WANACHAMA wa timu kubwa za Simba na Yanga wa mkoani hapa wamepokea kwa furaha uamuzi wa viongozi wawili wa Simba kujiuzulu nyazifa zao kwa sababu mbali mbali zikiwemo za mabingwa hao wa Tanzania bara kufanya vibaya kwenye ligi kuu ya Tanzania bara na ligi ya mabingwa Afrika.
Kufuatia hali hiyo baadhi ya wanachama wa timu hizo waliohojiwa kwa nyakati tofauti na Mtandao huu leo asubuhi walidai kwamba hatua hiyo huenda ukaondoa jinamizi la timu hiyo kufanya vibaya,wakidai kwamba viongozi wa timu hiyo ndio chanzo cha timu hiyo kufanya vibaya hivyo.
Takribani mwenzi mmoja sasa baadhi ya wanachama wa timu hiyo kote nchini walishinikiza viongozi wote wa timu hiyo kujiuzulu kwa madai kwamba wao ndio chanzo cha timu yao kufanya vibaya, miongoni mwa wanachama waliolipotiwa kushinikiza viongozi hao kujiuzulu ni wanachama wa tawi lenye nguvu la Mpira Pesa mabpo baada ya tawi hilo  kushinikiza jambo hilo uongozi wa timu hiyo ulilipiga mkwara na baadae kutangaza kulifungia.
Baada ya kuona kelele zinazidi jana viongozi wawili wa timu hiyo makamu mwenyekiti Godfrey Nyange'Kaburu' na mwenyekiti wa kamati ya usajiri Zacharia Hans Pope walitangaza kujiuzuru nyazifa zao hizo kwa maandishi.
Kufuatia uamuzi huo wa kijasili uliofanywa na  viongozi hao wawili  wanachama wa yanga na simba mkoani hapa wamewaponmgeza viongozi hao kwa hayua yao yab kuweka maslai ya timu mbele huku wakiwaponda wiongzo wanaoendela kung'angania madaraka kwenye timu hiyo.
" Rage alikaririwa na redio moja akisema kwamba kufanya vibaya kwa Simba uongozi hauusiki,wahusika ni wachezaji na benchi la ufundi mimi ni mwanachma wa yanga laniki nasema kauli ile ya Rage ni ya kizushi,mfano mimi ni dereva wa hii taksi mtu kagonga gari langu  kwambele nakulihabirbu vibaya muhusika kanilipa pesa nyingi sasa mimi badala ya kununua taa za mbele nakwenda kununua taa za nyuma tena zinmgine haziwaki, pointi yangu ni kwamba uongzi wa Simba umeuza kwa pesa nyingi washambuliaji wawili Mbwana Samata na Emmanuel Okwi,badala ya pesa hile kununua wahsmbuliaji wao wamenunua kipa ambapo hitaji la Simba lilikuwa sio kwenye nafasi ya kipa Kaseja bado anauwezo,hivyo kumnunu kipa wa Uganda ambaye ni mgonjwa ni sana na kununua taa za nyuma ambazo haziwaki hivyo Rage kusema hausiki mimi na kataa"alisema Salum ambaye ni mwanachama wa yanga

Naye Bernard alipohojiwa alidai kwamba timu yao ya simba tatizo liko kwenye uongozi na kwamba binafsi anawapongeza sana Kaburu na Hans Pope kwa kuweka maslai ya klabu mbele kwa kujiuzulu kwa lengo la kuepusha migogoro isiyokuwa na tija kwenye timu yao.
" Rage anachong'angania ni kitu gani au hizo pesa za Okwi?  kumbukumbu zinanionyesha hali kama hii iliwakuta watani zetu yanga viongozi wote walitangaza kujiuzulu Nchunga peke yake aligoma kufanya hivyo mpaka alivyotishiwa kuvamiwa nyumbani kwake ndio akatangaza kujiuzulu kwa shingo upande hayo ndio anayotaka Rage "alisema

photo

0 Responses so far.