Msanii Mkongwe wa Luninga na Vichekesho nchini Tanzania Asha Boko anategemea kuachia Video yake ya Kibonge Mnene mwisho wa mwezi huu. Video hiyo ambayo Audio yake ilifanyika katika Studio ya Kwanza Records iliyopo Morogoro imetayarishwa na Fasdo Video.Kwanza Records ni moja ya studio bora nchini Tanzania ambayo imekuwa ikisaidia kuinua vipaji vy muziki wa Bongo Fleva. Kwa wale wanaokumbuka Kwanza Records kwa mara ya Kwanza iliweza kumtambulisha Msanii Kitale aliyomshirikisha Marehemu Sharo Milionea iitwayo Hili Dude Noma.

Akiongea na Timu ya Mwaipaja Blog, Asha Boko amesema kuwa wadau wa Muziki wa Bongo Fleva wakae mkao wa kula kwakuwa amefanya mambo makubwa ndani ya Video hiyo.Asha Boko ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kufanya naye kazi ikiwemo filamu, movie na Bongo Fleva.

Kwa watakaohitaji kuwasiliana na Asha Boko wawasiliane nae kwa namba yake ya mkononi ambayo ni 0754 273904 ila wasibip wala kumwomba Vocha

photo

0 Responses so far.