TANZANIA BILA MAFISADI INAWEZEKANA,PIGA VITA UFISADI HATA KAMA UNAUPENDA.

UTAFITI NA MAIGIZO

Monday, October 5, 2009
Waigizaji wa kundi la MPLC- theatre Group wakiwa kazini kufikisha ujumbe kwa njia ya sanaa shirikishi.Vijana wanafanya kazi kubwa sana katika suala zima la sanaa mkoani Morogoro
Juma Gotagota na Thadey wakisalimiana kwa style mpya wakati wakifanya vitu vyao kwenye jukwaa.


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, October 05, 2009 | Maoni: 0

UTAFITI UMEANZA

Zile safari zangu za kuzunguka huku na kule katika Mji kasoro bahari zimeanza, hii yote ni katika kufanya tafiti za kisheria juu ya haki za wanawake na watoto katika Mkoa wa Morogoro, hapa ni Kipera, kata ya Mlali, wilaya ya Mvomero-Mkoani Morogoro, napumzika kabla ya kuendelea na safari yangu kuelekea Mgeta





Vumbi la eneo hili ni zaidi ya lile la unga wa Siment lakini wenyewe tunainjoy...sijui wewe




 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, October 05, 2009 | Maoni: 2

WAMI DAKAWA

Tuesday, September 29, 2009
Wami Dakawa, kila siku ya ijumaa kunakuwa na mnada wa mbuzi na ng'ombe, eneo hili linakaliwa na kabila la kimasai kwa sehemu kubwa, hapo wachinjaji wanapiga kazi, unahitaji mbuzi kwa bei ya halali?....piga namba hii 0714 523 489, kwa wanaohitaji mbuzi wa ukweli

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, September 29, 2009 | Maoni: 0

MGETA-MOROGORO











 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, September 29, 2009 | Maoni: 0

LADHA YA AKAPELA

SONDA YA DILHU, KIKUNDI CHA MUZIKI WA AKAPELA KUTOKA JIJINI DAR ES SALAAM KIKIWA KATIKA POZI BAADA YA KUTOKA KUONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KATIKA UKUMBI WA IDARA YA HABARI -MAELEZO JIJINI. AKAPELA NI MUZIKI USIOTUMIA VYOMBO AU ALA ZA MUZIKI LAKINI KWA KUTUMIA MDOMO MWIMBAJI ANAWEZA KUTOA SAUTI INAYOFANANA NA ALA YA MUZIKI
KUNDI JINGINE LINALOIMBA MUZIKI WA AKAPELA KUTOKA JIJINI DAR ES SALAAM, KWA TAARIFA YAKO KUNDI HILI NDILO LILILOIMBA KATIKA TANGAZO LA TIGO...DU DU DU DUDU DUDU......AHA.....OH NO...YAP YAP YAP, E BWANA YEE..


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, September 29, 2009 | Maoni: 0

AJARI ZINA KINGA

Monday, September 14, 2009
IMETOKEA MUDA SI MREFU, DALADALA IKIWA IMEGOTA KWENYE GENGE LA MCHANGA BAADA YA KUJARIBU KUIKWEPA PIKIPIKI MAENEO YA STESHENI ROAD MOROGORO, KARIBU NA HOTEL YA KINGTOM NA OASIS


WASAMALIA WEMA WAKIJARIBU KUINYANYUA PIKIPIKI TAYARI KWA KUPELEKWA KITUO KIKUU CHA POLISI. MWENDESHA PIKIPIKI ALIFARIKI MUDA MFUPI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALI YA MKOA YA MOROGORO




KAMA KAWAIDA....WATU WAMEKUSANYIKA KUSHANGAA KILICHOTOKEA...





 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, September 14, 2009 | Maoni: 0

USAFI ZIRO

Tuesday, September 8, 2009
KITUO KIKUU CHA MABASI MSAMBU KINAVYOONEKANA
UCHAFU KILA SEHEMU

LICHA YA JITIHADA ZINAZOFANYWA NA MAMA ZETU KATIKA KUKIWEKA KITUO CHA MSAMVU KATIKA HALI YA USAFI LAKINI ZOEZI HILI LINAONEKANA KUGONGA MWAMBA KUTOKANA NA TABIA ILIYOKITHIRI YA UTUPAJI TAKA OVYO.....


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, September 08, 2009 | Maoni: 0

JESHI LA MTU MMOJA

KWA MBALI WATU WAKIWA WAMEKUSANYIKA KUMUANGALIA MZEE WA MAKOMEDI


KIJANA MMOJA AMBAYE ANAJIITA MZEE WA MAKOMEDI AKIWA AMEWAKUSANYA WATU KATIKA KITUO CHA MABASI MSAMVU KWA AJILI YA KUWAPATIA SHOO KALI.


HAPIGI SHOO MPAKA UDONDOSHE KITU KIDOGO...IKITIMIA SHOO LINAANZA......MJINI SHULE



MWISHO WA SHOO





 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, September 08, 2009 | Maoni: 0

NEW SAVOY HOTEL

Tuesday, September 1, 2009
KWA WANAOTAKA KWENDA MAJUU TU ....PIGA NAMBA HIZO HAPO
MDAU WA BLOG YA WATU 'ELFADHILI' AKIWA AMEPOZI NJE YA OFISI YAKE YA INTANET ILIYOKO KATIKA MAJENGO YA HOTEL YA SAVOY MOROGORO

NEW SAVOY HOTEL


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, September 01, 2009 | Maoni: 0

MIMI NA MTANGAZAJI

Monday, August 3, 2009


BADO NIPO...NAENDELEZA LIBENEKE

MTANGAZAJI WA IDHAA YA KISWAHILI YA RADIO YA WAADVENTISTA ULIMWENGUNI " MADUHU EMANUEL" AKIWA KATIKA STUDIO AKIREKEBISHA BLOG YAKE www.mtangazaji.blogspot.com, unaweza kumcheki hapo

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, August 03, 2009 | Maoni: 0

MTANGAZAJI NAPOKUWA MZIGONI


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, August 03, 2009 | Maoni: 0

MIUNDOMBINU

Tuesday, July 14, 2009




SHIRIKA LA RELI TANZANIA -MOROGORO SIDHANI KAMA WAMESHACHUKUA TAHADHARI DHIDI YA MAAFA YANAYOTARAJIWA KUTOKEA KATIKA ENEO HILI.

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, July 14, 2009 | Maoni: 0

MAPINDUZI YA KWELI HUANZIA KICHWANI

Monday, June 29, 2009
WANANCHI NI WAONGO VIONGOZI WAKWELI WATOKE WAPI?

Na Abdallah Mtibora

Ni rahisi sana kuelezea uongo kuliko kusema uongo ni nini. Wengine wanasema, Uongo ni kinyume cha ukweli, wengine wanasema uongo ni ile hali ya kusema ama kutenda kinyume na linalo takiwa kusemwa au kutendwa. Mimi nasema uongo ni hali ya kusema jambo lisilo la ukweli, kuahidi jambo ambalo halikutekelezwa kama lilivyo ahidiwa, au kutenda kinyume na makubaliano iwe ki maandishi, maneno au kisheria hivyo kwa mujibu wa maana yangu ya uongo, kutotimiza wajibu ni uongo (Niko tayari kusahihishwa, kwenye jitihada zangu za kupanua maana ya neno Uongo), ingawa si lengo la makala haya kujadili maana ya neno uongo.

Nasukumwa na dhamira ya mijadala mbalimbali kuhusiana na namna wanasiasa wanavyoshambuliana kuhusu uongo, sitajadili nani ni mkweli, ama nani ni muongo kwa maana naamini kila mmoja ana nafasi yake kuhusiana na suala la uongo.

Kuelekea uchaguzi Mkuu mambo mengi yatajitokeza,na mengine yameshaanza kujitokeza. Wanasiasa wenyewe kwa wenyewe watatuhumiana,kadhalika wananchi wataendelea kuwatuhumu wanasiasa kwa hadaa zao, na ahadi zisizotekelezeka.

Natambua uongo ni jambo ovu, hakuna dini yeyote inayoruhusu udanganyifu, lakini kadiri dunia inavyozidi kuzunguka ndivyo uongo unavyozidi kushamiri na unaelekea kurasimishwa siku zijazo, kama haujarasimishwa.

Nitatoa mifanomichache kuonesha ni kwa nini uwezekano wa kuondoa hadaa za kisiasa itatuchukua miongo kadhaa ikiwa uongo unaoonekana ni “mdogo” usipodhibitiwa kalaaniwa na kubezwa.

Mathalani mzazi ambaye ili mwanaye mdogo asilie wakati atakapo ondoka kwenda kwenye shughuli nyingine ziwe za kijamii au kiuchumi anavyomdanganya malaika wake. Tumekuwa tukisikia ama mama akisema ‘narudi sasa hivi’!, au usilie nitakuletea pipi. Lakini kinyume chake, pindi mama anaporejea aidha anakuwa amekawia kurudi, kinyume na ahadi yake au anarejea bila ile zawadi aliyo ahidi kwa mwanae (pipi)

Matukio ya kudanganywa kwenye ngazi ya familia yanaendelea kila uchao, mara mtoto aahidiwe nguo ya sikukuu, lakini ikifika siku ya siku anapewa visingizio lukuki, sasa najiuliza mtoto wa aina hii atauchukuliaje uongo. Je atauchukulia kama sehemu ya kutuliza maumivu ya mlalamikaji kama wafanyavyo baadhi ya wanasiasa wetu au atauchukulia kama uovu?, na je mzazi anaye mdanganya mwanaye ana “moral justification” ya kumchukia ama kumsema mwanasiasa aliyetoa ahadi ya uongo?.

Mfano mwingine ni wa mfanyibiashara anaye kwepa kulipa kodi, anatumia udhaifu wa mfumo wetu wa ulipaji wa kodi pamwe na udhaifu wa baadhi ya wakusanya kodi kukwepa kulipa kodi. Watu hawa ni maadui wa maendeleo ya nchi hii, ni maadui wa elimu ya nchi hii, ni maadui wa maendeleo ya kilimo chetu, ni maadui wa maendeleo ya kila sekta hapa nchini. Mfanyibiashara anaye toa takwimu za uongo ili alipe kodi kidogo anasema uongo, lakini inapotokea pengine kuna ahadi ya serikali kuhusu jambo lolote ambalo anafaidika nalo, na serikali ikachelewa kulitimiza, muongo huyu atakuwa wa kwanza kuinua kidole chake kumnyooshea muongo mwenzake ‘serikali’.

Mtu wa aina hii hawezi kukemea au kudai utekelezwaji wa ahadi ya serikali wakati yeye mwenyewe dhamira ya kutotimiza ahadi yake (kulipa kodi stahili) ingali inamsuta.

Tazama kiongozi wa taasisi ya kidini, ambaye Serkali yake inamsamehe kodi ili aweze kuihudumia jamii, lakini yeye anadanganya kwamba anatumia msamaha huo kwa lengo lililokusudiwa kumbe anautumia kwa mambo yake binafsi, mwisho wa siku serikali inapoteza asilimia 30 ya mapato yake, kwa vile serikali huongozwa kwa kodi, serikali inaposhindwa kutimiza wajibu wake kwa wananchi wale waongo waliotumia msamaha wa kodi visivyo, watakuja juu kuwalaumu waongo wenzao (serikali) kwamba inawadanganya.

Kadhalika, unaweza kuangalia uongo mwingine pale ambapo mkulima anapodanganya kwamba bidhaa zake ni nzuri kumbe katikati amejaza bidhaa mbovu, huu ni uongo, wanunuzi wa bidhaa za barabarani kama vitunguu, nyanya na viazi kwenye barabara itokayo Iringa, Dodoma, Morogoro na ile iendayo Arusha kutokea Dar watakuwa wanaelewa udanganyifu huo. Waongo hao, pia wanasimama kidete kuwalaumu waongo wenzao (Serikali) pale ahadi fulani fulani zinapokuwa hazijatekelezwa, inachekesha sana.

Kwa kweli uongo umetamalaki kila sekta, hebu fikiria chombo cha habari kinajiita chombo huru, lakini kuna baadhi ya watu ambao aidha ni washindani wa kibiashara wa mmiliki wa chombo hicho, au wanatofautiana ki itikadi, habari zao ambazo ni nzuri na za kimaendeleohaziwezi kutolewa kwenye chombo hicho, chombo kama hicho kinacho endelea kujinadi ati ni chombo huru, kinawadanganya wananchi. Sasa chombo hiki, ambacho kinawadanganya watu kwa jambo dogo kama hilo, kinaweza kusimamia ukweli?.

Ama tazama mfano wa muhadhiri wa chuo kikuu anayefundisha kwamba kilimo kinaweza kumuondoa mtanzania kutoka kwenye lindi la ufukara, lakini yeye anafungua mradi wa baa (bar) muhadhiri huyu sio muongo kweli?, ama muhadhiri wa sheria anayefundisha haki za binadamu, wakati yeye mwenyewe anazivunja kwa wanafunzi wake, ni neno gani linafaa kwa huyu muhadhir?, mnafiki au muongo?,na vipi kuhusu muhadhiri anayefundisha umuhimu wa viwanda vidogo vidogo, wakati yeye mwenyewe hayuko tayari kuanzisha kiwanda hata kimoja, achia mbali kuhamasisha wananchi wa eneo anapoishi kulingana na maana yangu ya uongo, mtu huyo ni muongo maana anatuambia kwamba jambo fulani ni jema, lakini yeye haliendei jambo hilo, jina analofaa kuitwa ni muongo, maana anasema jambo ambalo yeye mwenyewe haliamini.

Au chukulia afisa wa serikali ambaye amepewa dhamana ya kuwahudumia wananchi, anakula kiapo kuwatumikia wananchi bila upendeleo, choyo ama huba, lakini hatimizi ahadi yake, mtumishi wa aina hii anapocheleweshewa stahili zake anasimama imara kulaumu serikali kwa kutoa ahadi hewa, bila kukumbuka au kwa kujifanya hakumbuki uongo wake wakati wa utumishi wake.

Unaweza kuchukulia mfano wa baadhi ya waalimu wetu wa shule za serikali,ni kweli wanafanya kazi kwenye mazingira magumu, lakini nao wamekuwa hawatimizi wajibu wao ipasavyo, kwa kushindwa kutimiza wajibu wao na kudai stahili za kazi ambayo imefanywa chini ya kiwango nauchukulia kama ni udanganyifu, hivyo hata watetezi wa haki za walimu wakati mwingine wanashindwa kutetea uozo huo.

Mfano mwingine ni wa mwanafunzi aliyefaulu kwa njia za udanganyifu, aidha kwa kutumia udhaifu wa taasisi zetu za mitihani, ama kwa kununuliwa na shule yake, ili shule ipate umaarufu, mwanafunzi huyoni mungo kwani daraja alilopata si daraja lake stahiki, hata kama angeweza kulipata bila ya udanganyifu. Mtoto huyu ni muongo, tunatengeneza msomi muongo, ili aje akemee ukweli au abariki uongo?, na je atamnyima mwanaye pesa ili akanunue mtihani?, na je baada ya hapo atampongeza kwa kufaulu au kwa kuweza kudanganya bila kugundulika?.

Mfano mwingine wa uongo wa rejareja kwenye jamii yetu ni pale ambapo kondakta wa daladala anapowadanganya abiria wawahi viti kwenye gari ambalo limejaa, kondakta huyo ni muongo kama kiongozi ambaye anayewaahidi wananchi ujenzi wa barabara, il hali barabara zinajengwa kutokana na vipaumbele (Sina uhakika kama bado vipaumbele vinazingatiwa).

Ama chukulia mfano wa msaidizi wa ndani (House girl), ambaye muajiri wake (Sina uhakika kama wanaajiriwa) hamruhusu kupumzika ama kwenda kusalimia ndugu zake, ili aende kuwasalimia ndugu zake, inabidi ama adanganye kwamba anaumwa, au amefiwa, ni dharura hizo tu ndio zinazoweza kumtoa kwenye ngwamba ya kazi za ndani. Akisema ukweli haruhusiwi kabisa, ama msaidizi huyo inapotokea akavunja kikombe cha “muajiri” wake hawezi kuwa na utetezi wowote zaidi ya kutafuta uongo maridhawa ili “mshahara” wake uskatwe. Ni hivyo hivyo kwa mlinzi, dereva, ‘shamba boy’ na mlisha ngo’mbe.

Orodha ya uongo unaofanywa nchini kwa viwango tofauti tofauti ni ndefu, mathalani chukulia na wengi ni mashahidi kwenye magari ya abiria maarufu kama daladala mtu anatakiwa kwenye kikao cha kifamilia Gongo la mboto, yeye yuko Mbezi mwisho akipigiwa simu na wanandugu ili kujua alipofikia hawezi kuwaambia kwamba yuko Mbezi mwisho, baadala yake atasema yuko Tazara, ama Buguruni, pengine ili kuwapamoyo ndugu zake ya kwamba yuko karibu kufika kama ambavyo alikuwa akidanganywa angeletewa pipi ama aandazi ili asilie pindi mama yake alipokuwa akiondoka.

Mara nyingi tumekuwa mashuhuda juu ya uongo unaofanana na huo wa mkazi wa Mbezi mwisho, kuonesha kwamba uongo unakaribia kurasmishwa, abiria wamekuwa wakiishia kutabasamu ama kucheka tu. Hili limeendelea kuwa Taifa la wasema uongo kila idara, kila rika na kwenye kila taasisi, na viongozi wa dini wamekaa kimya wakisubiri serikali “iwadanganye” itafuta msamaha wa kodi kwa bidaa wanazoingiza, nao “waidanganye” serikali ati wataandamana hadi Ikulu kama msamaha huo utafutwa.

Hivi waziri anayemjibu mbunge mwenye hasira juu ya barabara ya jimboni kwake itajengwe lini, kwamba itazingatiwa kwenye bajeti ya mwakani ili ampunguze hasira na kumpa moyo mbunge huyo, anatofauti gani na mama aliyemdanganya mtoto ili asilie?, mkaazi wa mbezi ambaye anadanganya yuko tazara wakati angali anaoga ili awape moyo ndugu zake waendelee kumsubiri?. Ukitaka kujua jinsi uongounavyoelekea kurasimishwa, au umesharasimishwa kimyakimya jaribu kufikiria kama mheshimiwa waziri angejibu kwamba Serikali haina mpango wa kujenga barabara husika kwa miaka ya karibuni, au yule ndugu aliyeko Mbezi awaambie ndugu zake kwamba ndo kwanza anaoga, au msichana ambaye huna mpango wa kumuoa na uko naye kimapenzi utakapomwambia ukweli juu ya nia yako hiyo. Utagundua kwamba, jamii yetu inapenda lau idanganywe lakini iahidiwe kitu, hata kama hakitekelezeki.

Kwa baadhi ya mifano hiyo, na mingine ambayo wewe unayo, inashangaza kuona wanaobariki uongo wanaendelea kushangaa, wanapoambiwa uongo na waongo wenzao, hivi kama jamii yote ni ya wafugaji inakuwaje tushangae kuwa na kiongozi ambaye ni mfugaji?

Kwa vile uongo hauwezi kuendelea kuwa utamaduni wetu, na kwa kuwa uongo haupendezi hata mbele ya Macho ya Mungu (Kwa wanao amini uwepo wake), sisi kama jamii, bado hatujachelewa, tubadilike, tujifunze kusema ukweli hata kama ukweli huo ni mchungu, na jitihada hizo, zianzie ngazi ya familia, kwa kumwambia mtoto “nakwenda msibani nitachelewa kurudi usilie mtoto”, au kumwambia msichana uliyemtamani“ nina mihemko tu ya kimwili, na si kwamba nakupenda”, au waziri wa miundo mbinu anaweza kujibu “barabara flani haiwezi kujengwa mwaka huu au mwaka kesho, kwa vile barabara hiyo haina tija kiuchumi”, au ndugu wa jambazi aliyeuawa kwenye risala waseme “ndugu yetu kabla hajauawa tulikuwa tunaushuku utajiri wake” na kama kiongozi mbadhirifu akifariki, kwenye salamu za rambirambi tuseme “marehemu pamoja na sifa zote, pia alikuwa mbadhirifu, mjivuni, muongo na ngoni”.

.Tukifika hapo tutakuwa na sababu ya msingi ya kuwabeza viongozi waongo maana watakuwa sio sehemu ya jamii yetu, lakini kwa mwendo huu tulionao tunapowalaumu viongozi waongo wenzetu, labda tunataka viongozi wetu wadondoshwe na Mungu toka juu mbinguni.

Sisemi kwamba tusikemee uongo, lakini najiuliza hao waongo wametokea wapi?,je sio sehemu ya jamii yetu?, sisi tumesema uongo mara ngapi?, au tunapima uongo kwa mizania gani?, au tunaona kibanzi kwenye macho ya wenzetu ili hali nasi tuna boriti?. Waongo hawaepukiki, likini basi waongo wawe wachache wakweli wawe wengi, lakini bila hata ya utafiti,ni dhahiri jamii yetu imejaa waongo wengi na wakweli wachache, tubadilike, viongozi wa dini wakumbuke jukumu lao, wazazi pia na jamii nzima, vinginevyo hakuna anayestahili kukemea uongo, maana wakati mbunge anamlaumu waziri kwa kutowajibika na kudanganya, mbunge huyo huyo hajawajibika na amewadanganya wapiga kura wake jimboni, na waliodanganywa jimboni, pia wamezidanganya familia na hawawajibiki kwazo, na mzumguko unakwenda hivyo hivyo.

Tukemee sasa au tukae kimya milele, tuseme kweli maana kweli itatuweka huru.

Muandishi wa Makala hii Abdallah Mtibora ni mwanafunzi wa shule ya sheria “law school” anapatikana kwa simu namba 0717 - 714 728, e mail mtibora@hotmail.com
 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, June 29, 2009 | Maoni: 0

MDAU

Monday, June 22, 2009
MMOJA WA WADAU WA KARIBU WA BLOG HII AKIWA KATIKA POZI

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, June 22, 2009 | Maoni: 0

RAHA YA KAMERA


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, June 22, 2009 | Maoni: 0

RAHA YA KAMERA


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, June 22, 2009 | Maoni: 0

SWALA ZIMA HALIKUKOSEKANA


KWENYE MATUKIO KAMA YA WARSHA VITU KAMA HIVI HUWA NI KAWAIDA SANA...

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, June 22, 2009 | Maoni: 0

WAANDISHI UTAWAJUA TU

DOTO KAHINDI (MWENYE SHATI JEUPE) AKIPATA MAELEZO KUTOKA KWA AFISA MAENDELEO YA JAMII WA WILAYA YA MVOMERO MARA BAADA YA KUMALIZIKA KWA WARSHA KUHUSU HAKI YA MWANAMKE KUMILIKI ARDHI ILIYOKUWA ILIYOFANYIKA KATIKA KUMBI ZA HOTELI YA NEW SAVOY MJINI MOROGORO. DOTTO KAHINDI NI MWANDISHI WA HABARI NA MTANGAZAJI WA RADIO UKWELI FM ILIYOKO MJI KASORO BAHARI.
MZEE LIBENANGA AMBAYE NI MWANDISHI MKONGWE AKIONGEA NA AFISA MAENDELEO YA JAMII WA WILAYA YA MVOMERO MARA BAADA YA KUMALIZIKA KWA WARSHA HIYO YA SIKU TATU


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, June 22, 2009 | Maoni: 0

MJI KASORO BAHARI







NIAMBIE.......MAENEO GANI HAYA



 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, June 22, 2009 | Maoni: 4

MITAA YA STESHENI YA TAZARA

Wednesday, June 17, 2009















 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Wednesday, June 17, 2009 | Maoni: 1

KA-ROUND ABOUT KARIBU NA POSTA-MORO


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Wednesday, June 17, 2009 | Maoni: 0

BADO NIPO MOSHI

Monday, May 25, 2009














 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, May 25, 2009 | Maoni: 0

NIPO MOSHI

BAADHI YA WANAFUNZI WA CHUO CHA USHIRIKA MOSHI WAKIJADILI KUHUSU KALE KA-TESTI MARA BAADA YA KUTOKA KATIKA CHUMBA CHA MTIHANI-NYERERE HALL.



 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, May 25, 2009 | Maoni: 0

SAFARI IMEFIKA UKINGONI

Saturday, April 25, 2009
JUST A PAUSE AFTER A LONG WALK TO PASTORALISTS....

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Saturday, April 25, 2009 | Maoni: 0

LAIGWENANI

Friday, April 17, 2009











UMENIONA?



 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, April 17, 2009 | Maoni: 0

SAFARI YANGU BADO INAENDELEA

BADO NIPO UMASAINI NIKIENDELEZA LIBENEKE...KUNG'ATA KAMA KAWA
NATOA MAFUNZO KWA JAMII YA.....................................


MAMBO YETU YALEE.......




HAPA NIMESIMAMA NA KIONGOZI WA KIMILA WA KABILA LA KIMASAI "LAIGWENANI" HUKO NYAKONGE-KIBATI WILAYA YA MVOMERO




 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, April 17, 2009 | Maoni: 0

FULL.................

Friday, March 27, 2009




 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, March 27, 2009 | Maoni: 0

LIBENEKE LINAENDELEA

VIATU VYA KWETU
CHAGUA MWENYEWE




HAUNIONI



 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, March 27, 2009 | Maoni: 0

BAADA YA MSOSI


BAADA YA NYAMA..... NIMEINGIA DARASANI KUWAPIGA DARASA WATOTO WA JAMII YA KIFUGAJI KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA MTOTO...NIMEKUPA MGONGO...UMENIONA?
MWANASHERIA NI MWALIMU...CHUKUA HIYO

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, March 27, 2009 | Maoni: 0

NIPO UMASAINI-NYAMA FULL KUJIACHIA

Nipo maeneo ya wafugaji nikiendeleza libeneke, huko hakuna mtandao wala network....hapa nikijiandaa kwa menyu ya mchana katika kijiji cha Mangae-Mnadani, eneo maarufu kwa shighuli za minada ya ng'ombe na mbuzi......nyama full kujiachia
BADO KIDOOGO...NITAKUKARIBISHA

NGOJA NIKUCHAGULIE NYAMA NZURI.... UNATAKA PAJA AU MGUU?


HII NDIO NZURI.......


KARIBU ZINAIVA......SIDAI NALENG (NZURI SANA).




 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, March 27, 2009 | Maoni: 0

KIJIJINI HAKUNA MTANDAO







 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, March 27, 2009 | Maoni: 0

REHEMA MWAKANGALE HATUNAYE TENA

Tuesday, March 3, 2009
Aliyekuwa mtangazaji wa ITV na Radio One Rehema Mwakangale (Aliyeshika kipaza sauti) enzi za uhai wake akiwa katika kuendeleza libeneke kwenye pita pita ya kukusanya maoni ya kipima joto kama anavyoonekana katika picha hiyo hapo juu.
Mungu ailaze roho yake mahali pema.

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, March 03, 2009 | Maoni: 0

HAURUHUSIWI KUCHEKA WALA KUTABASAM

Sunday, January 25, 2009
UMEINOTI NOTISI HIYO?
HURUHUSIWI KUWEKA ALAMA YOYOTE ILE...

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Sunday, January 25, 2009 | Maoni: 0

NAMFANANISHA NA................

SIJUI NANI?...............UTANI MWINGINE HAUCHEKESHI KABISA..........

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Sunday, January 25, 2009 | Maoni: 0

MSAADA KWENYE TUTA...

ALAMA HIZI ZINAMAANISHA NINI?
 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Sunday, January 25, 2009 | Maoni: 0

NIPO MJI KASORO BAHARI

NIPO MJI KASORO BAHARI WADAU WANGU NIKIENDELEZA LIBENEKE KWA MUDA TU....KISHA NITAREJEA KULE NILIKOTOKA....NADHANI UNAPAJUA.............JENGO HILI HUTUMIWA KAMA OFISI YA CCM WILAYA YA MOROGORO VIJIJINI, JENGO HILI LIKO MKABALA NA OFISI ZA MANISPAA YA MOROGORO...KAMA UNAELEKEA STESHENI VILE.....LINAPENDEZA SANA....HALIITAJI UKARABATI KABISAAAA

OFISI YA POSTA............SIJUI PANAITWAJE? LAKINI ZIPO KARIBU NA MAKTABA YA MKOA WA MOROGORO, OFISI YA MKUU WA WILAYA YA MOROGORO MJINI NA INATAZAMANA NA BENKI YA NBC......WENYEJI NISAIDIENI....PANAITWAJE VILE?


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Sunday, January 25, 2009 | Maoni: 2

NI MOROGORO




 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Sunday, January 25, 2009 | Maoni: 0

GENERAL NKUNDA

Saturday, January 24, 2009
 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Saturday, January 24, 2009 | Maoni: 1

UJANJA WOOOTE...KUSUMBUA KOOOTE


AMEISHIA MIKONONI MWA MIKONO YA WABABE WENZAKE...JAMAA AMEDAKWA NA SASA YUKO CHINI YA ULINZI MKALI HUKO RWANDA....ANATAMANI KURUMSITUNI BUT ITS TOO LATE...AMECHELEWA...PRESHA INAPANDA.......PRESHA INASHUKA....ANAHEMA KAMA ..........................

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Saturday, January 24, 2009 | Maoni: 1

MACHO HAYASHIBI KUONA

Friday, January 16, 2009




UKIKUTANA NA KITU KAMA HICHO HAPO KWENYE PICHA KIKIWA KIMESIMAMISHWA KWENYE CHOCHORO ZETU ZA USWAZI KWA HARAKA HARAKA UTAFIKIRIA NINI?UTACHUKUA HATUA GANI?....KUWA MUWAZI





 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, January 16, 2009 | Maoni: 2

MZUKA UNAPOPANDA

Sunday, November 23, 2008

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Sunday, November 23, 2008 | Maoni: 2

NIMERUDI WADAU WANGU

Nependa kuitumia nafasi hii kuwakaribisha tena wadau wote wa Blog Hii maridhawa kuwa nimerudi upya baada ya kuwa kimya kidooogo kutokana na kutingwa na kesi za EPA na majukumu mengine ya kisheria.

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Sunday, November 23, 2008 | Maoni: 2

MUOGO WA NANENANE

Thursday, August 7, 2008

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Thursday, August 07, 2008 | Maoni: 1

MJI KASORO BAHARI

Tuesday, August 5, 2008
Kwa mbaaaaali safu za milima ya uluguru ikikuita kukukaribisha Morogoro "Mji Kasoro Bahari" ingawa wenyeji huliita Bwawa la Mindu "Bahari ya Morogoro". Nipo Mkoani Kidogo nikipumzisha akili baada ya mapigano makali ndani ya Bahari ya sheria pale Mzumbe.

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, August 05, 2008 | Maoni: 0

MAMBO YA UGHAIBUNI

Monday, August 4, 2008


BONGO DJ's ENTERTAINMENT WANAKULETEA BBQ SUMMER BASH,IKISHIRIKIANA NA WANAMUZIKI MAHIRI WA KIKE KUTOKA KENYA AKIWEMO MWANADAFADA KAREN "KAZ".
KAENI MKAO WA KULA
 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Monday, August 04, 2008 | Maoni: 0

MISS TANZANIA - 2008

Sunday, August 3, 2008

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Sunday, August 03, 2008 | Maoni: 0

NINI MAANA YA MAISHA?

Tuesday, July 29, 2008

WAKATI WENGINE WAKIWAZA KUBADILISHA AINA MPYA YA KIATU, AKINA MIMI NA WALE BADO TUNA AINA ILEILE

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, July 29, 2008 | Maoni: 0

FAIDA YA POMBE

Tuesday, July 8, 2008


 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, July 08, 2008 | Maoni: 1

USTAARABU ULIOSTAARABIKA

Tuesday, June 17, 2008
Magari yakiwa yamesimama na kusababisha foleni ili kuwasubiri Bata na watoto wake wavuke barabara.Huu ni ustaarabu wa hali ya juu katika kuheshima hali za wanyama

 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Tuesday, June 17, 2008 | Maoni: 2

MWAKYEMBE...MWAKYEMBE...MWAKYEMBE

Friday, June 13, 2008
Wabongo kama kawaida yao walikuwa wamezusha kifo cha Dr Harrison Mwakyembe mbunge wa Kyela baada ya masahibu ya jana Bungeni lakini imejitokeza kuwa habari hizo si za kweli na yeye yuko salama Salmini mjini Dodoma. hata hospitali ameshatoka!!
Habari za kuenea kwa Kifo cha Mheshimiwa Mwakyembe zimesambaa kama umeme huku baadhi ya wadau mbalimbali wa blogu hii wakijaribu kutafuta ukweli juu ya tukio hilo ambalo watanzania waliowengi walishaanza kusikitika.
Nae Mzee wa Sumo [ Mpoki Bukuku] amelipoti:
MBUNGE wa Kyela (CCM), Dk Harrison Mwakyembe ameugua ghafla akiwa bungeni na kukimbizwa hospitali.Dk Mwakyembe ambaye aliongoza Kamati ya Bunge ya Kuchunguza Mchakato waUshindi wa Kuzalisha Umeme wa Dharura kwa Kampuni ya Richmond Development,aliingia bungeni jana akiwa na afya njema, lakini hali ilibadilika ghafla na kutaka kuanguka.Aliingia bungeni majira ya saa 2:00 asubuhi akiwa na afya njema, lakini ilipotimu saa 3:30 asubuhi alianza kujisikia vibaya, huku akitaka kudondoka chini.Hata hivyo, Mbunge wa Lupa(CCM), Victor Mwambalaswa alibaini hali hiyo nakumuondoa bungeni pole pole akiwa amemshikilia na kumtoa nje ya Ukumbi waBunge.Baada ya kumfikisha nje, Mwambalaswa aliita gari la kubeba wagonjwa nakumkimbiza kwenye kliniki iliyopo majengo ya Bunge ambako alipata hudumaya kwanza, lakini baadaye alihamishiwa sehemu ambako haijulikani.
 
© Amani Mwaipaja Tarehe: Friday, June 13, 2008 | Maoni: 0
Idadi ya watu