Mbunge wa kuteuliwa, mh.James Mbatia, amegomea uteuzi uliofanywa na waziri mkuu, Mizengo Pinda na kutaja sababu tatu za kukataa kushiriki katika tume iliyoundwa kuchunguza matoke mabaya ya kidato cha nne ya mwaka 2012.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana,Mbatia alisema amegomea uteuzi huo kwasababu tatu.

Mosi ni kwamba hajapata barua rasimi ya uteuzi,lakini pia ana hoja bungeni ambayo haijafika mwisho na tatu haiungi mkono tume hiyo.

Wakati huo huo,taarifa ya waziri mkuu alioitoa jana wakati akitangaza wajumbe wa tume hiyo inaonyesha kuwa ufaulu umeshuka toka asilimia 89 mwaka 2005 mpaka ailimia 43 mwaka 2012.

Kwa maneno memgine, tangu Kikwete aingie madarakani ufaulu umeshuka toka asilimia 89 mpaka asilimia 43.

Source:Tanzania Daima online la tarehe 03/03/2013.

Updates:
Gazaeti la habari leo online nalo pia linaripoti ya kuwa katibu mkuu wa chama cha walimu Tanzania, CWT, bwana Ezekiel Oluoch, ambae nae ameteuliwa kuwa mjumbe wa tume hiyo nae amekata uteuzi huo kwa kwasilisha barua ya kujitoa katika ofisi ya waziri mkuu.

Pia,gazeti hilo limefafanua ya kuwa habari za uhakika zinasema mh. Mbatia alipigiwa simu na katibu mkuu ofisi ya waziri mkuu, bwana Penniel Lyimo, akachukue barua yake ya uteuzi kama wenzake lakini hata hivyo mh.Mbatia hakuitikia wito huo.

Source:Habari leo online
.


0 Responses so far.