa steji akiwarusha mashabiki

Lile tamasha la kupinga matumizi ya Rushwa na utoaji limefana sana jana Jijini Arusha kwenye viwanja vya general tyre.Kauli mbiu ya tamasha hilo ilikuwa "RUSHWA SIO" na kubebwa na ujumbe mzito wa mimi ni afrika na afrika ni mimi.
Dhumuni kubwa la tamasha hilo ilikuwa ni kutoa elimu kwa wanainchi juu ya madhara ya utoaji na upokeaji rushwa,kiingilio ilikuwa ni bure kabisaaa.Sambamba na elimu iliyotolewa viwanjani hapo pia wakazi wa Jiji la arusha walipata nafasi ya kupata burudani ya kufa mtu kutoka kwa wasanii kama izo b,stamina,weusi,chindo man,roma,fid q,linah,naziz na vanessa mdee.
  PICHA NA HABARI KWA HISANI YA DJ SEK BLOG

photo ,

 Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akipongezwa na Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kwa kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Mbunge, jioni mjini Mbalizi, jijini Mbeya. Viongozi hao wamo kwenye ziara ya kuimarisha chama na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Akizungumzia uteuzi huo, mjini Mbalizi jioni hii,

Dk. Migiro amemshukuru Rais Jakaya Kikwete kwa uteuzi huo ambao ameupokea kwa furaha, na kueleza kuwa kitendo hicho kinadhihirisha jinsi Rais Kikwete alivyo na imani naye pamoja na imani kwa Wanawake wa Tanzania
 Dk. Migiro (kulia), akipongezwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwa uteuzi wake huo.
 Dk. Migiro akizungumza na vyombo vya habari, jinsi alivyopokea kwa furaha uteuzi wake huo.
 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro akimpongeza Dk. Migiro kwa kuteuliwa na Rais Kikwete kuwa Mbunge.

photo ,


Huu ni mtaro ambao umeziba na maji hayaendi,na watu kutupa uchafu ndani yake kama unavyoonekana.
Juu ya huo mtaro kuna mgahawa wa chakula,ambao watu wanautumia kwa mahitaji ya chakula.
Kama picha inavyoonesha maji machafu yakiwa yametuama,na uchafu ukiwa umetupwa ndani yake.
Ikifika mchan watu hukaaa hapo juu na kupata chakula hii ni hatari kwa afya ya binadamu.

Ukifika maeneo ya makumbusho nyuma ya Jengo la Tigo maarufu mtaa wa kwa bwela kwa wauza viatu maarufu kwa wakina dada,hali ya usafi katika mitaro ya eneo hili ni ya kutisha ingawa imezungukwa na maofisi makubwa kama kampuni za simu na mabenki mengi.Dj sek blog ilifanya utafiti makini na kujione hali ya mitaro hiyo ikiwa katika hali mbaya kiusafi,Kwanza mitaro hiyo imeziba hivyo kusababisha maji kutuama na kupelekea maji hayo kuvunda na kuwa rangi ya njano.

Kingine cha kushangaza zaidi ndani ya mitaro hiyo watu hutumia kama sehemu ya kutupia uchafu kama mifuko ya rambo,makopo n,k.Jambo lingine ambalo ni la hatari zaidi ni eneo la juu ya mitaro hiyo kuna mgahawa ambao unauza chakula kwa ajili ya matumizi ya binadamu.Jambo la kujiuliza je watoa huduma katika mgahawa huo hawaoni hali hiyo ya uchafu ambao upo kwenye eneo lao?na je hawaoni kwamba ni hatari kwa afya za binadamu wanaokula eneo hilo?Tulipojaribu kuwauliza walikuwa hawana majibu ya kutoa.Tunaomba serikali ya mtaa wa makumbusho walione hili na kulishughulikia na sio kukaa ofisini mpaka magonjwa yatokee ndipo tuanze kuhangaika.
PICHA NA HABARI KWA HISANI YA DJ SEK BLOG

photo ,

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika PICHA|MAKTABA 
Dar es Salaam.Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo inaanza kikao chake cha siku mbili ikitarajiwa kujadili masuala mazito, hasa misukosuko iliyokikumba katika siku za karibuni.
Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika ilisema kikao hicho kitakachofanyika Dar es Salaam kitapokea, kujadili na kufanya uamuzi wa masuala mbalimbali ikiwamo hali ya siasa na ripoti ya fedha.
“Suala mojawapo litakuwa kujadili mihutasari ya mikutano iliyopita na yatokanayo na mikutano hiyo, taarifa ya hali ya siasa na ripoti ya fedha,” ilisema taarifa hiyo ya Mnyika, ambaye yuko ziara ya kikazi huko Uturuki.
Pia utajadili mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba, taarifa ya utekelezaji wa Programu ya Chadema ni Msingi na shughuli za kanda na taarifa ya utekelezaji wa Mpango Mkakati kuhusu maboresho.
Chadema katika mawimbi makali
Miongoni mwa mambo ambayo yanatarajiwa kujadiliwa katika kikao hicho ni mustakabali wake katika kipindi hiki ambacho kinapita katika mawimbi makali kutokana na kuibuka kwa malumbano ya waziwazi baina ya viongozi wake waandamizi na pia kusimamishwa kwa baadhi ya viongozi wa mikoani.
Matukio ya karibuni yanajumuisha malumbano kati ya Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kuhusiana na masuala ya posho, kusimamishwa kwa Mwenyekiti wa Chadema wa Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba, kuvunjwa kwa uongozi wa Mkoa wa Mara na pia kuondolewa kikaoni kwa Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda.
Wafuatiliaji wa mambo ya siasa watakuwa wanakitazama kikao hiki kama fursa ya kuweka sawa mambo ili kiendelee kutoa ushindani kwa chama tawala.
Alipoulizwa kama matukio ya hivi karibuni yatajadiliwa katika kikao hicho, Mnyika alikataa kuingia kwa undani na badala yake alisema taarifa zitatolewa baada ya kikao.
“Niko nje ya nchi, mengine utapewa majibu kesho (leo) kwa yale ambayo yatakuwepo katika taarifa zitakazowasilishwa. Yale ambayo hayatakuwepo utajulishwa pia iwapo hayatajadiliwa,” alisema Mnyika.
Zitto na Lema
Zitto na Lema waliingia katika vita ya maneno mwanzoni mwa Novemba kuhusiana na masuala ya posho ya vikao.
Vita hiyo ilianzishwa na Lema katika kikao cha wabunge wiki iliyopita aliposema kuwa Zitto anafanya unafiki kukataa posho.
Lema alimtuhumu Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kwamba anakataa posho za vikao bungeni, lakini anapokea posho nyingi kutoka mashirika mbalimbali ya kijamii nchini.
Lema aliweka tuhuma hizo kwenye Mtandao wa Jamii Forum huku akisema suala hilo halihitaji vikao vya chama kulijadili isipokuwa vyombo vya habari na hususan, mitandao ya kijamii kwani hata Zitto hutumia mitandao hiyo.
Akijibu hoja hizo, Zitto alisema tangu siku nyingi alikwisha piga marufuku kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kupokea posho kutoka taasisi au mashirika yanayosimamiwa na kamati hiyo.
Alisema tangu alipokuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma(POAC), alipiga marufuku posho na pia aliwahi kuwashtaki Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) wabunge wanaochukua posho kutoka taasisi za Serikali.
Ripoti kuhusu Zitto mtandaoni
Zitto pia alipata msukosuko mwingine baada ya kusambazwa ripoti inayoitwa ‘Taarifa ya Siri ya Chadema’ iliyomtuhumu kuwa alikuwa anashirikiana na CCM na viongozi wa Idara ya Usalama wa Taifa kuhujumu chama hicho.
Ripoti hiyo inayodaiwa kuwa iliandaliwa na Idara ya Upelelezi ya Chadema, ilieleza kuwa Zitto alikuwa akipokea fedha kutoka kwa maofisa wa usalama na kuzisambaza kwa makada wengine wa chama hicho ili wafanye kazi ya kukihujumu.
Hata hivyo, Chadema kupitia kwa Mnyika ilitoa taarifa kupinga vikali suala hilo.
CAG kukagua ruzuku
Pia, Zitto aliingia katika malumbano na chama chake baada ya kutuhumu vyama vya siasa kuwa hesabu zake hazikaguliwi na CAG.
Chadema ilipinga vikali madai hayo na kueleza kuwa imekuwa inatumia taasisi binafsi kufanya kazi hiyo.
Mwigamba, Shibuda na uongozi Mara
Suala jingine linalotazamiwa kujadiliwa katika kikao hicho ni kusimamishwa kwa Mwigamba na Baraza la Uongozi Kanda ya Kaskazini ambako kulizuka vurugu kiasi cha kunyang’anywa kompyuta mpakato (laptop) baada ya kudaiwa alikuwa anasambaza taarifa za kuhujumu chama hicho.
Suala lake linasubiri uamuzi wa kikao cha Kamati Kuu kama lile la kuvunjwa kwa uongozi wa Chadema wa Mara.
Pia kitendo cha Baraza la Kanda ya Ziwa Mashariki kumtimua Shibuda kwa madai kwamba halina imani naye nacho kina uwezekano mkubwa wa kujadiliwa. Chanzo: MWANANCHI

photo ,



Katika hali ya kuonyesha kwamba wafanyabiashara wa eneo la kariakoo hawataki wala kusikia kuhusu mashine za T.R.A,Wafanyabiashara hao wameamua kufunga mabango katikati ya mitaa yakiwa na ujumbe wa kupinga matumizi ya mashine hizo.
Leo ni siku ya pili kwa wafanyabiashara hao kugoma kufanya biashara,Swali la msingi je Serikali inaonaje hali hii ya wanainchi kukosa huduma?na pia huu ni mkoa wa nne sasa baada ya Mbeya,Morogoro na Mtwara.PICHA NA DJ SEK

photo ,