Msemaji wa Kamati ya Mazishi ya Marehemu Albert Mangwea ambaye pia ni Director kutoka Visual lab Bw Adam Juma akielezea ratiba ya Shughuli nzima ya Mazishi itakavyokuwa mara baada ya zoezi la kutoa heshima za mwisho zitakapomalizika
 Baadhi ya Wasanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Wa Kwanza Kabisa ni Mkoloni akifuatiwa na Madee ambaye ni wa Tatu kutoka Mbele wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Marehemu Albert Mangwea
 Msanii Wa Muziki wa Kizazi Kipya Nasibu Abdul almaarufu kama Diamond akipita kutoa heshima zake za mwisho.
Baadhi ya Wasanii wa Fani mbalimbali pamoja na ndugu,jamaa na marafiki wakipita pembezoni mwa jeneza lililobeba mwili wa Marehemu Albert Mangwea na kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu Albert Mangwea leo katika viwanja vya leaders
 Msanii wa Muziki Keisha (aliyejifunga kiremba Cheupe) akifuatiwa na Noora wakiwa na nyuso za huzuni wakati wakipita kwaajili ya kutoa heshima zao za mwisho katika viwanja vya leaders
 Wasanii wa fani ya Maigizo hapa Nchini Mzee Magari (aliyeshika Koti jeusi) akifuatiwa na Msanii Natasha Pamoja na Monalisa wakipita kwaajili ya Kutoa Heshima zao Za mwisho kwa Marehemu Albert Mangweha leo katika Viwanja vya leaders
Baadhi ya Ndugu, Jamaa na Marafiki wakitoa Heshima za Mwisho
Jeneza lenye Mwili wa Marehemu  Albert Mangweha likiwa juu ya meza tayari kwa Wakazi wa Jiji la Dar Kuanza kutoa Heshima Zao za Mwisho katika Viwanja Vya Leaders.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Habari, utamaduni na Michezo Bi Lilian Bereko akitoa Salamu za Rambirambi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo leo katika viwanja vya leaders kabla ya Wakazi wa Jiji la Dar hawajaanza kutoa heshima zao za mwisho
Mmoja kati ya watu wa karibu wa Marehemu Albert Mangwea ambaye pia ni msanii wa muziki wa Kizazi kipya kutoka Katika Kundi aliloanzisha Marehemu Albert Mangwea Mez B akitoa historia fupi ya Kundi la Chamber Squade katika viwanja  vya leaders. Picha zote kwa hisani ya Lukaza Blog

photo ,

0 Responses so far.