Maduhu Emanuel (wa kwanza kushoto)ambaye pia ni katibu wa Kampuni ya Acappella Kwanza,Amani mwaipaja-Mwenyekiti wa Kampuni ya Acappella Kwanza (mwenye Batiki),Enos Kazuzu (wa tatu kutoka kushoto-mkuu wa mawasiliano)na Yusuph Mcharia (makam mwenyekiti-mwenye shati jeupe). Picha hii imepigwa mara tu baada ya kutoka kuzungumza na waandishi wa habari juu ya Tukio la tamasha kubwa la kihistoria la muziki wa A cappella litakaloshirikisha vikundi mbalimbali nchini Tanzania.


Hawa ni vijana wa Sonda ya Dlhu kutoka ukonga jijini Dar es salaam..vijana hawa wanaimba muziki wa A cappella ama muziki usiotumia ala za muziki.Ni vijana wadogo kiumri lakini hufanya mambo makubwa wawapo jukwaani.Wanaimba muziki wa Injili.Vijana hawa pia watakuwepo katika Tamasha la muziki wa Acappella litakalofanyika siku ya jumapili katika ukumbi wa Msimbazi centre.Vijana hawa uimbaji pia nyimbo za makabila mbalimbali.Wana albam moja ambayo itazinduliwa hivi karibuni.




1 Response so far.

  1. asante sana kaka mwaipaja kwa ukurasa wako huu...mungu akusaidie ili uweze kutuletea habari mbalimbali zitakazokuwa zinajili huko ughaibuni.