Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd (wa pili kushoto) akiwa katika meza kuu pamoja na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI,Mh. Hawa Ghasia (kushoto),Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Mh. Said Meck Sadick (wa pili kulia),Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi,Prof. Joseph Sembojo (katikati) pamoja na Dkt. Remy Sietchiping kutoka UN-Habitat wakati wa Mkutano wa Kikanda uliojadili Ukuaji wa maisha ya baadae kwa miji ya Afrika,uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,Jijini Dar es salaam. Picha na Emmanuel Masaka,Globu ya Jamii.
 Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi,Prof. Joseph Sembojo akizungumza wakati wa ufunguzi Mkutano wa Kikanda uliojadili Ukuaji wa maisha ya baadae kwa miji ya Afrika,uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,Jijini Dar es salaam. 
 Muwakilishi kutoka Shirika la UN-Habitat,Dkt. Remy Sietchiping akifafanua jambo juu ya changamoto mbali mbali zinazoikabili miji mingi ya mikubwa Afrika Mashariki wakati wa Mkutano wa Kikanda uliojadili Ukuaji wa maisha ya baadae kwa miji ya Afrika,uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,Jijini Dar es salaam. 
 Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi,Prof. Joseph Sembojo akiteta jambo na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd wakati wa Mkutano wa Kikanda uliojadili Ukuaji wa maisha ya baadae kwa miji ya Afrika,uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,Jijini Dar es salaam.Katikati ni Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI,Mh. Hawa Ghasia. 
 Sehemu wa washiriki wakiw katika Mkutano wa Kikanda uliojadili Ukuaji wa maisha ya baadae kwa miji ya Afrika,uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,Jijini Dar es salaam.
 Mtoa Mada katika Mkutano huo,Prof. David Simon akizungumza jambo wakati Mkutano wa Kikanda uliojadili Ukuaji wa maisha ya baadae kwa miji ya Afrika,uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,Jijini Dar es salaam.
 Mmoja wa wadau wa Mkutano huo akichangia mada.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Kikanda uliojadili Ukuaji wa maisha ya baadae kwa miji ya Afrika,uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,Jijini Dar es salaam.
Picha ya pamoja.

Na Chalila Kibuda Makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd,amesema watu wegi waonaishi maeneo ya mijini katika Afrika na dunia nzima wanapata changamoto ambazo ni lazima ziainishwe katika kuweza kuzikabili.
Balozi Idd ameyasema hayo leo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kikanda uliowakutanisha viongozi na watunga sera kutoka nchi za Afrika Mashariki kuzungumzia changamoto za ukuaji wa miji na kushughulikia hali ya baadaye ya miji ya Afrika na jinsi gani tunataka kuishi mwaka 2050,uliofanyika katika ukumbi wa Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
‘’Maeneo ya mjini  katika Afrika yana  fursa lakini maeneo hayo yana changamoto kutokana na ukuaji wa uchumi pamoja na mwingiliano wa kijamii’’amesema Balozi Idd.
Amesema maeneo ya mijini na majiji ni vituo vya fursa za uchumi,Teknolojia na sehemu ya kubadilishana mawazo na uzoefu  na kufanya watu wa vijijini kuvutika zaidi wakiwemo vijana kukombilia mjini kwa ajili ya urahisi wa kupatikana kwa fursa pamoja na huduma mbalimbali.
Balozi Idd amesema watu wanaokwenda katika  majiji wanajifunza njia  mpya za kuishi na kufikiria jinsi ya kuendesha maisha yao kutokana na kuwepo hali hiyo majiji yanapambana dhidi ya umasikini na kuweka mikakati bora  ya kuendesha majiji hayo.
Aidha amesema kushindikana na uimara katika miji na majiji matokeo yake ni umasikini unaingia ,magonjwa na kuwepo hali hiyo inaleta maswali ambayo yanatakiwa kuangalia ni jinsi gani ya kuweza kuyatatua.
Nae Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi wa Afrika kwa Maendeleo Endelevu,Profesa Joseph Semboja amesema jukwaa hilo la leo ni kuangalia changamoto na fursa mbalimbali  zinazoletwa na ukuaji wa miji ya ukanda wa Afrika Mashariki  na jinsi ya viongozi wa Afrika wanavyoweza kukabiliana nazo kwa pamoja.

‘’Kuna changamoto na uwiano mkubwa wa ongezeko la watu Afrika na duniani kwa ujumla wanaoishi mijini na kusababisha msongamano na shinizo la nyumba ,ajira huduma za kijamii’’amesema Prof.Semboja.

photo , ,

0 Responses so far.