k
Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali ndugu Sabanitho Mtega amewaasa waandishi wa Habari kutumia Taasisi na Wataalam wa ofisi ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali katika kupata majibu sahihi yanayotokana na Uchunguzi unaofanywa na taasisi hiyo ili kuisadia jamii kupata majibu na taarifa iliyo sahihi kutoka kwenye ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali amesema kuwa ili waandishi wa habari waweze kuandika habari za uhakika ipo haja ya wanahabari hao kushirikiana kwa karibu na ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali na kwa kufanya hivyo watakuwa wameepuka tatizo la kuandika habari za kubahatisha.

Ndugu Mtega ameyasema hayo wakati akitoa ufafanuzi kwenye mafunzo kwa waandishi wa habari na wadau kutoka taasisi zisizo za serikali kwenye ukumbi wa Mikutano wa Wakala wa Maabara wa Mkemia Mkuu wa Serikali

photo

0 Responses so far.