Moja ya mambo ambayo kijana wa leo anaweza kujivunia ni namna anavyoweza kushiriki kikamilifu katika mambo ya siasa. ni vema tukakumbuka kuwa hata mwasisi wa Taifa hili Mwalimu Julius Nyerere wakati wa harakati za kudai uhuru yeye pamoja na wapigania uhuru wengi wa afrika walikuwa bado vijana, wenye nguvu na hali ya pekee katika kupigania haki za wanyonge.
Kama vijana hawashiriki kikamilifu katika mambo ya siasa, siku moja watakuja kujikuta wametawaliwa na mtu wa Hovyo, mpumbavu na mwendawazimu, nchi zote zilizo huru duniani viongozi wake huchaguliwa kupitia michakato ya kisiasa, Mwalimu Nyerere aliwahi kusema ili nchi iendelee inahitaji vitu vinne navyo ni ardhi,watu, siasa safi na uongozi bora.
Ni vema tukatambua pia kuwa siasa sio chafu kwa asili yake bali kuna viongozi wachafu ndani ya siasa, hawa ndio wanaoichafua taswira nzuri ya siasa
hivyo basi......Ukiona vijana kama akina Mnyika, Tundu Lisu, Halima Mdee, David Silindi, Kafulila,Joshua Nassari na wengineo wengi wanapigania haki za wanyonge, usipowaunga mkono,ukiwapinnga sasa, nawe ukiwa mzee utapingwa pia
![]() |
| Mbunge mtarajiwa wa Morogoro mjini kupitia CHADEMA Bw. Amani Theophilus Mwaipaja ,anatarajia kuzindua KITABU chake tarehe 30/03/2013 mjini Morogoro,ambamo ndani yake kitakuwa mahususi kwa ajili ya SHUKRANI kwa wapenda maendeleo wote na wanaharati wote wa ukombozi wa wanyonge na pia waliokuwa nae bega kwa bega katika uchaguzi uliopita. Katika uzinduzi huo anatarajia kuzindua na blog yake na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni Kiongozi wa kitaifa wa CHADEMA. Kama unahitaji KITABU hicho ufanye mawasiliano mapema kwa simu: 0787 070 707 na 0714 559 910. |
![]() |
| Huu ni UMATI wa watu waliokuja kuhudhuria kampeni za JUBILEE katika mitaa ya Kapkatet, Bungoma na Homabay ,uchaguzi utakafanyika jumatatu tarehe 4/3/2013 |
![]() |
| Mwana dada akifurahia kampeni za upande wa JUBILEE ,akiwa amevaliwa vazi lenye jina la chama cha TNA ambacho Uhuru Kenyatta ndie anakiwania nacho urais wa Kenya Jumatatu Ijayo. Kwa hisani ya Wazalendo 25 Blog |
![]() |
| Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maalumu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia. |









---

STATEMENT BY H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AT THE SIGNING CEREMONY OF THE PEACE, SECURITY AND COOPERATION FRAMEWORK FOR THE DEMOCRATIC REPUBLIC OF CONGO (DRC) AND THE REGION,24TH FEBRUARY 2013, ADDIS ABABA, ETHIOPIA.
--
Wanakijiji nikumbusheni...mnyama huyu huwakilisha nnini kwenye hela yetu?
Unaweza kupagundua mahali hapa? hivi watu wa mipango miji wanajua madhara ya kuruhusu ujenzi wa namna hii?ebu wadau wasilisheni hoja maana kila nikikumbuka kile kilichotokea katika soko la mwanjerwa moyo wangu huruka kichurachura
Hili ndilo kundi la Acappella kutoka Africa ya kusini lijulikanalo kama Ladysmith black Mambazo.Kundi hili linaimba muziki wa asili bila kutumia vyombo vya muziki yaani akapela na lilianzishwa mwaka 1964 na kiongozi wa kundi hilo - wa kwanza kutoka kushoto mstari wa mbele ambaye anaitwa Joseph shabalala.
Kundi hili ni moja ya vikundi maarufu duniani vinavyoimba muziki wa acappella kutoka Africa na kwa taarifa yako limesafiri na kushirikishwa na waimbaji mbalimbali maarufu duniani. Sauti za kundi hili ndizo zinazosikika katika ile picha ya Eddie Murphy iliyotokewa kupendwa sana ya COMING TO AMERICA.kama hujawahi kuitazama nenda kaikandamize sasa hivi.
Jamaa hawa wako mbioni kuja nchini Tanzania kwa udhamini wa Nyanza Company Limited
Hii imekaaje?
Mwanamke wa shoka...unamkumbuka huyu?.....hata kama humkumbuki lakini amini kuwa siku hazigandi
Hii ndiyo njia inayoelekea kituo cha watoto yatima Simike jijini Mbeya.......Kituo cha Simike kimeanzishwa miaka 17 iliyopita, wadau naomba niwapeleke moja kwa moja mkajionee wenyewe mandhari ya huko ili tusaidiane kwa pamoja katika kuwasaidia hawa wadogo zetu.
Safari yangu kuelekea kinjia hiko juu ilianzia hapa
Mtoto huyu umuoneaye hapo alipo hasikii, haoni na wala haongei.
Ni mmoja wa watoto yatima wanaolelewa na kituo cha Simike jiji Mbeya.
Wema Sepetu? !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Wadau toeni maoni juu ya hili......mimi naona haikubaliki totally
Ni vitu vya kawaida ukiwa ughaibuni kutinga makoti kama haya....nimepozi na Frank Zacharia..Mkurugenzi wa Nyanza Company Limited
Wabongo wengi wamekuwa na kasumba ya kuogopa kutoa damu...hivi tatizo ni nini?ukosefu wa elimu au?Michuzi unasemaje?kama huogopi njoo
Afande Sele akiwa katika pozi ndani ya gari lililokuwa likitumiwa na tour ya wanaume halisi na ndege tunduni...jamaa anatisha sana katika utunzi wa mashairi yaliyokwenda shule....Kitururu unamzungumziaje mshikaji huyu?...toa hoja

















