Katibu Mkuu wa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abduwakil akizungumza na kuwapongeza wajumbe wa Kikao Kazi cha Uandaaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara yake wa mwaka wa fedha 2015/2016 katika kazi hicho kinachoendelea mjini Morogoro.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mwamini Malemi akitoa mwongozo wa majadiliano kwa Wakuu wa Idara, Maafisa Ununuzi, Maafisa Bajeti na Wakurugenzi Wasaidizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi baada ya kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Ununuzi kwa mwaka wa fedha 2014/2015 kutoka kwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi cha wizara hiyo Mapesi Manyama katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara wa mwaka wa fedha 2015/2016 kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro. Kushoto ni Kamishna wa Fedha wa Jeshi la Magereza Gaston Sanga aliyesimama ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mapesi Manyama.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Manyama Mapesi akitoa ufafanuzi wa taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Ununuzi kwa mwaka wa fedha 2014/2015 wa wizara hiyo, aliyoiwasilisha katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara wa mwaka wa fedha 2015/2016 kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro. Wa kwanza kutoka kulia walioketi ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mwamini Malemi katikati ni Kamishna wa Fedha wa Jeshi la Magereza Gaston Sanga akifuatiwa na Kamishna wa Lojistiki na Fedha wa Jeshi la Polisi Clodwig Mtweve.
Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi cha Jeshi la Polisi Asenga akitoa maelezo na kuwapitisha katika Sheria Mpya ya Ununuzi ya mwaka 2011 katika Taasisi za Umma wajumbe wa Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa mwaka wa fedha 2015/2016 wa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Mapitio hayo yamefanyika katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara wa mwaka wa fedha 2015/2016 kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro.
Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Usajili wa Vyama Marlin Komba katika wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya Kisheria kuhusu masuala ya Ununuzi katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wa mwaka 2015/2016 kinachowahusisha Maafisa Bajeti, Maafisa Ununuzi, Wakurugezi, Wakurugenzi Wasaidizi na Wakuu wa Taasisi zote za wizara hiyo kinachoendelea katika hoteli ya Oasisi mjini Morogoro , Wanaomsikiliza ni baadhi ya wajumbe wa kikao hicho kutoka Jeshi la Polisi na Uhamiaji.
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Haji Janabi akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya Kifedha yanayohusu Ununuzi katika Taasisi za Umma katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa mwaka wa fedha 2015/2016 wa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Kikao kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro.
Mrakibu Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Fane Kapinga akiwasilisha Mada kuhusu Uandaaji wa Mpango wa Ununuzi wa Mwaka wa Fedha wa 2015/2016 kwa kutumia Majedwali yaliyoainishwa na Wakala wa Ununuzi Serikalini (PPRA) katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wa mwaka 2015/2016 kinachowahusisha Maafisa Bajeti, Maafisa Ununuzi, Wakurugezi, Wakurugenzi Wasaidizi na Wakuu wa Taasisi zote za wizara hiyo kinachoendelea katika hoteli ya Oasisi mjini Morogoro.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lilian Mapfa akifuatilia kwa makini ufafanuzi wa Sheria Mpya ya Ununuzi ya mwaka 2011 katika Taasisi za Umma wakati Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi cha Jeshi la Polisi Mathew Asenga akitoa maelezo na kuwapitisha katika Sheria Mpya ya Ununuzi ya mwaka 2011 katika Taasisi za Umma wajumbe wa Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa mwaka wa fedha 2015/2016 wa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro.
Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Makame wa kwanza kutoka kulia akifuatiwa na Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji TRITA mjini Moshi John Choma na watatu kutoka kulia ni Kamishna wa Utawala na Fedha wa Idara ya Uhamiaji Piniel Mgonja wakimsikiliza kwa Makini Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Manyama Mapesi wakati akitoa ufafanuzi wa taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Ununuzi kwa mwaka wa fedha 2014/2015 wa wizara hiyo, aliyoiwasilisha katika Kikao Kazi cha Utayarishaji wa Mpango wa Ununuzi na Mpango Kazi wa wizara wa mwaka wa fedha 2015/2016 kinachoendelea katika hoteli ya Oasis mjini Morogoro.

photo , ,

0 Responses so far.