Hawa ni moja kati ya watoto wengi waliotoka kufanyiwa.....kwa habari zaidi bofya hapa www.saharanvibe
Hili ni ziwa masoko..ni moja kati ya maziwa machache yenye maajabu na historia ya pekee kama ile ya Ziwa kisiba....watu mbalimbali hufika kuangalia mandhari ya ziwa hili lililozungukwa na milima.
Mashamba ya chai
Mlima Rungwe unavyoonekana kwa mbali
Wanajiografia nisaidieni....hii inaitwa nini vile?
Hili ndilo daraja laMungu lililoko mbele kidogo ya Kiwira.Hapo zamani daraja hili lilikuwa na maajabu ya pekee.Siwezi kueleza maajabu yote lakini hiko kidaraja unachokiona hapo hakijawahi kujaa hata siku moja hata mafuriko yawe makubwa kiasi gani...
Haya ndiyo maporomoko ya Kaporogwe...kwa kidhungu wanasema ..Kaporogwe falls
Mto Kiwira
Hivi karibuni nimepata maoni kupitia email na namba yangu ya simu kutoka kwa wadau mbalimbali wa blog hii kuwa wanapata shida sana katika taratibu za kutuma maoni yao.
Zifuatazo ni hatua muhimu katika kutuma maoni kupitia blog hii
1. Bofya kwenye sehemu iliyoandikwa maoni
2. ikishafunguka bofya tena sehemu iliyoandikwa post a comment
3.Ikifunguka anza kuandika maoni yako
4.Jaza maneno yanayoonekana katika kiboksi (word verification) kisha
5.Chagua sehemu iliyoandikwa anonymous kisha
6.Bofya sehemu iliyoandikwa "publish your comment "
Ukikamilisha taratibu hizi hapo maoni yako yatachapishwa moja kwa moja katika sehemu ya maoni.
Karibu tena....
Hapa ni uwanja wa mpira sokoine ambapo wanaume halisi walifanya makamuzi ya kufa mtu.Afande sele anaonekana kwa mbali akiwapag....mashabiki
Mashabiki
Rais Joseph kabila siku alipofunga pingu za maisha...kaka michuzi umeiona hii?jina siwatajii..ila atakayelipatia nitampa zawadi
Magari mbalimbali yakielekea eneo la chuo kikuu Dar kwa ajili ya kubeba mizigo ya wanafunzi.
Picha na Issa Michuzi.
Wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam wakifungasha vilago baada ya kutolewa kwa tamko la kuondoka chuoni hapo baada ya mgomo wa kuingia darasani ili kuishinikiza serikali kutoa asilimia 100 kkwa hela ya field.
Mwanamuziki Ray C katika katika pozi
Salama Jabri...mtangazaji wa Kituo cha East Africa radio na Tv,mwana Dada huyo ni mmoja kati ya wadau wakubwa wa maendeleo ya muziki wa bongo fleva hapa nchini.
Jacline.......siku hizi amekuwa mwanamuziki wa......
Mchungaji Mtani...ambaye ni askofu wa kanisa la waadventista wasabato nyanda za juu kusini.
Mandhari ya chuo cha ufundi veta-mbeya yanavyoonekana
Kuna mdau ameniomba nimtumie picha zinazoonesha sura ya jiji la Mbeya kupitia Blog hii.
Hapa ni sehemu ya mnara kama unaelekea Hospitali ya taifa ya Rufaa Mbeya Kwa mbali ni round about kama unashuka kwenda stend kuu ya mabasi Mbeya
Safu za milima ya mbeya zikionekana kwa mbali
Jinsi soko la Mwanjelwa lilivyoungua
Baadhi ya watu wakishuhudia jinsi moto ulivyolitafuna soko la mwanjelwa huku wengine wakijaribu bahati zao kwa kufukuafukua hapa na pale.
Siku soko la mwanjelwa lilipokumbwa na zahama ya moto..kama ilivyo kawaida yetu...matukio ya hatari kama haya yanapotokea huwa hatubaki nyuma katika kushuhudia...ingawa ilikuwa ni usiku lakini watu kibao kutoka pande mbalimbali za jiji la mbeya walikusanyika kama unavyowaona hapa
Remigius Komba a.k.a Reyme K -Chief photographer wa Blog hii akiwaza kwa makini jinsi ya kuweza kuiboresha zaidi blog hii kwa picha zenye ubora na kiwango cha hali ya juu.Mshikaji ni mwanafunzi wa mwaka wa pili Digrii ya sheria chuo kikuu Mzumbe.
Sio siri jamaa anatisha sana katika maswala ya photos...michuzi upo?ana ma skilz kibao katika maswala ya production za muziki,picha na kompyuta.
Kwa taarifa yako...picha zote unazoziona humu ni kazi ya mikono yake Reyme K.
Upendo Merere a.k.a-Perlon mmoja wa wadau wakubwa wa Blog hii akiwa katika pozi wakati akitoka katika kikao cha wanafunzi watokao mikoa ya nyanda za juu kusini kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo kikuu Mzumbe-Mbeya Campus.
Jeneza liliobeba mwili wa marehemu.Marehemu Rajabu Tenga alikuwa pia mtumishi wa jeshi la polisi. (Usalama wa Raia). alifariki katika harakati za kuwaokoa wananchi na wanafunzi wenzake katika tukio la ujambazi lililohusisha kutupiana risasi kati ya majambazi na polisi.katika harakati hiyo ndipo jambazi moja lilipompiga risasi ya kichwa iliyopoteza maisha ya mwenzetu katika hospitali ya rufaa mbeya. (picha na Rayme A..K)
Wanafunzi wakiwa wamejipanga tayari kwa kuupokea mwili wa marehemu Tenga ...waliovaa jezi ni baadhi ya wachezaji wenzie wa mpira wa miguu enzi za uhai wake.
Gari la polisi lililobeba mwili wa marehemu likionekana kwa mbali likiingia katika viwanja vya chuo kikuu Mzumbe Mbeya - kampas
Mwili wa marehemu ukiingizwa chuoni na kikosi maalum cha ubebaji kilichoteuliwa kwa ajili ya kazi hiyo.
Wabebaji
Mwili ukishushwa na kuwekwa katika meza maalum
Tarehe 13/01/2007 Mzumbe brothers tukiwa katika kanisa la Mbeya Mjini tulipoalikwa kama kikundi katika tamasha lililofanyikia kanisani hapo
Wa kwanza kutoka kushoto ni Berius-anaimba sauti ya tatu
Marehemu Tenga wa pili kutoka kushoto-anaimba sauti ya nne
Mimi wa tatu niliyevaa batik na Magesa masige .
Hapa tuko katika ukumbi maarufu jijini Mbeya ujulikanao kama Dhandho tulipoalikwa kusindikiza uzinduzi wa kwaya ya kanisa la wasabato Mbeya Mjini.Mwenye suti ni mlezi wa chama cha wanafunzi wa kisabato Kampas ya Mbeya
Hapa marehemu Tenga akiwa na mchumba wake ambaye nae ni mwanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe Mbeya Kampas......pole sana Dada Alavuya...mungu akupe uvumilivu. (Picha zote na Remigius A.K-Ambaye ndiye chif photographer wa blog hii)
Kwa mbali Turubai likionekana...wanafunzi wakiwa katika majonzi makubwa baada ya kupotelewa na mwanafunzi mwenzao...Rajabu Tenga aliyeuawa na majambazi jana jioni baada ya majambazi hayo kuvamia supamaket iliyoko karibu na chuo kikuu Mzumbe Mbeya campas.
WAOMBOLEZAJI
Belius na Mimi Tukiwa katika hali ya huzuni baada ya kupotelewa na mwimbaji mwenzetu (marehemu Tenga) tuliyekuwa tukiimba nae pamoja katika kundi la A cappella la Mzumbe Brothers.Marehemu Tenga alikuwa akiimba sauti ta nne (bez)
Huzuni ikiwa imetawala katika msiba...hapa wanafunzi wanasikiliza maelezo kutoka kwa mawaziri wa serikali ya wanafunzi (hawapo pichani)




