Mh Amina chifupa akiapa mbele ya Bunge.....nimeipenda picha hii, wewe je?

photo ,

Nani alaumiwe kwa hili?



Picha hii nimetumiwa na mdau kutoka jijini Arusha...ni kama anasikia raha eh?


Wanakijiji nikumbusheni...mnyama huyu huwakilisha nnini kwenye hela yetu?
Unaweza kupagundua mahali hapa? hivi watu wa mipango miji wanajua madhara ya kuruhusu ujenzi wa namna hii?ebu wadau wasilisheni hoja maana kila nikikumbuka kile kilichotokea katika soko la mwanjerwa moyo wangu huruka kichurachura



Aliyekuwa Rais wa Benki ya Dunia akitafakari jambo......


Usipomjua huyu wewe si Mtanganyika....anaitwa nani vile?


Wapi hapa?


Hili ndilo kundi la Acappella kutoka Africa ya kusini lijulikanalo kama Ladysmith black Mambazo.Kundi hili linaimba muziki wa asili bila kutumia vyombo vya muziki yaani akapela na lilianzishwa mwaka 1964 na kiongozi wa kundi hilo - wa kwanza kutoka kushoto mstari wa mbele ambaye anaitwa Joseph shabalala.
Kundi hili ni moja ya vikundi maarufu duniani vinavyoimba muziki wa acappella kutoka Africa na kwa taarifa yako limesafiri na kushirikishwa na waimbaji mbalimbali maarufu duniani. Sauti za kundi hili ndizo zinazosikika katika ile picha ya Eddie Murphy iliyotokewa kupendwa sana ya COMING TO AMERICA.kama hujawahi kuitazama nenda kaikandamize sasa hivi.
Jamaa hawa wako mbioni kuja nchini Tanzania kwa udhamini wa Nyanza Company Limited


Hii imekaaje?
Mwanamke wa shoka...unamkumbuka huyu?.....hata kama humkumbuki lakini amini kuwa siku hazigandi


Hii ndiyo njia inayoelekea kituo cha watoto yatima Simike jijini Mbeya.......Kituo cha Simike kimeanzishwa miaka 17 iliyopita, wadau naomba niwapeleke moja kwa moja mkajionee wenyewe mandhari ya huko ili tusaidiane kwa pamoja katika kuwasaidia hawa wadogo zetu.
Safari yangu kuelekea kinjia hiko juu ilianzia hapa


Mtoto huyu umuoneaye hapo alipo hasikii, haoni na wala haongei.
Ni mmoja wa watoto yatima wanaolelewa na kituo cha Simike jiji Mbeya.



Mtoto huyu anayejulikana kwa jina la Amani ni mmoja kati ya watoto yatima wanaolelewa na kituo cha watoto yatima cha Simike...Mtoto huyu alipelekwa kituoni hapo akiwa na umri wa wiki moja baada ya mama yake aliyemzaa kumtelekeza katika hospitali ya wazazi ya Meta.Hapa alikuwa akiwaimbisha wenzake.
Watoto hawa wanahitaji msaada wako, hata kuwatembelea na kuwajulia hali na kuongea nao ni sehemu mojawapo ya kuwapatia faraja


Mazingira ya ndani.....mbele ya hilo pipa kwa upande wa kulia ndipo kilipo chumba hiki hapa chini


Chumba hiki hutumiwa kama sebule na darasa kwa watoto wa kituo cha Yatima Simike


Wema Sepetu? !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Wadau toeni maoni juu ya hili......mimi naona haikubaliki totally


Ni vitu vya kawaida ukiwa ughaibuni kutinga makoti kama haya....nimepozi na Frank Zacharia..Mkurugenzi wa Nyanza Company Limited



Ukiingia tu ndani ya geti la Hospitali ya wazazi Meta karibu na jengo la damu utakaribishwa na ujumbe huu


Wabongo wengi wamekuwa na kasumba ya kuogopa kutoa damu...hivi tatizo ni nini?ukosefu wa elimu au?Michuzi unasemaje?kama huogopi njoo


Afande Sele akiwa katika pozi ndani ya gari lililokuwa likitumiwa na tour ya wanaume halisi na ndege tunduni...jamaa anatisha sana katika utunzi wa mashairi yaliyokwenda shule....Kitururu unamzungumziaje mshikaji huyu?...toa hoja



Hawa ni moja ya wadau wangu wa blog hii ambao nao wanakandamiza digrii ya sheria ughaibuni....jamaa anaitwa Keny ambaye pia ni mtunzi mashuhuri wa mashairi ya kidhungu...huyo mdada aliyenaye ndiye my nanii wake


Ikulu inavyoonekana kwa mbele. Soma historia yake fupi hapa chini

Ikulu ya tanzania ndiyo ofisi kuu ya Rais wa jamhuri ya tanzania ambapo ilianza kutumika kama ofisi ya Rais wa Tanzania mwaka 1962.


Jengo hili la Ikulu lilijengwa kwa mara ya kwanza mwaka 1919 na Gavana wa kwanza wa kijerumani ndugu Horrace Byatt. Baada ya gavana huyu kuingia madarakani alilazimika kukaa katika makazi ya muda yaliyoko karibu na Ikulu ya sasa ambayo makazi hayo yanatumika kama ofisi za wizara ya Afya.


Ujenzi huo ulikuja kukamilika mwaka 1922 huku baadhi ya nakshi za jengo hilo zikiwa zimewekwa na ndugu J. H Sinclair - Mtaalam wa majengo wakati wa ukoloni.


Mapambo mengine katika jengio hilo yalikuja kuongezeka baada ya uhuru ambapo mataifa mbalimbali yaliyotoa zawadi kama sehemu ya furaha yao katika kusherehekea uhuru wa tanzania.





Hili ndilo Fuvu la chief wa wahehe....MKWAWA likiwa katika sehemu ya makumbusho huko Kalenga-Iringa.Fuvu hili lilirudishwa nchini Tanzania (Tanganyika kwa wakati huo) na serikali ya kijerumani mwaka 1954 kwa kuzingatia mkataba wa versaile mwaka 1919 ulioitaka serikali ya kijerumani kulirudisha fuvu hilo.
Chief Mkwawa inasemekana alizaliwa kati ya mwaka 1855 -1898 akiwa mtoto wa Mwinyigumba aliyefariki mwaka 1879


Hiki ndicho kivuko cha Ferry jijini Dar es salaam


Teddy Sodoyeka akitabasam baada ya kugundua kuwa kamera ya kutoka duniani ipo sambamba na uwepo wake...mdada anakamua Digrii ya sheria Ughaibuni


Wadau wa Blog hii wakiwa katika nyuso za furaha.....kutoka kulia ni Teddy Sodoyeka, Neema Haki na rafiki yao kipenzi anayefanya makamuzi pale Hope Univeristy

Uspime



Mshikaji akiwa katika pozi...maeneo ya arusha nilipotembelea hivi karibuni.


Yale matokeo ya kidato cha sita yaliyokuwa yakisubiriwa kwa hamu kubwa na watahiniwa wa mtihani huo yameshatoka huku shule nyingi zikiwa zimefanya vibaya uklinganisha na miaka iliyopita. Kiwango cha kufaulu kwa mujibu wa baraza la mitihani la taifa kimepungua kwa asilimia sita ukilinganisha na mwaka jana.
Matokeo hayo hivi saa yanapatikana live bila chenga kupitia mtandao wa
www.moe.go.tz
Bofya hapo kuangalia matokeo


Kwa wale wasioifahamu vizuri sura halisi ya Idd enzi za uhai wake
Jamaa alijitwika mavyeo kibao....




Utamaduni huu hatuwezi kuuiga....kwa habari zaidi bofya hapa www.saharanvibe.blogspot.com


Huyu ndiye Miss Tanzania wa kwanza kabisa ambaye kaka michuzi ametupatia taarifa za hivi karibuni kuwa hatuko naye tena duniani....alikuwa akijulikana kwa jina la mama theresa. kwa habari zaidi bofya hapa

Sio siri...habari hizi zimenishtua sana...asanate sana kaka michuzi kwa taarifa hii muhimu


Mwinjilisti wa kimataifa Amon Mkangara..kwa habari zake zaidi hebu bofya hapa.


Hawa ni moja kati ya watoto wengi waliotoka kufanyiwa.....kwa habari zaidi bofya hapa www.saharanvibe


Hili ni ziwa masoko..ni moja kati ya maziwa machache yenye maajabu na historia ya pekee kama ile ya Ziwa kisiba....watu mbalimbali hufika kuangalia mandhari ya ziwa hili lililozungukwa na milima.



Hapa ndipo yalipokuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni ya wajerumani...
Majjid Mjengwa niambie hapa ni wapi?


Nyumba nyingi kijijini kwetu huonekana hivi.Hapa ni Tukuyu...wilaya ya Rungwe


Mashamba ya chai
Mlima Rungwe unavyoonekana kwa mbali
Wanajiografia nisaidieni....hii inaitwa nini vile?


Hili ndilo daraja laMungu lililoko mbele kidogo ya Kiwira.Hapo zamani daraja hili lilikuwa na maajabu ya pekee.Siwezi kueleza maajabu yote lakini hiko kidaraja unachokiona hapo hakijawahi kujaa hata siku moja hata mafuriko yawe makubwa kiasi gani...
Haya ndiyo maporomoko ya Kaporogwe...kwa kidhungu wanasema ..Kaporogwe falls
Mto Kiwira


Hivi karibuni nimepata maoni kupitia email na namba yangu ya simu kutoka kwa wadau mbalimbali wa blog hii kuwa wanapata shida sana katika taratibu za kutuma maoni yao.
Zifuatazo ni hatua muhimu katika kutuma maoni kupitia blog hii


1. Bofya kwenye sehemu iliyoandikwa maoni

2. ikishafunguka bofya tena sehemu iliyoandikwa post a comment

3.Ikifunguka anza kuandika maoni yako

4.Jaza maneno yanayoonekana katika kiboksi (word verification) kisha

5.Chagua sehemu iliyoandikwa anonymous kisha

6.Bofya sehemu iliyoandikwa "publish your comment "
Ukikamilisha taratibu hizi hapo maoni yako yatachapishwa moja kwa moja katika sehemu ya maoni.


Karibu tena....




Mtangazaji wa radio ya watu...Tayana


Hapa nimepozi na mdau wangu

photo